Matokeo ya Kura za Maoni CCM yanaonyesha kuwa Viongozi wa Chini wanapingana kimtazamo na Mwenyekiti wao Taifa

Benson Mramba

JF-Expert Member
Oct 29, 2013
644
1,482
Binafsi nimeshtushwa sana na matokeo ya kura za maoni za CCM kuanzia Udiwani wa Kata hadi Ubunge. Kwa ujumla ni kuwa kila ambalo Mwenyekiti (Rais) aliloonyesha kulitaka au kulitamani Wajumbe wamelipinga kwa nguvu.

1. Wanachama wote wa vyama vya upinzani ambao hawana asili na CCM wameshindwa kura za maoni.

2. WanaCCM wengi ambao Rais amekuwa akionyesha kuwaunga mkono wameshindwa vibaya Mfano Makonda na Mwakyembe

3. WanaCCM ambao Rais ameonyesha kuwakosoa na kuwaponda hadharani wameshinda kwa kishindo mfano Mrisho Gambo na Ndugulile.

Hizi ni salamu nzito kwamba Mwenyekiti anafikiria tofauti na viongozi wa Chini na Wanachama! Angalia Kinana alivyoshangiliwa Dodoma kwenye mkutano Mkuu!

Kinana anasema hakuna Uchaguzi rahisi kwasababu kura ziko kwenye mioyo ya watu! Sasa Rais awe makini na jinsi atavyowahandle wapinzani wake kwenye uchaguzi Mkuu maana wananchi wanahasira ya kukosa Bunge Live na kuzuiliwa kwa shughuli za kisiasa.

Kesho Lissu anarudi kama ni kweli! Busara aliyoitumia Kikwete kwa Lowassa kumpa nafasi bila kutumia polisi ndio kwa mtazamo wangu inapaswa kutumika kesho.

Lissu alindwe aachwe aropoke atakavyo asaidiwe afanye kampeni zake ajibiwe kwa hoja! Nguvu yoyote inaweza kuleta matokeo mabaya sana kwa Rais. Watanzania hawapendi watu wababe kwa washindani wao!
 
Benson Mramba, naona umejionea mwenyewe Ccm inawenyewe.
Mwisho hivi vyama vinaendeshwa na Binadamu wenye mapungufu kwahiyo tuvumiliane Kiongozi.

Nazani umeona makamanda waliounga juhudi walivyofanywa na kupotezwa kwenye Ramani ya siasa.
Rudi nyumbani. Upinzani ndiyo sehemu ya Vijana kutoka kirahisi kwenye siasa.
Mbowe anamapungufu kama ilivyo kwa Magufuli na ndiyo Ubinadamu wenyewe.
 
Benson Mramba, naona umejionea mwenyewe Ccm inawenyewe.
Mwisho hivi vyama vinaendeshwa na Binadamu wenye mapungufu kwahiyo tuvumiliane Kiongozi.

Nazani umeona makamanda waliounga juhudi walivyofanywa na kupotezwa kwenye Ramani ya siasa.
Rudi nyumbani. Upinzani ndiyo sehemu ya Vijana kutoka kirahisi kwenye siasa.
Mbowe anamapungufu kama ilivyo kwa Magufuli na ndiyo Ubinadamu wenyewe.
Inabidi ianzishwe kampeni ya back to the root
 
Wengine tunaweka akiba maoni yetu kwanza. Kuna mengi sana hatuoni na yanatoa taswira ya tulipotoka na tunapoenda.

Kama unaipenda hii nchi iweke kwenye maombi, achana na ushabiki wa vyama. Tuwe tayari kuilinda nchi yetu bila unafiki na kwa uzalendo mkuu.
 
Hizo hoja za kumjibu Lissu ndio Hana kabsa, ivi akiulizwa kwanini hajaongeza mishahara Kwa hii miaka mitano jibu atakuwa nalo??? Au ataanza kutusimulia bombadia?

Hata statutory annual increment hamna 5years?

Kwa ufupi meko hatoboi labda wamuuee lissu!
 
Nikiwahi kusema ccm mashinani imemeguka, imekata center bolt, kuanzia ngazi ya mkoa watu wako peponi wanakula mema, ngazi ya wilaya wako taabani ajira zao Ni kinda Kura kubeba spika na kujaza mikutano, mbaya zaidi majitu waliyopambana nayo ndio yanapewa mvinyo mpya yanakaa meza kuu, waliomzunguka mwenyekiti hawajawahi shinda nafasi yeyote yakisiasa akina bashiru polepole mangula hata ukiwaambia wagombee umwenyekiti wa mtaa hawashindi
 
Siasa ni kuangalia fursa. Wailoondoka kwa nyodo CHADEMA wanaumia. Kafulila,lijualikali, mambo moto
 
Miaka mitano hamna kilichokamilika, ndio kwanza ajira zimedorora, watu wote tumeegemea ruler tumenyooka, unaenda kufungua nssf ya mtu akulipe faini? Halafu wenye shida na pesa zao unawambia wafikishe miaka 60 kweli?
 
Baada ya kuona huna nafasi ccm hii awamu hata nafasi ya uteuzi umeona afadhali ujipendekeze tena upinzani
 
Hii imempa picha kwamba wazo la kuongeza mda alifute.Kama ccm itashinda October, kuanzia mwakani utii kwa mwenyekiti utapungua au kutoweka kabisa wakimaanisha ni kipindi chake cha mda wa kuondoka ndipo Makundi yatakapojitokeza,2025 mwenyekiti atakanwa na kukosolewa live na Wana chama.
 
Hilo la kuto kubalika ndani na nje ya CCM linajulikana vzr, ndiyo sababu hata fomu ya urais ilikuwa moja tuu
 
Wahamiaji kina katambi, lijuakali, Nassari waanze kumtembeza bahasha kutafuta kazi,wazo la kufikiria kuna teuzi wasahau wavute kabisa ccm ijayo mwenyekiti Hana nguvu nayo tena.
Pia mbinu ya manunuzi ili kuuwa upinzani imebuma balaa imewapa hasara awatoitumia tena.So suala la teuzi za cv ya kuabudu limekufa natural death.
 
We we ndiyo unaropoka subirini huruma sasa na ukuu wa wilaya. Hakuna mtu atawaamini wakatwa mikia
 
Wajumbe wamefyeka tumaini la kuongezewa mda.Membe kafanya mistake Sana kuhama angetulia tu Kama wenzake milango ipo wazi mbeleni
 
Back
Top Bottom