kinepi_nepi
JF-Expert Member
- Aug 16, 2007
- 869
- 235
ndugu wana JF bila kujali itikadi zetu na hisia, ningeomba tujadili kwa undani nini hasa kilitokea kwenye mauji yaliohusisha Barricks na wananchi wa Nyamongo.
Upande wa serikali unasema wale walikuwa wavamimizi waliotaka kuiba dhahabu. waliwazidi walinzi (Polisi) nguvu hivyo polisi iliwapasa kutumia silaha za moto.
Hapo hapo tunaona serikali hiyo hiyo ikijihusisha na mazishi kwa kununua majeneza na kudai kusaidia kufikisha miili kwa ndugu wa marehemu. Je huu ni utaratibu wa serikali?
Je uhusiano wa mwekezaji na wanakijiji ukoje. tatizo ni mwekezaji au serikali yetu. Mkataba wa Barricks North mara unasemaje? Je uchimbaji huu umewaongezea wananchi wa Nyamongo nafuu ya maisha au umekuwa kero na taabu.
Nini hasa wananchi wa Nyamongo walikuwa wanakifanya mpaka mauti ilipowakuta?
Naomba tujadili .
Upande wa serikali unasema wale walikuwa wavamimizi waliotaka kuiba dhahabu. waliwazidi walinzi (Polisi) nguvu hivyo polisi iliwapasa kutumia silaha za moto.
Hapo hapo tunaona serikali hiyo hiyo ikijihusisha na mazishi kwa kununua majeneza na kudai kusaidia kufikisha miili kwa ndugu wa marehemu. Je huu ni utaratibu wa serikali?
Je uhusiano wa mwekezaji na wanakijiji ukoje. tatizo ni mwekezaji au serikali yetu. Mkataba wa Barricks North mara unasemaje? Je uchimbaji huu umewaongezea wananchi wa Nyamongo nafuu ya maisha au umekuwa kero na taabu.
Nini hasa wananchi wa Nyamongo walikuwa wanakifanya mpaka mauti ilipowakuta?
Naomba tujadili .