Matapeli hawa ulikutana nao wapi?chukua tahadhari

Matapeli hawa ulikutana nao wapi?chukua tahadhari

Hao sijakutana nao ila kuna wale wanalinipigia simu nakumbuka nilikua chuo mwanza eti wapo na wazungu kuna dawa wanazitaka so nikanunue mahali halafu wakifika na hao wazungu watainunua kwa bei ya mara tatu niliyonunulia mimi halafu ile faida nagawana nao nilisumbuana nao sana siku hiyo sintasahau

Ha Ha Ha Brt Walifanikiwa Kumtapeli Kwa Njia Kama Ya Kwako, Ila Ilikuwa Ni 5000 Ya Vocha Maana Walimwomba Kwanza Vocha.
 
Songea 2005, niliongozana nao nikawape fungu lao huku naelekea kituo cha polisi. Nilipokaribia na eneo la shinyanga guest house huku wanakiona kituo cha polisi walipiga u turn na kwenda zao.
 
Hao sijakutana nao ila kuna wale wanalinipigia simu nakumbuka nilikua chuo mwanza eti wapo na wazungu kuna dawa wanazitaka so nikanunue mahali halafu wakifika na hao wazungu watainunua kwa bei ya mara tatu niliyonunulia mimi halafu ile faida nagawana nao nilisumbuana nao sana siku hiyo sintasahau

Nilishakutana nao hao....
 
Nilishawai kukutana nao lumumba St, nje ya benki crdb vijana 2001. Kumbe born town kitambo
 
Nimekutana nao kitambo sana hao. Kijitonyama walinionesha 'almasi' kinondoni walikuwa wanatafuta ofisi za madini, shaurimoyo walikuwa wanatafuta hosp ya mnazimmoja wakiwa kuna mwenzao kapata ajali, kariakoo msimbazi mmoja alidondosha bahasha mwingine akaokota akaniomba tukagawane aliyedondosha akawa analia akisema amedondosha bahasha yenye hela nyingi. Hawajanipata hata tukio moja
 
Dah usinikumbushe Mimi na ushamba wangu nilitokea kijijini kwenda mbeya. nilikutana nao stend u nayoeleza hivyohivyo ndo walivyoniingiza mjini Mimi, nikaona nauaga umaskini kilaini niliwasindikiza hadi waliposema wanaenda kuuza hayo madini nipate mgao. wakaanza kubishana Yule mwenye mzigo akasema ananiamini Mimi tu hivyo niubebe hadi mwanjelwa wao watakuja nyuma ila niache Simu na tupesa nilitonato nikaona haina shida wanipe na Mie niingie nao mtini. nilipewa nauli ya kwenda tu ya daladala sikujali nilifurahi sana aisee, nikashuka maeneo anayoishi kaka yangu lengo kumpa akauze tukajenge Ghorofa kijijini, Ile kufungua mzigo nikakuta betri ndogo 2 zimechakaa. basi ikala kwangu
 
Mimi nilikutana na matapeli kama hao mwaka 2002 maeneo ya Ubungo Bus Terminal wakiulizia ilipo hospitali ya Mikocheni. Nilichowajibu huku nimekunja uso ni kwamba "bado mnahangaika na utapeli wa siku nyingi hivyo? Mimi ndiyo kazi yangu na hiyo mbinu nilisha achana nayo miaka mingi" Ikabidi waondoke huku wakisema "Samahani mzee hatukujua kama na wewe ni mwenzetu". Naona waliamini nilichowaambia japo maishani mwangu sijawahi kufanya utapili kwa mtu. Ila ilisaidia kuwaondoa haraka kwangu.

Hahahaha uliwakomesha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom