Winniek
New Member
- Mar 16, 2018
- 4
- 2
Hello wanajukwaa, nimekuja ndugu yenu ninahitaji msaada wenu.
Mume wangu anasumbuliwa na vidonda vya tumbo kwa miaka sasa na ameshatumia dawa za kila aina. Changamoto ya sasa anasema anapata maumivu shingoni, kuna muda mdomo unakuwa mchachu kama ana homa.
Kaenda hospitali, kapigwa X-ray na ultrasound akaambiwa hana shida na gesi kwenye tumbo hamna. Akaenda kwa daktari wa koo na pua, akaambiwa ni gesi imepanda ndiyo maana inamletea shida hiyo.
Akapatiwa dawa aina nne kama si tano, lakini baada ya kumaliza dawa, ile hali imeanza tena. Leo kaenda hospitali, kaambiwa akamuone daktari wa mifupa.
Kiukweli hali yake inaniumiza sana kwa sababu anakuwa hana amani. Naomba msaada kama kuna mtu alishawahi pata changamoto hii au mwenye kufahamu ni nini alifanya au nini nifanye.
Asante.
Mume wangu anasumbuliwa na vidonda vya tumbo kwa miaka sasa na ameshatumia dawa za kila aina. Changamoto ya sasa anasema anapata maumivu shingoni, kuna muda mdomo unakuwa mchachu kama ana homa.
Kaenda hospitali, kapigwa X-ray na ultrasound akaambiwa hana shida na gesi kwenye tumbo hamna. Akaenda kwa daktari wa koo na pua, akaambiwa ni gesi imepanda ndiyo maana inamletea shida hiyo.
Akapatiwa dawa aina nne kama si tano, lakini baada ya kumaliza dawa, ile hali imeanza tena. Leo kaenda hospitali, kaambiwa akamuone daktari wa mifupa.
Kiukweli hali yake inaniumiza sana kwa sababu anakuwa hana amani. Naomba msaada kama kuna mtu alishawahi pata changamoto hii au mwenye kufahamu ni nini alifanya au nini nifanye.
Asante.