Econometrician
JF-Expert Member
- Oct 25, 2013
- 15,797
- 28,458
Washukiwa watatu wa utekaji na mauaji ya watoto wa chini ya miaka 10 wilayani Njombe, kusini magharibi mwa Tanzania wamepandishwa mahakamani hii leo.
Watuhumiwa hao waliowekwa wazi kwa mara ya kwanza hii leo ni Nasson Kaduma, Joel Nziku na Alphonce Danda.
Wote wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Njombe.
Gazeti la Mwananchi linaripoti kuwa Nje ya mahakama hiyo ulinzi mkali wa polisi umeimarishwa na msafara wa watuhumiwa hao ukisindikizwa na magari sita ya polisi.
Washukiwa wa mauaji ya watoto Tanzania wapandishwa mahakamani