Mauaji yanayoendelea ni dalili ya ugonjwa katika jamii

SUTAGI-

JF-Expert Member
Nov 9, 2018
269
511
Kumekuwepo na mfululizo wa matukio ya mauaji yanayoacha shaka kuhusu hali za afya ya akili zaa watu wanaotekeleza mipango hiyo.

Mauaji mengi yameacha simanzi kwa watu kwa kuwa wengi wao walioua, kujiua au waliouwa wazazi wao au wenza wao walionesha dalili ambazo jamii ilizitafsiri kama viashiria vibaya. Bahati mbaya viashiria hivyo hushtukiwa baada ya utekelezaji wa matukio.

Viashiria vingi vinavyojitokeza na kuelezewa huwa ni dalili za magonjwa ya akili. Lakini kwa kuwa jamii haina utambuzi wa kuoanishi dalili hizo na ugonjwa, inapotezea na mwisho wa siku tatizo likiwa sugu husababisha madhara makubwa.

Kama wananchi watapata elimu kuhusu magonjwa yanayoathiri afya ya akili huenda wakanusulu matukio mengi yanayotokea katika jamii.

Jitihadi za haraka zifanyike katika ngazi ya jamii kwa kuwapatia elimu.

Wahusika wote wa visa vya mauaji ya kutatanisha watapelekwa hospitali ya Mirembe ili kufanyiwa uchunguzi wa kuthibitisha hali ya afya ya akili ya watuhumiwa.

Endapo watakutwa na ugonjwa wa akili watapatiwa matibabu na kurudishwa uraiani. Kama utaratibu huu wa matibabu unafanyika ni wakati mwafaka sasa Wataalamu hao wasambae kwenye jamii kwa lengo la kutoa elimu itakayosaidia kung'amua wagonjwa wa akili na kupatiwa matibabu stahiki kabla ya majuto.

Wizara ya mambo ya ndani haitoweza kudhibiti haya mauaji bila kushirikiana na wizara ya afya.
 
Kuna mambo ambayo serikali inapaswa kusikiliza ushauri kuhusu mauaji haya yanayoendelea hivi sasa hapa nchini. Imesemekana kuwa watu wengi waliohusika na mauaji hayo wana magonjwa ya akili ; hata kama ni kweli wana hayo magonjwa, je tunajua chanzo cha hayo maradhi?

Kuna tabia ambayo imeshamiri sana katika jamaii yetu siku hizi ambayo serikali inaishabikia kwa kisingizo cha kuwa chanzo cha mapato yake ingawa athari zake kwa wananchi ni mbaya na za muda mrefu. Michezo hii ni kamali ambayo kwa jina lingine wanaita michezo ya KUBET. Hii michezo ya KUBET imeenea karibuni nchi nzima sasa, na imethibitika pasipo shaka na wanasayansi kuwa michezo hii kama yalivyo madawa ya kulevya ni ADDICTIVE; yaani mtu anayecheza sana hii michezo inakuwa hawezi kuacha kuicheza kwani anakuwa na hamu isiyomwisha kama inavyokuwa kwa wale walioathirika na pombe au madawa ya kulevya! Tofauti yake tu ni kwamba wakati walioathirika na madawa ya kulevya unaweza kuwatambua kwa muonekano wao lakini hawa walioathirika kwa kucheza sana kamali [ KUBET} huwezi kuwatambua kwa kuonekano wao bali kwa jinsi mchezo huo unavyoweza kubadirisha maisha yao! Wale wliothirika na kamali mara nyingi hufilisika na kwa vile hawawezi kujizuia kutokucheza huo mchezo hujikuta wanatafuta kila mbinu za kupata fedha za kuwawesha kuendelea na hue mchezo hivyo inabidi wajiingize kwenye wizi na uharifu wa aina mbali mbali!

Kwa jamii maskini kama ya kwetu ndio utasikia kijana amemuua mama yake kwa sababu ya shillings elfu mbili ambazo alimuomba mama yake na akanyimwa ; au mume amemuua mkewe kwa ugonvi wa fedha, yote hiyo inatokana na maradhi hayo ya addiction ya watu wengi siku hizi kwenda kwenye kuweka mikeka[ KUBET] ambako watu wengi wanapoteza fedha zao na hakuna ambaye mwishowe anafaidika na umaskini unazidi kukithiri!!

Kwa wale wafanya kazi kwenye taasisi za fedha na mabwana fedha kwenye halmashauri ndio utasikia wamekwapua fedha ili kwenda kukidhi haja /maradhi yao haya ya kucheza hizo kamali. Ingawa ni kweli kampuni hizo za kamali zinalipa kodi kwa Serikali ni ukweli usiofichika kuwa athari za kampuni/michezo hii kwa jamii yetu ni kuharibu uchumi wa jamii yetu kwa Watu kufirisika pamoja na nguvu kazi yetu kuharibiwa na haya maradhi ya ADDICTION to gambling! Serikali isiridhike na hizi kodi za muda mfupi at the expense ya madhara ya muda mrefu kwa nchi nzima. Kuna haja ya Serikali kufikiria upya kama kuna haja ya kweli ya kuwapa leseni hawa wanaochezesha michezo hii ya kamali nchini kwani wahanga wakubwa ni vijana wetu ambao mwishowe wanakuja kufanya uharifu kwa jamii inayowazunguka.
 
Kuna mambo ambayo serikali inapaswa kusikiliza ushauri kuhusu mauaji haya yanayoendelea hivi sasa hapa nchini. Imesemekana kuwa watu wengi waliohusika na mauaji hayo wana magonjwa ya akili ; hata kama ni kweli wana hayo magonjwa, je tunajua chanzo cha hayo maradhi?

Kuna tabia ambayo imeshamiri sana katika jamaii yetu siku hizi ambayo serikali inaishabikia kwa kisingizo cha kuwa chanzo cha mapato yake ingawa athari zake kwa wananchi ni mbaya na za muda mrefu. Michezo hii ni kamali ambayo kwa jina lingine wanaita michezo ya KUBET. Hii michezo ya KUBET imeenea karibuni nchi nzima sasa, na imethibitika pasipo shaka na wanasayansi kuwa michezo hii kama yalivyo madawa ya kulevya ni ADDICTIVE; yaani mtu anayecheza sana hii michezo inakuwa hawezi kuacha kuicheza kwani anakuwa na hamu isiyomwisha kama inavyokuwa kwa wale walioathirika na pombe au madawa ya kulevya! Tofauti yake tu ni kwamba wakati walioathirika na madawa ya kulevya unaweza kuwatambua kwa muonekano wao lakini hawa walioathirika kwa kucheza sana kamali [ KUBET} huwezi kuwatambua kwa kuonekano wao bali kwa jinsi mchezo huo unavyoweza kubadirisha maisha yao! Wale wliothirika na kamali mara nyingi hufilisika na kwa vile hawawezi kujizuia kutokucheza huo mchezo hujikuta wanatafuta kila mbinu za kupata fedha za kuwawesha kuendelea na hue mchezo hivyo inabidi wajiingize kwenye wizi na uharifu wa aina mbali mbali!

Kwa jamii maskini kama ya kwetu ndio utasikia kijana amemuua mama yake kwa sababu ya shillings elfu mbili ambazo alimuomba mama yake na akanyimwa ; au mume amemuua mkewe kwa ugonvi wa fedha, yote hiyo inatokana na maradhi hayo ya addiction ya watu wengi siku hizi kwenda kwenye kuweka mikeka[ KUBET] ambako watu wengi wanapoteza fedha zao na hakuna ambaye mwishowe anafaidika na umaskini unazidi kukithiri!!

Kwa wale wafanya kazi kwenye taasisi za fedha na mabwana fedha kwenye halmashauri ndio utasikia wamekwapua fedha ili kwenda kukidhi haja /maradhi yao haya ya kucheza hizo kamali. Ingawa ni kweli kampuni hizo za kamali zinalipa kodi kwa Serikali ni ukweli usiofichika kuwa athari za kampuni/michezo hii kwa jamii yetu ni kuharibu uchumi wa jamii yetu kwa Watu kufirisika pamoja na nguvu kazi yetu kuharibiwa na haya maradhi ya ADDICTION to gambling! Serikali isiridhike na hizi kodi za muda mfupi at the expense ya madhara ya muda mrefu kwa nchi nzima. Kuna haja ya Serikali kufikiria upya kama kuna haja ya kweli ya kuwapa leseni hawa wanaochezesha michezo hii ya kamali nchini kwani wahanga wakubwa ni vijana wetu ambao mwishowe wanakuja kufanya uharifu kwa jamii inayowazunguka.
uwo wivu sasa.
 
uwo wivu sasa.

Namuonea wivu nani sasa? Hao wajinga wanaofilisika kwa hiyo kamali? Wagonjwa kama wewe hamjitambui kwasababu you are addicted! Ndio maana unafikiri mnaonewa wivu, hapana tunawaonea huruma; you never win in gambling!!
 
Back
Top Bottom