No research no right to speak, awali nilihofu kwamba pengine hii mada ingefutwa humu haraka sana baada ya kuiona bado inapumua naendelea na Part -2 ya Mauaji ya kikatili wanayofanyiwa wavuvi kanda ya ziwa, eneo la Chato Mganza kwenye kisiwa cha Rubondo.
Nina ushahidi 100% na Tayari hii Habari naiandaa ili kuifikisha kwenye vyombo vya Habari vya kimataifa ili Dunia ijue Tanzania ilikofikia kwa sasa.
Mandela aliwahi kuwaambia makaburu kuwa, "Huwezi kuua sauti zote, kila sauti moja unayoiua zinafufuka sauti elfu moja zaidi ".
Simulizi ya X inaliza na kuumiza mno, anadai kuwa wauaji wale si askari wa wanyama pori bali ni wanajeshi anaodai wana nasaba na taifa la Rwanda.
"Tumekamatwa mara nyingi mno na Watanzania wenzetu askari pori lakini walikuwa wakituachia na kutueleza kuwa tusirudie tena, lakini tulipokamatwa na wale wanajeshi, tulipelekwa sehemu zenye maiti nyingi na kisha tukaambiwa kuwa Hao ndio wenzetu waliopotea, kwa sababu mimi sijaoa Niliambiwa sina hasara kwa hiyo nishuhudie kwanza mauaji ya wenzangu ".
"Moto ulikokwa chini na wenzangu wakaambiwa wanabanikwa Kama jinsi ambavyo wao wamekuwa wakibanika Samaki, waliuawa huku naona kwa macho yangu, kisha nikaambiwa nenda kasimulie wenzako "
X anadai aliambiwa magereza yamejaa hivyo kuna maagizo toka juu wamalizwe kila wanapokamatwa.
Analia akidai Kama watu hawaamini basi waende wakachunguze na kubaini ukweli.
Habari hizi zimetapakaa pote lakini hakuna Chombo chochote cha Habari chenye uthubu wa kuandika.
Kwa sababu Damu ya mtu haipotei bure ni lazima Dunia ijue,na Mungu atajitwalia kisasi mwenyewe.
Hivi kosa la kuvua Samaki bila kibari adhabu yake ni kifo cha kikatili kiasi hicho?
Eeeh Mungu, sema na Tanzania.
Sent using
Jamii Forums mobile app