Hivi karibuni nimepata mshangao wa mwaka mara baada ya kuona matukio mawili yanayokinzana TAnzania. La kwanza ni llile ambapo Sheikh Mkuu (nimewaambia awali kuwa huyu nu chaguo la CCM) alipowaasa waislamu wote Tanzania kutoshiriki maandamano ambayo kwa mujibu wake yenye vurugu ya CHADEMA. Lakini haukupita muda, kundi la watu wanaojiita waislamu waliingia mtaani na kuandamana wakipinga "mauaji" yanayofanywa na nchi za magharibi dhidi ya "nchi ya kiislamu", Libya. MAtukio haya mawili yamenishtua kusema kweli.
Nimeshtuka kwasababu wakati chaguo la CCM Mufti Simba anawashawishi watanzania wenye haki ya kudai maisha bora, hakusikika akipinga wananchi hao hao wakipigania maisha bora ya nchi ya Libya. Hivi kuna uzalendo kweli hapo? Lakini labda nieleze ni kwanini naona sasa watanzania tunaelekea kwenye ulofa sasa.
Awali ya yote yanayotokea Libya hayahusikani na dini maana wapinzani na walio upande wa Ghadafi wengi wao ni waislamu. Kinachotokea ni mapigano yanayotokana na ukabila baina ya watu wa mashariki walio na makao yao makuu Tripoli na wale wa magharibi walio na makao yao makuu Benghazi. KWa maana hiyo kuuleta udini katika hili ni kuwa na ufahamu haba wa matukio ya kimataifa.
La pili linalofanya mapigano haya yawepo na ndilo linaloniumiza zaidi kuhusu watanzania ni suala la kiuchumi. KWa wale wasiojua, sababu mojawapo iliyomfanya Ghadafi abaki madarakani kwa miaka 40 sasa ni uwezo wake wa kuwakumbuka wananchi wake japo kwa shingo upande. Kila mwezi, Ghadafi kwa kutumia pato la mafuta amekuwa akiwapa wananchi wake pato (social benefit) la dola za kimarekani 2,000 wawe wanafanya kazi au la. KWa level ya kitanzania iyo ni pesa kubwa mno. Ila kwa kifupi ni kwamba wananchi wameanza kufunguka na kutaka zaidi maana anachobaki nacho Ghadafi na familia yake achilia mbali kabila lake ni kubwa mno. Kinachoniuma hapa ni kwamba, wale wanaopewa dola 2,000 kwa mwezi hata wakiwa hawana kazi wanaandamana na kutafuta haki yao zaidi. Lakini waislamu wenzao ambao pamoja na kuwa nchi yao ina kila aina ya madini ikiwa na yale yasiyopatikana kokote kule duniani (Tanzanite), wanakatazwa kuandamana sio wakiomba pato zaidi bali wakitaka bei ya sukari ipunguzwe.
NAjiuliza hivi watanzania ni malofa kiasi gani? Dola 2,000 wanaopewa walibya walio jobless kwetu ni mshahara wa profesa mlimani. LAkini bado watu wakilalama wanakuwa wapinzani, waharibu amanai na kadhalika. Kuna akili ipi katika haya yote tukijua ya kuwa nchi yetu ina utajiri wa kupitiliza wa mali asili? Niliwahi kuwapa takwimu hapa kwamba japo ng'ombe wote waliopo Botswana ni wachache kuliko wale walioko katika mkoa wa Shinyanga peke yake, bado pato la beef Botswana ni kubwa kuliko mapato yetu ya madini yote ukijumlisha na pato linalopatikana katika utalii. Hivi tumelogwa?
Jk mwanzilishi wa siasa za udini Tanzania majuzi tu alimwambia Magufuli atumie "utu na ubinadamu" katika bomoa bomoa. Hivi ni utu gani alioutumia kuidhinisha mkataba wa Richmond ambao kila mtu anajua Lowasa alikuwa ni fall guy tu? Au ubinadamu gani aliutumia kupitisha mkataba wa DOWANS? Utu upi aliutumia kutaka kuharakisha malipo ya bilioni 94 ya dowans? Pengine upo utu pale ambapo katika karne ya 21 DAr es Salaam mji mkubwa kuliko yote kiuchumi TAnzania hauwezi kuwapa wakazi wake maji safi na umeme wa uhakika. Kama hayo yapo DAr, huko Nanjilinji kukoje?
BAdo ninawaasa waislamu ambao wengine ni marafiki zangu wakubwa tukiokuwa pamoja tangu utoto na wengine tukahudhuria pamoja madrasa tukijifunza KHalifu, Bete n.k. JK na kundi lake la maharamia kama Rostam, Makamba, UVCCM na wengineo kama Mufti Simba hawana wema na nyie hata kidogo. Wangekuwa nalo lolote la msingi leo hii Tanzania ingekuwa na mahakama ya KAdhi kama Kenya nchi yenye waislamu wachache kuliko sie lakini hilo lipo kwenye katiba yao. PIa TAnzania ingeshajiunga na OIC tena muda mrefu. Umewahi kufikiria ni kwanini pamoja na safari za kila leo nje ya nchi za JK hadi leo hajapata muda wa kuwa Alhaji (kwenda hijja Mecca)? Ni kwasababu usilamu kwake sio issue. Issue ni matumbo yao na familia zao na watafanya lolote ikiwa ni pamoja na kutugawakiudini kukamilisha agenda zao.
Waislamu wa Tunisia, Egypt, Libya, Yemen, Syria na Jordan wameshatufundisha kukataa ufisadi uliojificha kwenye udini. Tusipojifunza ushujaa wao si tu tunawaangusha watoto wetu na vizazi vijavyo bali tunageuka malofa. NAWAKILISHA!!!
Nimeshtuka kwasababu wakati chaguo la CCM Mufti Simba anawashawishi watanzania wenye haki ya kudai maisha bora, hakusikika akipinga wananchi hao hao wakipigania maisha bora ya nchi ya Libya. Hivi kuna uzalendo kweli hapo? Lakini labda nieleze ni kwanini naona sasa watanzania tunaelekea kwenye ulofa sasa.
Awali ya yote yanayotokea Libya hayahusikani na dini maana wapinzani na walio upande wa Ghadafi wengi wao ni waislamu. Kinachotokea ni mapigano yanayotokana na ukabila baina ya watu wa mashariki walio na makao yao makuu Tripoli na wale wa magharibi walio na makao yao makuu Benghazi. KWa maana hiyo kuuleta udini katika hili ni kuwa na ufahamu haba wa matukio ya kimataifa.
La pili linalofanya mapigano haya yawepo na ndilo linaloniumiza zaidi kuhusu watanzania ni suala la kiuchumi. KWa wale wasiojua, sababu mojawapo iliyomfanya Ghadafi abaki madarakani kwa miaka 40 sasa ni uwezo wake wa kuwakumbuka wananchi wake japo kwa shingo upande. Kila mwezi, Ghadafi kwa kutumia pato la mafuta amekuwa akiwapa wananchi wake pato (social benefit) la dola za kimarekani 2,000 wawe wanafanya kazi au la. KWa level ya kitanzania iyo ni pesa kubwa mno. Ila kwa kifupi ni kwamba wananchi wameanza kufunguka na kutaka zaidi maana anachobaki nacho Ghadafi na familia yake achilia mbali kabila lake ni kubwa mno. Kinachoniuma hapa ni kwamba, wale wanaopewa dola 2,000 kwa mwezi hata wakiwa hawana kazi wanaandamana na kutafuta haki yao zaidi. Lakini waislamu wenzao ambao pamoja na kuwa nchi yao ina kila aina ya madini ikiwa na yale yasiyopatikana kokote kule duniani (Tanzanite), wanakatazwa kuandamana sio wakiomba pato zaidi bali wakitaka bei ya sukari ipunguzwe.
NAjiuliza hivi watanzania ni malofa kiasi gani? Dola 2,000 wanaopewa walibya walio jobless kwetu ni mshahara wa profesa mlimani. LAkini bado watu wakilalama wanakuwa wapinzani, waharibu amanai na kadhalika. Kuna akili ipi katika haya yote tukijua ya kuwa nchi yetu ina utajiri wa kupitiliza wa mali asili? Niliwahi kuwapa takwimu hapa kwamba japo ng'ombe wote waliopo Botswana ni wachache kuliko wale walioko katika mkoa wa Shinyanga peke yake, bado pato la beef Botswana ni kubwa kuliko mapato yetu ya madini yote ukijumlisha na pato linalopatikana katika utalii. Hivi tumelogwa?
Jk mwanzilishi wa siasa za udini Tanzania majuzi tu alimwambia Magufuli atumie "utu na ubinadamu" katika bomoa bomoa. Hivi ni utu gani alioutumia kuidhinisha mkataba wa Richmond ambao kila mtu anajua Lowasa alikuwa ni fall guy tu? Au ubinadamu gani aliutumia kupitisha mkataba wa DOWANS? Utu upi aliutumia kutaka kuharakisha malipo ya bilioni 94 ya dowans? Pengine upo utu pale ambapo katika karne ya 21 DAr es Salaam mji mkubwa kuliko yote kiuchumi TAnzania hauwezi kuwapa wakazi wake maji safi na umeme wa uhakika. Kama hayo yapo DAr, huko Nanjilinji kukoje?
BAdo ninawaasa waislamu ambao wengine ni marafiki zangu wakubwa tukiokuwa pamoja tangu utoto na wengine tukahudhuria pamoja madrasa tukijifunza KHalifu, Bete n.k. JK na kundi lake la maharamia kama Rostam, Makamba, UVCCM na wengineo kama Mufti Simba hawana wema na nyie hata kidogo. Wangekuwa nalo lolote la msingi leo hii Tanzania ingekuwa na mahakama ya KAdhi kama Kenya nchi yenye waislamu wachache kuliko sie lakini hilo lipo kwenye katiba yao. PIa TAnzania ingeshajiunga na OIC tena muda mrefu. Umewahi kufikiria ni kwanini pamoja na safari za kila leo nje ya nchi za JK hadi leo hajapata muda wa kuwa Alhaji (kwenda hijja Mecca)? Ni kwasababu usilamu kwake sio issue. Issue ni matumbo yao na familia zao na watafanya lolote ikiwa ni pamoja na kutugawakiudini kukamilisha agenda zao.
Waislamu wa Tunisia, Egypt, Libya, Yemen, Syria na Jordan wameshatufundisha kukataa ufisadi uliojificha kwenye udini. Tusipojifunza ushujaa wao si tu tunawaangusha watoto wetu na vizazi vijavyo bali tunageuka malofa. NAWAKILISHA!!!