Mawakala Msaada wa M-pesa T-pesa A-money

Mawakala Msaada wa M-pesa T-pesa A-money

WATANZANIA WENGI TUNAJITENGENEZEA MAZINGIRA YA KUTAPELIWA/RUSHWA SISI WENYEWE. laini hiyo/hizo inatolewa BURE. kikubwa ni wewe kutimiza vigezo na masharti: kitambulisho chako, picha, leseni hai ya biashara, nambari ya utambuzi ya mlipa kodi (TIN-tax identification number). zaidi utaulizwa eneo lako la kazi na uwezo wako wa mtaji na/au uelewa wako kuhusu biashara husika. ukitumia middle-man (dalali) ujiandae kulipia atakachokuhudumia iwe direct/indirect.
*sio mbaya endapo utaamua kununua laini iliyotumika moja kwa moja toka kwa mteja endapo tu utakuwa tayari kubeba athari zake (bare risks). na hizi sio laini za kawaida kama tunavyosajiliwa mitaani kwa 500. itategemea na bei anayoitaka muuzaji na pengine soko la eneo ama yeye alinunuaje. yaweza kukuhitaji mamia kadhaa ya maelefu (100,000+)
*voda wanakupa line/cheap 2-ya stoo na ya kazi
[HASHTAG]#ukiamua[/HASHTAG] kuchukua USED IN USE. utaitambuaje kuwa ni till au laini ya kawaida? chunguza nyuma ya laini zote 2. zina chapa ya 64 sio 32.
*airtel na tigo wanatumia line 1
##kuwa huru kuuliza mengine nitakumegea kile nikijuacho. uliza hapa hapa sio pm ili na wengine wawe huru kuelewa au kunikosoa.
Ahsante hivi kwa kupata reseni ya biashar kima cha chini kwa biashara hii kinaweza kua shingapi na ukishapata TIN na leseni itachukua mda gani kupata lain
 
Ahsante sana Robert hv kwa kima cha chini cha kodi kwa biashara hii kinaweza kua kama. Shingapi na ukishapata TIN na leseni itachukua mda gani kupata lain maana kuna wakala mkuu aliniambia et unaweza chukua miez 3hujapata lain za uwakala ninkweli??
 
Mkuu ahsante sana ila naomba niulize swali la. Ziada hvi kama ushakamilisha tin na leseni ya biashara utatumia mda wa siku kama ngapi kupata hizo lain na bp T R A ukienda kukata resen ya biashara kama hii kima cha chini zaid cha kodi ni kama shingap na
TIN inatolewa na mamlaka ya mapato TRA bure kabisa. picha wanakupiga wao kwa mitambo iliyopo ofisini kwao, utachukuliwa taarifa zako binafsi kama majina kamili-lau matatu, alama za vidole, aina ya biashara/leseni za vyombo vya moto haikuhitaji kutaja biaaharam na hiyo hiyo ukiwatajia inaunganishwa na kutumika pia kibiashara. gharama zaweza kuwa nauli na malazi kuzifikia ofisi zao maana kwa mikoani sio kila ofisi (wilayani) zinatoa huduma hiyo. muda wa kupata tin inategemea na uhakika wa mtandao kwa siku husika na umakini/haraka ya mhudumu (afisa wa tra) na utaenda na nakala yako papo hapo.
 
Ahsante hivi kwa kupata reseni ya biashar kima cha chini kwa biashara hii kinaweza kua shingapi na ukishapata TIN na leseni itachukua mda gani kupata lain
leseni ya biashara hutolewa na halmashauri ya wilaya, manispaa au jiji (unapofanyia biashara) hii haina kiwango maalum. aghalabu hukadieiwa na maafisa biashara kulingana na miongozo ya TAMISEMI juu ya aina ya biashara.
**kama una duka tayari na ulikata leseni ya duka na unatarajia kuunganisha biashara ya pesa kwa jina hilo hilo SI LAZIMA kukata leseni mpya
 
leseni ya biashara hutolewa na halmashauri ya wilaya, manispaa au jiji (unapofanyia biashara) hii haina kiwango maalum. aghalabu hukadieiwa na maafisa biashara kulingana na miongozo ya TAMISEMI juu ya aina ya biashara.
**kama una duka tayari na ulikata leseni ya duka na unatarajia kuunganisha biashara ya pesa kwa jina hilo hilo SI LAZIMA kukata leseni mpya
Ahsante kwa mfano mtaji wako laki tatu unataka kufanya biashara tpesa m pesa unaweza kukadiliwa kodi kama kiasi gani
 
Ahsante sana Robert hv kwa kima cha chini cha kodi kwa biashara hii kinaweza kua kama. Shingapi na ukishapata TIN na leseni itachukua mda gani kupata lain maana kuna wakala mkuu aliniambia et unaweza chukua miez 3hujapata lain za uwakala ninkweli??
kama nilivyokueleza hapo juu, changamoto. kwa kuanza ni kuwa vibali/nyaraka zinatolewa na mamlaka anuai hivyo inakulazimu kufuata taratibu za ofisi husika. kuepuka hiyo mizunguko ndio maana wadau wanakuuzia zilizo tayari.
*leseni na tin kama umekamilisha vihezo vyao unarudi nayo nyumbani
*suala la kukutengenezea laini yako baada ya kujaza mkataba laweza kufika au kupungua muda huo uliotajiwa na wakala kulingana na jiografia ya eneo husika. mf. ujiji-kigoma, kyerwa-karagwe, mtukula-misenyi, nzaza-kaba ya ngara, namtumbo, newala na huko ndani ndani sana zoezi la kukusanya mikataba ikiyojazwa laweza kuchukua zaidi ya miezi 3 maana wahitaji/waelewa/wateja wapya ni wachache na inatumwa kwa idadi maalum (minimum yaweza kuwa 30pc) kabla wakala mkuu hajaituma makao makuu ili ichakatwe; sasa kokotoa jiografia yako
 
Ukienda kukata lesen wanakukadilua kodi hiyo kodi ukilipa. Ndo unapewa leseni au unapewa afu kod kulupa kwa mda wako
 
Ahsante kwa mfano mtaji wako laki tatu unataka kufanya biashara tpesa m pesa unaweza kukadiliwa kodi kama kiasi gani
masuala ya kukadiliwa kodi nadhani (sina uhakika) tra haina cha kukutoza hapo. labda leseni ya baishara kwa malaka ya halmashauri. tra mtakutana kwenye makato ya 10% za kamishen yako
 
Mkwamo wa vigezo vya kupata hizo line na Muda Wa kuzitengeneza unafanya wengi kuzikosa..... Vitu kama leseni na tin number wengi hawana.... Nipigie 0762208190 AU 0718978295 nikuuzie line ya M-Pesa na airtel money Gharama haizidi 250,000 kila moja...... Nicheck
 
Ukienda kukata lesen wanakukadilua kodi hiyo kodi ukilipa. Ndo unapewa leseni au unapewa afu kod kulupa kwa mda wako
kwenye vibanda vya kuuza pesa SINA uzoefu sana zaidi ya kuwahi kuifanya nikiwa ninaendesha shughuli za duka pia nimefanya kazi kwenye ofisi ya wakala mkuu ambaye ni super dealer wa m-pesa, airtel money na tigo pesa kwa zaidi ya mwaka lkn miaka ya 2013/14 huko na ninaongelea UZOEFU japo mjumbe mmoja hapo juu kaweka sawa kuwa cheaps/line za voda sasa inatolewa moja moja sio mbili km zamani. mfumo ninaoufahamu zaidi (sidhani kuwa umebasilika sana) ni wa zamani.
*TRA lazima watahitaji kodi chini ya kipengele cha MAPATO endapo utakuwa na mtaji mkubwa. wao wanakadiria mapato kulingana na mtaji wako unavyozungushwa kwa mwaka. upande huu, nina uzoefu wa kimashine cha kusaga na kukoboa mahindi. nalipia 150,000 kwa mwaka sawa na 75,000 miezi 6. na hii iko chini ya viwanda vidogo vidogo. leseni ya halmshauri ni 60,000 kwa mwaka. (hii hubadilika kulingana na miongozo ya TAMISEMI).
**kwa mtaji ulioutaja 300,000-400,000 sikushauri kufungua duka la biashara ya pesa peke yake. changanya na biashara zingine ili kuongeza mzunguko wa pesa. kwa kiwango hiko: kuna miamala/trans-actions hautazimudu. kwa mantiki hii (kama utakuwa na mtandao mmoja. utakuwa na cash 200,000 na salio 200,000. hapo akija mteja kutoa 210,000 hautamuhudumia uaacha aende kwa jirani. pia mf. zaidi ya 500,000/1,000,0000 kwenda juu na hizi ndizo zenye kamisheni kubwa.
**lakini ukiwa na biashara zingine zenye mtaji baki mfano 800,000 ni rahisi kujikopa mauzo na kumhudumia mteja. mwisho wa siku unarudisha kwenye fungu husika na hesabu ya pesa inaendelea kama kawaida.
 
Back
Top Bottom