Matusi na Ubabe Bungeni: Behind the scene

Matusi na Ubabe Bungeni: Behind the scene

Ni Mkakati wa makusudi kabisa, imeandaliwa na kuratibiwa na Chama kikongwe kwa madhumuni ya kutafuta sababu za kuwahadaa wananchi wakubaliane na mpango wa kusitisha kurusha matangazo ya bunge LIVE (moja kwa moja).

Kwa Hiyo wakisitisha Bunge ndio

1. Matusi yatakuwa halali huko Mafichoni?
2. Matusi yatapungua

Ni suluhisho la Kijuha sana
 
Hapana! Hakuna mpango mkakati wowote ulioandaliwa.
Ukweli ni kuwa uwelewa wa siasa za vyama vingi ndiyo unaochangia mabishano yasiyokuwa na msingi na hatimaye kuishia kwenye kutukanana. Wabunge wa CCM wamepoteza dira. Wamehama kabisa kutoka kuwa chombo cha kuisimamia serikali na kuwa chombo cha kuitetea serikali. Badala ya Mawaziri kuitetea serikali sasa majibu ya utetezi yanatolewa na wabunge wa CCM. Kiti cha Spika wa Bunge badala ya kuwa mwamuzi kimekuwa kiti cha kutetea makosa ya serikali na wabunge wa CCM wanaokosea. Tabia hii imejenga usugu kwa wabunge wote wa upinzani na kutaka kujihami dhidi ya jambo lolote hata pale ambapo wana makosa ya kiufundi. Kumejengeka tabia ya kushambulia na kujilinda dhidi ya mashambulizi. Bunge limepoteza mwelekeo badala kuwa chombo cha majadiliano kimekuwa chombo cha mashambulizi na kujibu mapigo.
Tuone mfano mdogo: Mbunge wa CDM anailalamikia Serikali kuwa haina utawala bora sababu watu wasio na makosa, wanatekwa, wanapigwa, na kuteswa vibaya chini ya serikali yenye jukumu la kulinda usalama wa kila raia. Mbunge wa CCM anainuka kutetea hatua hii. Je; huyu Mbunge anatetea kama serikali au Mbunge? J;hilo ndilo jukumu lake lililompeleka bungeni.
Mfano mwingine ni pale Mbunge wa chama fulani anatoa lugha ya matusi mbeleya kiti cha Spika, watanzania wote wakimsikia kupitia Luninga zao, anachwa hivi hivi, lakini Mbunge wa upinzani anapoomba mwongozo wa Spika kuhusu kanuni anaambiwa atoke nje ya Bunge. Hapa ni wazi kuna mazingira matumizi mabaya ya kiti.
Kwa asili binadamu hawapendi kupuuzwa kudharauliwa wala kuonewa. Upo ushahidi wa kitafiti kuwa mtu ukimdharau hata angalikuwa ni mtoto wako atakurudishia dharau pia. Nina hakika Kiti cha Spika kikisimamia kanuni za Bunge kwa haki, Bunge litarudi kwenye mstari na wabunge wa CCM wakiongea kwa heshima kwa nia kutimiza majukumu yao yaliyowapeleka bungeni wataheshimiwa lakini pia bunge litaheshimiwa.
Ni Mkakati wa makusudi kabisa, imeandaliwa na kuratibiwa na Chama kikongwe kwa madhumuni ya kutafuta sababu za kuwahadaa wananchi wakubaliane na mpango wa kusitisha kurusha matangazo ya bunge LIVE (moja kwa moja).
 
Paliamentary proceedings must be televised live
wakisitisha tu.....
the revolution would be televised live.
 
Bunge ni sehemu ya burudani kama vile : FUTUHII,PUPPET SHOW, Orijino komedi, Vioja mahakamani na sasa BUNGE kweli usikose hasa akiwa naibu spika ushabiki mbele kanuni nyuma sijui kama mkuu au m-sure anaangaliaga.....aah!aah..teh..teh
 
Wabunge wengi wana dirty mind. Ndo maana hayo matusi wanayoporomosha hawachukui hata sekundi kuyafikiri maana yapo kichwani kwao na just a matter of time kabla hawajaanza kuyaporomosha. Na usidanganyike, hata wakiwa mtaani ni watu wa matusi matusi tu!
 
Ni Mkakati wa makusudi kabisa, imeandaliwa na kuratibiwa na Chama kikongwe kwa madhumuni ya kutafuta sababu za kuwahadaa wananchi wakubaliane na mpango wa kusitisha kurusha matangazo ya bunge LIVE (moja kwa moja).
Nzenzu kama essence yake ni kutorusha LIVE bunge basi lengo lake mbona liko wazi? Wameshagundua kuwa wanachemka na hiyo inawapa opposition credit sasa hawataki watu waone maana siyo rahisi kupiga propaganda kwa kitu ambacho Wananchi wanaona na kusikia!!
 
Nzenzu kama essence yake ni kutorusha LIVE bunge basi lengo lake mbona liko wazi? Wameshagundua kuwa wanachemka na hiyo inawapa opposition credit sasa hawataki watu waone maana siyo rahisi kupiga propaganda kwa kitu ambacho Wananchi wanaona na kusikia!!

Akili za kina mwigulu hazina tofauti na matope!
 
Ndugu let me enlight you, In your posting what you r recommending is the DOOMS DAY, Very unfortunately although i am not affiliated to any Party, whether u believe me or not, Dr.Slaa is never the right choice, nor will he ever be, God forbid that this man ever has any chance to lead this blessed country. He is part of the MOTHER OF ALL EVIL, In Chadema there are many potential leaders 100 times better than, the CHEATING PRIEST who betrayed god just for LUST, What will he do when he has a whole nation at his disposal. While Chadema has people like MBOWE, ZITTO, HALIMA nk, why this guy who still thinks he is at the pulpit he dicrerated. Please stop this foolishness

What ever you may say leadership goes with maturity,and character we need a strong leader in tanzania than never before, the country is rotten and it requires a full overhaul
 
Ndugu let me enlight you, In your posting what you r recommending is the DOOMS DAY, Very unfortunately although i am not affiliated to any Party, whether u believe me or not, Dr.Slaa is never the right choice, nor will he ever be, God forbid that this man ever has any chance to lead this blessed country. He is part of the MOTHER OF ALL EVIL, In Chadema there are many potential leaders 100 times better than, the CHEATING PRIEST who betrayed god just for LUST, What will he do when he has a whole nation at his disposal. While Chadema has people like MBOWE, ZITTO, HALIMA nk, why this guy who still thinks he is at the pulpit he dicrerated. Please stop this foolishness

Ukiona mtu hamkubali Dr.W.P.Slaa,lazima iko tatizo,kama siyo GAmBa!?
 
Yan hivi ni tunaondolewa umakini wa kulifuatilia bunge n la bajeti lkn n nani ambaye ametangaza bajeti ya ofisi ya waziri mkuu kwa hyo tusipokuwa makini unajikuta uelewi nn knaendelea MJENGONI.
 
Back
Top Bottom