Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 359,898
- 828,496
#BREAKINGNEWS
Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha linawashikilia watuhumiwa watano kwa tuhuma za mauaji ya Askari Polisi, Omary Mnandi (30), aliyekuwa mkazi wa Jiji la Arusha.
Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Oktoba 12, 2025, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, SACP Justine Masejo, amesema tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia leo katika Baa ya Simaloi iliyopo eneo la Kaloleni, Jijini Arusha.
Kamanda Masejo amesema watuhumiwa hao wanadaiwa kumshambulia Mnandi na kumsababishia majeraha makubwa sehemu mbalimbali za mwili wake, hali iliyosababisha kifo chake alipokuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mount Meru.
Ameeleza kuwa uchunguzi wa awali umebaini chanzo cha tukio hilo ni ugomvi uliotokana na ajali ndogo ya magari, baada ya gari la marehemu lenye namba T.402 CNC kugonga gari jingine lenye namba T.734 AXR linalomilikiwa na mmoja wa watuhumiwa, jambo lililosababisha kutoelewana na hatimaye kushambuliwa.
Kamanda Masejo amesema Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo na kwamba watuhumiwa watapelekwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha linawashikilia watuhumiwa watano kwa tuhuma za mauaji ya Askari Polisi, Omary Mnandi (30), aliyekuwa mkazi wa Jiji la Arusha.
Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Oktoba 12, 2025, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, SACP Justine Masejo, amesema tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia leo katika Baa ya Simaloi iliyopo eneo la Kaloleni, Jijini Arusha.
Kamanda Masejo amesema watuhumiwa hao wanadaiwa kumshambulia Mnandi na kumsababishia majeraha makubwa sehemu mbalimbali za mwili wake, hali iliyosababisha kifo chake alipokuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mount Meru.
Ameeleza kuwa uchunguzi wa awali umebaini chanzo cha tukio hilo ni ugomvi uliotokana na ajali ndogo ya magari, baada ya gari la marehemu lenye namba T.402 CNC kugonga gari jingine lenye namba T.734 AXR linalomilikiwa na mmoja wa watuhumiwa, jambo lililosababisha kutoelewana na hatimaye kushambuliwa.
Kamanda Masejo amesema Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo na kwamba watuhumiwa watapelekwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.