Makanyaga
JF-Expert Member
- Sep 28, 2007
- 11,544
- 7,484
Matiko akiri kumiliki silaha
Najiuliza swali fikirishi kwamba ni nini cha ajabu huyu mtu kumiliki silaha, kwa hadhi yake kama mbunge?
=====
Matiko akiri kumiliki silaha
Alidai mahakamani wakati akitoa ushahidi wake mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, baada ya kuhojiwa na Jamhuri dhidi ya utetezi wake.
Shahidi huyo aliongozwa na Wakili wa utetezi, Peter Kibatala.
Akihojiwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon, mshtakiwa huyo alidai kuwa ingawa anamiliki silaha hiyo hajawahi kuitumia wala hakumbuki kama iliwahi hata kufyatuka mahali popote.
Alidai wakati akiongozwa na Wakili wa utetezi, Kibatala kuwa katika kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Kinondoni, alipewa jukumu la kufuatilia nakala za viapo na barua za utambulisho wa mawakala.
Alidai kuwa yeye ni mkazi wa Tarime Mjini, Februari 15, 2018 alipofika Dar es Salaam, aliwasiliana na mmoja wa viongozi wa kamati ndogo ya uchaguzi, Benson Kigaila kwa simu kumfahamisha kuwa amefika.
"Aliniteua mimi na Mbunge wa Viti Maalum, Susan Lyimo, kufuatilia barua za utambulisho pamoja na hati za viapo vya mawakala," alidai Matiko.
Akifafanua zaidi alidai kuwa walianza kufuatilia barua hizo Februari 16, 2018, saa nne asubuhi walikwenda kumuona Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni ambaye ndiye alikuwa msimamizi wa uchaguzi huo ili awasaidie kupata barua hizo.
Alidai kuwa walifika ofisini kwa Mkurugenzi na kuambiwa wasubiri mpaka walipoonana naye saa saba mchana, lakini aliwaambia anashughulikia jambo hilo hivyo wasubiri mpaka saa 12 jioni.
"Tulisubiri mpaka saa 12, lakini hatukufanikiwa kupata barua hizo na mkurugenzi aliwahakikishia watapata mpaka kufikia saa moja usiku wa siku hiyo," alidai na kuongeza:
"Tulipewa namba za simu za msimamizi wa uchaguzi na msaidizi wake na kuendelea kuwasiliana na msimamizi msaidizi wa uchaguzi aliyemtaja kwa jina la Victoria Charles, mpaka saa tano usiku na kwamba alionekana kutingwa na kazi ya kusambaza vifaa vya uchaguzi hivyo akashindwa kumpatia barua hizo na kumwahidi kuwa atawasiliana naye saa 11 alfajiri ya Februari 17, 2018 ambayo ndiyo ilikua siku ya uchaguzi," alidai Matiko.
Alidai kuwa mpaka kufikia saa 11 alfajiri barua na nakala za viapo hivyo zilikuwa hazijapatikana, alitoa taarifa kwa msimamizi wa uchaguzi na baadaye kwa viongozi wa kamati ndogo ya uchaguzi na jukumu lake likaishia hapo.
Mbali na Matiko, washtakiwa wengine ni Mwanyekiti wa Chadema Freeman Mbowe, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu, Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, Mbunge wa Kibamba John Mnyika na Mbunge wa Bunda, Esther Bulaya.
Pia wamo Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Vincent Mashinji.
Chanzo: Nipashe
Najiuliza swali fikirishi kwamba ni nini cha ajabu huyu mtu kumiliki silaha, kwa hadhi yake kama mbunge?
=====
Matiko akiri kumiliki silaha
Alidai mahakamani wakati akitoa ushahidi wake mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, baada ya kuhojiwa na Jamhuri dhidi ya utetezi wake.
Shahidi huyo aliongozwa na Wakili wa utetezi, Peter Kibatala.
Akihojiwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon, mshtakiwa huyo alidai kuwa ingawa anamiliki silaha hiyo hajawahi kuitumia wala hakumbuki kama iliwahi hata kufyatuka mahali popote.
Alidai wakati akiongozwa na Wakili wa utetezi, Kibatala kuwa katika kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Kinondoni, alipewa jukumu la kufuatilia nakala za viapo na barua za utambulisho wa mawakala.
Alidai kuwa yeye ni mkazi wa Tarime Mjini, Februari 15, 2018 alipofika Dar es Salaam, aliwasiliana na mmoja wa viongozi wa kamati ndogo ya uchaguzi, Benson Kigaila kwa simu kumfahamisha kuwa amefika.
"Aliniteua mimi na Mbunge wa Viti Maalum, Susan Lyimo, kufuatilia barua za utambulisho pamoja na hati za viapo vya mawakala," alidai Matiko.
Akifafanua zaidi alidai kuwa walianza kufuatilia barua hizo Februari 16, 2018, saa nne asubuhi walikwenda kumuona Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni ambaye ndiye alikuwa msimamizi wa uchaguzi huo ili awasaidie kupata barua hizo.
Alidai kuwa walifika ofisini kwa Mkurugenzi na kuambiwa wasubiri mpaka walipoonana naye saa saba mchana, lakini aliwaambia anashughulikia jambo hilo hivyo wasubiri mpaka saa 12 jioni.
"Tulisubiri mpaka saa 12, lakini hatukufanikiwa kupata barua hizo na mkurugenzi aliwahakikishia watapata mpaka kufikia saa moja usiku wa siku hiyo," alidai na kuongeza:
"Tulipewa namba za simu za msimamizi wa uchaguzi na msaidizi wake na kuendelea kuwasiliana na msimamizi msaidizi wa uchaguzi aliyemtaja kwa jina la Victoria Charles, mpaka saa tano usiku na kwamba alionekana kutingwa na kazi ya kusambaza vifaa vya uchaguzi hivyo akashindwa kumpatia barua hizo na kumwahidi kuwa atawasiliana naye saa 11 alfajiri ya Februari 17, 2018 ambayo ndiyo ilikua siku ya uchaguzi," alidai Matiko.
Alidai kuwa mpaka kufikia saa 11 alfajiri barua na nakala za viapo hivyo zilikuwa hazijapatikana, alitoa taarifa kwa msimamizi wa uchaguzi na baadaye kwa viongozi wa kamati ndogo ya uchaguzi na jukumu lake likaishia hapo.
Mbali na Matiko, washtakiwa wengine ni Mwanyekiti wa Chadema Freeman Mbowe, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu, Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, Mbunge wa Kibamba John Mnyika na Mbunge wa Bunda, Esther Bulaya.
Pia wamo Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Vincent Mashinji.
Chanzo: Nipashe