Maulizo juu ya ajira mpya 2020

Maulizo juu ya ajira mpya 2020

Maxmax72

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2018
Posts
578
Reaction score
1,054
Wakuu kwema?

Mimi ni kijana wa kiume muhitimu wa shahada ya elimu tangu 2017, kiukweli nimesota sana mtaani tangu kumaliza kwangu chuo nimefanya kazi za kila aina ili kujikimu lakini kiukweli sioni mwanga wa kubadilisha mfumo wangu wa maisha kwa hizi kazi nizifanyazo kwa sasa. Kwa jinsi hiyo, inabidi nipate kwanza ajira ili kuongeza mtaji.

Mhe Rais Magufuli siku za hivi karibuni akihutubia kwenye sherehe za chama cha walimu alihaidi hivi karibuni atatoa ajira za walimu, ajira hizi najua zitakuwa chache akilinganisha na sisi wahitimu na ndo maana siyo kila mtu atapata kwani hata mimi nimekuwa mhanga wa kutopata ajira hizi takiribani miaka mitatu, hivo kwa kulitambua hilo naomba kupitia kwenu wana JF nipate mtu atayenifanyia connection hasa kwa watu wa Tamisemi ili nami ajira zijazo nipate post sehemu yoyote nitakayo pangiwa nitaenda kufanya kazi.

Mimi ni mwalimu wa Biologia na Geographia. Kwa Ndugu yeyote atakaye wezesha mchakato huu ataombewa kwa sala na dua ili Mungu ampe maisha yenye heri duniani.

Asanteni sana.
 
Nimewahi kusikia wanaopewa kipaumbele ni Walimu wa Sayansi, naona wewe una biology.

Nimewahi kusikia wanaangaalia ukubwa wa GPA, Nyakati hizi zenye competition, sijui wewe GPA yako ipo vipi.

Kumbuka humu unaweza kupata msaada kwani wapo watu wenye nafasi zao, lakini pia kumbuka kuwa makini kwa kuwa MATAPELI WAPO.

Maxmax72
 
Nimewahi kusikia wanaopewa kipaumbele ni Walimu wa Sayansi, naona wewe una biology

Nimewahi kusikia wanaangaalia ukubwa wa GPA, Nyakati hizi zenye competition, sijui wewe GPA yako ipo vipi

Kumbuka humu unaweza kupata msaada kwani wapo watu wenye nafasi zao, lakini pia kumbuka kuwa makini kwa kuwa MATAPELI WAPO

Kipaumbele ni walimu wa Sayansi ila Mathematics na Physics Kwa mfano intek iloko mtaani wa hayo masomo ni wale walomaliza mwaka jana 2019, na katika ajira zinazokuja lazima waajiriwe wote.

Sababu moja kubwa ni kwamba wanahitajika zaidi ila wako wachache sana. Baada ya arts walimu ambao wako wengi sa hivi ni wa Biology na Chemistry.

Mtoa mada uko sahihi kwa hayo masomo unasafari ya kutopata ajira haraka kama hakuna connection .
Kila la heri tuu itokee hiyo bahati
 
Kama kweli hizo ajira zingekuwepo basi nafikiri wangekuwa tayar washatoa ili shule zikifunguliwa wanafunzi wakutane na Walimu ili kuziba hayo mapengo.

Tatizo la Serikali ya Magufuli ni kupenda kuongea sana. Unachotakiwa kufanya ni kuvuta subra mbona kila mtu akitafuta upenyo huo sijui itakuwaje huko.
 
Nimewahi kusikia wanaopewa kipaumbele ni Walimu wa Sayansi, naona wewe una biology

Nimewahi kusikia wanaangaalia ukubwa wa GPA, Nyakati hizi zenye competition, sijui wewe GPA yako ipo vipi

Kumbuka humu unaweza kupata msaada kwani wapo watu wenye nafasi zao, lakini pia kumbuka kuwa makini kwa kuwa MATAPELI WAPO
GPA yangu ni upper second 3.5
 
Kumbe hata CBG wanaongea lugha moja na mtu wa HKL! Mkuu unachotakiwa kuelewa ni kwamba maisha yamebadilika sana, jaribu kutafuta ajira hata shule za private.

Kujitolea ili kukuza taaluma yako ila hii utaifanya kama taaluma ya ualimu upo moyoni. Ila Kama ulisoma ualimu usoma ili ipate tu ajira maisha yasonge naomba ukomae na kazi zingine man.

Ila sema kweli wapo wengi mno huwa nakutana nao mpaka huruma japo n mm Ni msomi but nahangaika na mishe zilizo nje ya taaluma yangu.

Mungu akutanguliye mkuu
 
Ninavyojua mimi Walimu wa masomo ya Science wengi wao sio wote walikuwa wanajitolea kufundisha katika shule mbalimbali za serikali tangu January mpaka 17 March hawa ndio watakuwa KIPAUMBELE CHA HIZO AJIRA.
 
GPA yangu ni upper second 3.5
Serikalini hawaangalii hizo GPA,wanaangalia mahitaji, mfano kwa sasa mahitaji na kipaumbele ni Mathematics na Physics, then Chemistry & Biology, Private huangalia ufaulu wa vyeti but umahili wa masomo unayofundisha uwepo, kifupi ueleweke na ufaulishe kwa masomo unayofundisha.

Muone Samson Charles wa Eatv kwenye ukurusa wake wa Facebook juzi alitangaza hizo nafasi za ualimu wa masomo ya science. Kila la kheri
 
Nenda shule za vijijini ndani ndani huko ambako kuna uhaba wa walimu, jitolee kufundisha , baada ya muda, ongea na mwalimu mkuu awasiliane na afisa elimu wakuunge kwenye ajira
 
nenda shule za vijijin ndan ndan huko ambako kuna uhaba wa walimu, jitolee kufundisha , baada ya muda, ongea na mwalimu mkuu awasiliane na afisa elimu wakuunge kwenye ajira
Siku hizi mwenye kibali cha ajira za ualimu ni raisi na tamisemi wala siyo afisa elimu.
 
Ninavyojua mimi Walimu wa masomo ya Science wengi wao sio wote walikuwa wanajitolea kufundisha katika shule mbalimbali za serikali tangu January mpaka 17 March hawa ndio watakuwa KIPAUMBELE CHA HIZO AJIRA.
Hii program nadhali ilifanyika kwa shule za dar,na mm sikuwa na uwezo wa kuishi dar kufatana na gharama zake za maisha
 
Nakushukuru sana Mungu wa Mbinguni muumba mbingu na nchi. Hakika pamoja na kwamba ujana ulichangia lakini nakushukuru sa a kwa kuniepusha na hili janga la ualimu. Sijui leo hii ningekuwa mgeni wa nani
 
Back
Top Bottom