Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Jan 29, 2021
572
2,553
Unaelewa nini ukiambiwa umeze dawa kutwa mara tatu?

Maduka mengi ya dawa pamoja na hospitali zetu hutumia lugha hii kimakosa pasipo kuwaelewesha vizuri wagonjwa. Kwa kiasi kikubwa, huwafanya wagonjwa wasitumie vizuri dawa wanazopewa.

Siku moja ina saa 24, kwa kuzingatia mgawanyiko sawa wa vipindi vya kumeza dawa, mgonjwa hupaswa kuzimeza kila baada ya masaa 8. Hivyo, badala ya kusema dawa imezwe kutwa mara tatu, ni vizuri ikisemwa kuwa imezwe mara tatu ndani ya saa 24, au kila baada ya masaa 8.

Vivyo hivyo kwa kutwa mara moja, au kutwa mara mbili. Mgonjwa anapaswa kuambiwa ameze mara moja tu kwa siku, au mara mbili kwa siku kila baada ya masaa 12 mtawalia.

Watoa huduma wanapaswa kuhakikisha kuwa wanatoa maelezo kwa usahihi, pia wagonjwa wanapaswa kufuata maelekezo hayo ili kuongeza ufanisi na kupunguza madhara ya dawa husika.

Neno kutwa huleta maana isiyo sahihi kimantiki, huwafanya wagonjwa wameze dozi nzima ya dawa kwa mgawanyiko wa saa 12 pekee yaani asubuhi, mchana na jioni pasipo kukumbuka kuwa siku nzima huhusisha mjumuiko wa saa 24.
 
Unaelewa nini ukiambiwa umeze dawa kutwa mara tatu? Au ukiambiwa umeze asubuhi, mchana na jioni?

Maduka mengi ya dawa pamoja na hospitali zetu hutumia lugha hii kimakosa pasipo kuwaelewesha vizuri wagonjwa. Kwa kiasi kikubwa, huwafanya wagonjwa wasitumie vizuri dawa wanazopewa.

Siku moja ina saa 24, kwa kuzingatia mgawanyiko sawa wa vipindi vya kumeza dawa, mgonjwa hupaswa kuzimeza kila baada ya masaa 8. Hivyo, badala ya kusema dawa imezwe kutwa mara tatu, ni vizuri ikisemwa kuwa imezwe mara tatu ndani ya saa 24, au kila baada ya masaa 8.

Vivyo hivyo kwa kutwa mara moja, au kutwa mara mbili. Mgonjwa anapaswa kuambiwa ameze mara moja tu kwa siku, au mara mbili kwa siku kila baada ya masaa 12 mtawalia.

Watoa huduma wanapaswa kuhakikisha kuwa wanatoa maelezo kwa usahihi, pia wagonjwa wanapaswa kufuata maelekezo hayo ili kuongeza ufanisi na kupunguza madhara ya dawa husika.

Neno kutwa huleta maana isiyo sahihi kimantiki, huwafanya wagonjwa wameze dozi nzima ya dawa kwa mgawanyiko wa saa 12 pekee yaani asubuhi, mchana na jioni pasipo kukumbuka kuwa siku nzima huhusisha mjumuiko wa saa 24.
Binafsi nimekuelewa vizuri hongera Kwa elimu uliyoitoa.
 
Emu fafanua ...mfano nameza Saa moja , ingine nimeze Saa nane na ingine nimeze Saa tatu hiyo Kwa Kwa kutwa mara tatu..na kama kutwa mara mbili nimeze Saa moja na ingine Saa nane si ndio maana yako au !?
 
mara tatu ndio.

nitameza asubuhi hapo ni kati ya saa 1 hadi saa mbili.

then nitameza tena mchana kati ya saa 7 hadi saa 8 (unaona hapo tayri ni karibu masaa yale yale 8.)
theni nitameza usiku saa 1 hadi saa 3 usiku. bado masaa yatacheza yale yale 8.
 
Emu fafanua ...mfano nameza Saa moja , ingine nimeze Saa nane na ingine nimeze Saa tatu hiyo Kwa Kwa kutwa mara tatu..na kama kutwa mara mbili nimeze Saa moja na ingine Saa nane si ndio maana yako au !?
Kutwa mara tatu maana yake dawa husika utaimeza kila baada ya masaa 8. Mfano saa 1, saa 9 na saa 5 usiku.

Kutwa mara mbili maana yake dawa utaimeza kila baada ya masaa 12 mfano saa moja asubuhi hadi saa 2 usiku.
 
mara tatu ndio.

nitameza asubuhi hapo ni kati ya saa 1 hadi saa mbili.

then nitameza tena mchana kati ya saa 7 hadi saa 8 (unaona hapo tayri ni karibu masaa yale yale 8.)
theni nitameza usiku saa 1 hadi saa 3 usiku. bado masaa yatacheza yale yale 8.

Boss asante kwa hoja yako, lakini hatupaswi kufanya hivi kwa kukadiria kama ambavyo hoja yako inaelezea. Ili ufanisi wa dawa uwe sahihi ni lazima kufuata muda katika kuzimeza.

Kutwa mara tatu maana yake dawa husika utaimeza kila baada ya masaa 8. Mfano saa 1, saa 9 na saa 5 usiku.

Kutwa mara mbili maana yake dawa utaimeza kila baada ya masaa 12 mfano saa moja asubuhi hadi saa 2 usiku.
 
Back
Top Bottom