KERO Matatizo ya Kimara yamehamia Bunju

KERO Matatizo ya Kimara yamehamia Bunju

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

MTAZAMO

Platinum Member
Joined
Feb 8, 2011
Posts
20,088
Reaction score
35,281
Kwa ufupi,

Sijui mipango ya hii miji inapangwa vipi. Kipindi serikali inafanya juhudi kutanua Morogoro road moja ya sababu kuu ilikuwa ni kuzidiwa kwa wingi wa magari.

Hivi nani aliamua mabasi sasa yaanze kupita Bagamoyo road na huku Morogoro imetanuliwa na bila upanuzi wa Bagamoyo road? Hivi mnaona yanayoendelea kwenye hiyo barabara? Hayo maeneo ndio premium kwa nchi kwasasa na magari ni mengi ila barabara finyu.

Mabasi ya mikoani kwenye barabara ile kweli njia mbili? Mnasubiri janga lipi mtambue zile hatari za Kimara zinahamia Bunju?

Anyway, hizi barabara tunatumia wote! Ila hatari haichagui. Mnawapa mizigo trafiki isiyo na ulazima.

Juzi mmeona yaliyotokea! Wote tunaona yanakuja mengi zaidi. Chukueni hatua!
 
Kwa ufupi,

Sijui mipango ya hii miji inapangwa vipi. Kipindi serikali inafanya juhudi kutanua Morogoro road moja ya sababu kuu ilikuwa ni kuzidiwa kwa wingi wa magari.

Hivi nani aliamua mabasi sasa yaanze kupita Bagamoyo road na huku Morogoro imetanuliwa na bila upanuzi wa Bagamoyo road? Hivi mnaona yanayoendelea kwenye hiyo barabara? Hayo maeneo ndio premium kwa nchi kwasasa na magari ni mengi ila barabara finyu.

Mabasi ya mikoani kwenye barabara ile kweli njia mbili? Mnasubiri janga lipi mtambue zile hatari za Kimara zinahamia Bunju?

Anyway, hizi barabara tunatumia wote! Ila hatari haichagui. Mnawapa mizigo trafiki isiyo na ulazima.

Juzi mmeona yaliyotokea! Wote tunaona yanakuja mengi zaidi. Chukueni hatua!
Mabasi ya mikoani kwenye barabara ile kweli njia mbili? Mnasubiri janga lipi mtambue zile hatari za Kimara zinahamia Bunju?
 
Sasa hivi hiyo barabara ajali kila kukicha! Imagine mashule yaliyojaa huko na school buses achilia mbali watumia njia wengine. Mabasi yanatanua kwa kasi bila kujali kabisa.
Kwahiyo tatizo ni uendeshaji mbaya wa madereva wa mabasi sio?
 
Kwahiyo tatizo ni uendeshaji mbaya wa madereva wa mabasi sio?
Barabara nyembamba sana unategemea nini kwa mabasi ya mikoani na malori? Ni hatari sana
 
Mwezi wa 4 hiyo barabara kulitokea ajali 3 mfululizo😢. 1. Lori kutoka wazo liligonga bajaji 2. Mwana dada akiwa pembeni mwa barabara akapitiwa na gari 3. Bodaboda na abiria wake waligongwa na bus.
 
Ok umelaumu, basi toa solution wafanyaje, tatizo lililopo kwa wabongo wengi sana uwa ni kulaumu tu bila kusema nini kifanyike kutatua hilo tatizo. Tupo nyuma sana sijui elimu au akili zetu ni ndogo.
 
Barabara nyembamba sana unategemea nini kwa mabasi ya mikoani na malori? Ni hatari sana
Nimetumia sana njia hio nuda wa jioni madereva wa huko ukiachilia mbali wa mabasi wanaendesha hovyo sana. Hio hio njia nyembamba maderva wanalazimisha njia tatu hadi nne unategemea nini?
 
Back
Top Bottom