Mauaji Geita: IGP atoa sh10m

Mauaji Geita: IGP atoa sh10m

big_in

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2013
Posts
4,507
Reaction score
1,105
MAUAJI GEITA: IGP E. Mangu leo ametangaza bingo ya Sh10m kwa mtoa taarifa zitakazosaidia kukamatwa kwa watu waliovamia kituo cha polisi jana usiku mkoani Geita.
 
Ki ukweli wanainchi tusaidie kuwabaini. Majambazi kama wanajitawala hivi!
 
Nami naongeza m10 jumla zitakuwa 20m kufanikisha zoezi hilo. Karibuni wadau wengine kwenye harambee hii.
 
MAUAJI GEITA: IGP E. Mangu leo ametangaza bingo ya Sh10m kwa mtoa taarifa zitakazosaidia kukamatwa kwa watu waliovamia kituo cha polisi jana usiku mkoani Geita.
isije kuwa ni majambazi wa burundi na rwanda. Geita imetawaliwa sana na wahamiaji haramu, ni wengi sana na wale waliokuwa wamefurushwa na operation kimbunga wamerudi wote. operation kimbunga inatakiwa irudi tena ili kusafisha kabisa na wanajeshi washirikishwe kwenye ulinzi na upelelezi wa mambo hayo huko ushirombo. ukitoka ushirombo hadi ufike nyakanazi unashukuru Mungu. kwa wale tuliotoka maeneo hayo tunaua hali halisi ilivyo. majambazi mengi yanatoka burundi na rwanda, na hata wale wa tz maeneo mengine makao yao makuu huwa ni mkoa wa geita.
 
Kama vituo vinavamiwa hivi je wananchi tupo katika hali gani?, polisi acheni kubweteka...
 
Twende mbele na kurudi nyuma, hv jamani huwa hamuwaoni askari jinsi wanavyokaa kizembe zembe huku wakinywa kahawa kwenye benchi na wakiwa hawana silaha na buti wamevua wamevaa kandambili?? Jamani huwa hamuwaoni? Mbona hili hamlisemi? Sasa unategemea nini? Tukio la kuuwawa askari ni uzembe wao, majambazi matano wao sita, tena wapo kituoni lakini hawakuwa na silaha wameridhika!! Wasipobadilika watauwawa sana, uhamiaji nao wamekuwa wala rushwa wakubwa, wahamiaji haramu hadi wanaingia nchini wanafanya kazi bila kugundulika, rejea makomandoo wa nepal, unategemea nini hapo?
 
hao ni warundi tu milion kumi mrundi utampata wapi!!!
 
Pesa za kutoa zawadi tunazo lakini pesa kwa ajili ya kujikinga na majanga kama hayo kwa kuimarisha ulinzi wa mipaka na kuweka doria za uhakika ili kuzuia maafa hazipo
 
Twende mbele na kurudi nyuma, hv jamani huwa hamuwaoni askari jinsi wanavyokaa kizembe zembe huku wakinywa kahawa kwenye benchi na wakiwa hawana silaha na buti wamevua wamevaa kandambili?? Jamani huwa hamuwaoni? Mbona hili hamlisemi? Sasa unategemea nini? Tukio la kuuwawa askari ni uzembe wao, majambazi matano wao sita, tena wapo kituoni lakini hawakuwa na silaha wameridhika!! Wasipobadilika watauwawa sana, uhamiaji nao wamekuwa wala rushwa wakubwa, wahamiaji haramu hadi wanaingia nchini wanafanya kazi bila kugundulika, rejea makomandoo wa nepal, unategemea nini hapo?


Askari wetu ni walinzi wa viongozi na siyo raia, raia wakienda wanashida kituoni mpaka watoe chochote kwahiyo inafika wakati wanajisahau wanakaa kibiashara zaidi na kusahau majuku yao, utashangaa leo vituo vingi vitaimarisha ulinzi lakini baada ya week moja tu wameshasahau wapo kama vile hawakuvamiwa
 
isije kuwa ni majambazi wa burundi na rwanda. Geita imetawaliwa sana na wahamiaji haramu, ni wengi sana na wale waliokuwa wamefurushwa na operation kimbunga wamerudi wote. operation kimbunga inatakiwa irudi tena ili kusafisha kabisa na wanajeshi washirikishwe kwenye ulinzi na upelelezi wa mambo hayo huko ushirombo. ukitoka ushirombo hadi ufike nyakanazi unashukuru Mungu. kwa wale tuliotoka maeneo hayo tunaua hali halisi ilivyo. majambazi mengi yanatoka burundi na rwanda, na hata wale wa tz maeneo mengine makao yao makuu huwa ni mkoa wa geita.

Mkuu hao majambazi kutoka nchi za jirani lazima wawena watu kutoka tz mgeni hawazi kuja bila mwenyeji
 
Back
Top Bottom