Matapeli hawa ulikutana nao wapi?chukua tahadhari

Matapeli hawa ulikutana nao wapi?chukua tahadhari

AG.6851

Member
Joined
Jul 31, 2013
Posts
97
Reaction score
87
Habaar wana JF

Kwa muda wa iaka mitatu Tofauti Na Katika Maeneo Tofauti, Tanga Na Mbeya, Kuna Watu Nimekutana Nao Wakiwa Na Style Na Mazungumzo Yanayofanana.Jana ndiyo nimetambua kumbe ni wezi/matapeli.

Story Yenyewe Ni Kama Hii

Siku moja katika pitapita zangu maeneo ya Tanga na Mbeya kuna watu walijitokeza mbele yangu na kuonyesha sura ya huzuni na kuchoka na kuniuliza "unaifahamu Hospitali ya Mission ilipo, kwani kuna ajali imetokea ikihusisha Wazungu na sisi tulifanikiwa kuokota kitu flani kwenye eneo la tukio (Akaonesha bahasha ndogo yenye kitu ndani yake)"

Nilimuuliza jina la Hospitali akadai yeye anaijua kwa jina hilo la Hospitali ya Mission, nikamhoji nini lengo lako kama utaipata hiyo Hospital?akajibu "Nimeambiwa nipeleke kitu hiki halafu nitapewa Tsh. milioni moja (1000,000,000/=).

Baada ya kujibu siijui, anatokea jamaa mwingine kama mpita njia alivyotupita huyo jamaa akasema " labda tumuulize huyu anayepita huenda anajua."akamwita na kumuuliza na akauliza "hicho kitu kiko wapi?" akasema "hiki hapa lakini naomba msije kuninyang'anya" alipofungua bahasha ilikuwa na maandishi "Dhahabu hii ni mali ya kaampuni ....... na thamani yake ni Tsh. 100,000,000,000/="

Huyo mpita njia akashangaa kwa mstuko na kuniambia chinichini "Tumnyang'anye unaona dili hili" binafsi sikujua kinachoendelea na nilizidi kumhoji maswali huyo mwenye bahasha alipoona maswali yamezidi na Mungu ameniongoza bila kujua ni wezi walichukuana wawili na kudai wanaenda kuuza.

Kwa style hiyohiyo jana kuna jamaa kalizwa simu sababu eti walibadilishana kwa kuambiwa lata simu yako ma wewe ushike madini haya halafu tunakuja, wakatikomea bila kurudi.

Swali: Wewe walikukuta wapi na kwa style ipi?hata kama walikuliza funguka tu ili iwe funzo kwa wengine.
 
Me nimekutana nao wengi sana ngoja nikupe chanzo chao cha hayo ambapo ni Mfumo wa kupata kwa haki ushauzwa kwa wachache wengi wanahangaika kama ulokutana nao, ka mfumo ungekua mzuri wala usingeleta mada ka iyo.
 
Hao sijakutana nao ila kuna wale wanalinipigia simu nakumbuka nilikua chuo mwanza eti wapo na wazungu kuna dawa wanazitaka so nikanunue mahali halafu wakifika na hao wazungu watainunua kwa bei ya mara tatu niliyonunulia mimi halafu ile faida nagawana nao nilisumbuana nao sana siku hiyo sintasahau
 
Mimi nilikutana nao maeneo ya magomeni hospital kitambo kidogo ilikuwa mwaka 2002.
 
Habaar wana JF

Kwa muda wa iaka mitatu Tofauti Na Katika Maeneo Tofauti, Tanga Na Mbeya, Kuna Watu Nimekutana Nao Wakiwa Na Style Na Mazungumzo Yanayofanana.Jana ndiyo nimetambua kumbe ni wezi/matapeli.

Story Yenyewe Ni Kama Hii

Siku moja katika pitapita zangu maeneo ya Tanga na Mbeya kuna watu walijitokeza mbele yangu na kuonyesha sura ya huzuni na kuchoka na kuniuliza "unaifahamu Hospitali ya Mission ilipo, kwani kuna ajali imetokea ikihusisha Wazungu na sisi tulifanikiwa kuokota kitu flani kwenye eneo la tukio (Akaonesha bahasha ndogo yenye kitu ndani yake)"

Nilimuuliza jina la Hospitali akadai yeye anaijua kwa jina hilo la Hospitali ya Mission, nikamhoji nini lengo lako kama utaipata hiyo Hospital?akajibu "Nimeambiwa nipeleke kitu hiki halafu nitapewa Tsh. milioni moja (1000,000,000/=).

Baada ya kujibu siijui, anatokea jamaa mwingine kama mpita njia alivyotupita huyo jamaa akasema " labda tumuulize huyu anayepita huenda anajua."akamwita na kumuuliza na akauliza "hicho kitu kiko wapi?" akasema "hiki hapa lakini naomba msije kuninyang'anya" alipofungua bahasha ilikuwa na maandishi "Dhahabu hii ni mali ya kaampuni ....... na thamani yake ni Tsh. 100,000,000,000/="

Huyo mpita njia akashangaa kwa mstuko na kuniambia chinichini "Tumnyang'anye unaona dili hili" binafsi sikujua kinachoendelea na nilizidi kumhoji maswali huyo mwenye bahasha alipoona maswali yamezidi na Mungu ameniongoza bila kujua ni wezi walichukuana wawili na kudai wanaenda kuuza.

Kwa style hiyohiyo jana kuna jamaa kalizwa simu sababu eti walibadilishana kwa kuambiwa lata simu yako ma wewe ushike madini haya halafu tunakuja, wakatikomea bila kurudi.

Swali: Wewe walikukuta wapi na kwa style ipi?hata kama walikuliza funguka tu ili iwe funzo kwa wengine.

Huo utapeli ni wa siku nyingi sana sema wamerudia tena baada ya kudhani watu wamesahau.
 
Hawa nilishawahi kukutana nao DSM mara tatu barabarani. Mara ya kwanza ilikuwa barabara ya United Nations, mara ya pili Samora na ya tatu Azikiwe. Mara zote wanadai kupotea njia na kutafuta ofisi ya madini. Kwa kuwa mara ya kwanza waliniliza siku hizi hawanipati tena. Normally wanakuwa 2 au 3. Kama siyo ofisi za madini wanajifanya kupotea mahali wanapokwenda.
 
Hii ndio wazungu wanasema "there is a sucker born every minute". Hii kitu toka niko shule ya msingi mpaka leo wanapigwa?
 
Hawa jamaa mbeya hapa kabla ya bank nmb loleza . Wanawaibia watu sana hadi huku jacaranda wanafika wanawatapeli hata dada wa nyumbani.
 
Hii ndio wazungu wanasema "there is a sucker born every minute". Hii kitu toka niko shule ya msingi mpaka leo wanapigwa?

Walisema pia mjini wajinga wengi zaidi. Na ndio maana karata tatu , sijui shinda gari , tv na music kila siku watu wanawaona hao matapeli wamevipanga pale lakini siku moja na wao hujaribu na kuonja joto yake
 
Hiyo nshu du! Mwaka 2005 Kigoma kwa bela wenyewe huulizia baptist hahaha
 
Habaar wana JF

Kwa muda wa iaka mitatu Tofauti Na Katika Maeneo Tofauti, Tanga Na Mbeya, Kuna Watu Nimekutana Nao Wakiwa Na Style Na Mazungumzo Yanayofanana.Jana ndiyo nimetambua kumbe ni wezi/matapeli.

Story Yenyewe Ni Kama Hii

Siku moja katika pitapita zangu maeneo ya Tanga na Mbeya kuna watu walijitokeza mbele yangu na kuonyesha sura ya huzuni na kuchoka na kuniuliza "unaifahamu Hospitali ya Mission ilipo, kwani kuna ajali imetokea ikihusisha Wazungu na sisi tulifanikiwa kuokota kitu flani kwenye eneo la tukio (Akaonesha bahasha ndogo yenye kitu ndani yake)"

Nilimuuliza jina la Hospitali akadai yeye anaijua kwa jina hilo la Hospitali ya Mission, nikamhoji nini lengo lako kama utaipata hiyo Hospital?akajibu "Nimeambiwa nipeleke kitu hiki halafu nitapewa Tsh. milioni moja (1000,000,000/=).

Baada ya kujibu siijui, anatokea jamaa mwingine kama mpita njia alivyotupita huyo jamaa akasema " labda tumuulize huyu anayepita huenda anajua."akamwita na kumuuliza na akauliza "hicho kitu kiko wapi?" akasema "hiki hapa lakini naomba msije kuninyang'anya" alipofungua bahasha ilikuwa na maandishi "Dhahabu hii ni mali ya kaampuni ....... na thamani yake ni Tsh. 100,000,000,000/="

Huyo mpita njia akashangaa kwa mstuko na kuniambia chinichini "Tumnyang'anye unaona dili hili" binafsi sikujua kinachoendelea na nilizidi kumhoji maswali huyo mwenye bahasha alipoona maswali yamezidi na Mungu ameniongoza bila kujua ni wezi walichukuana wawili na kudai wanaenda kuuza.

Kwa style hiyohiyo jana kuna jamaa kalizwa simu sababu eti walibadilishana kwa kuambiwa lata simu yako ma wewe ushike madini haya halafu tunakuja, wakatikomea bila kurudi.

Swali: Wewe walikukuta wapi na kwa style ipi?hata kama walikuliza funguka tu ili iwe funzo kwa wengine.

Me nilikutana nao Dodoma wakifanya utafiti na twaweza.........
 
Mimi nilikutana na matapeli kama hao mwaka 2002 maeneo ya Ubungo Bus Terminal wakiulizia ilipo hospitali ya Mikocheni. Nilichowajibu huku nimekunja uso ni kwamba "bado mnahangaika na utapeli wa siku nyingi hivyo? Mimi ndiyo kazi yangu na hiyo mbinu nilisha achana nayo miaka mingi" Ikabidi waondoke huku wakisema "Samahani mzee hatukujua kama na wewe ni mwenzetu". Naona waliamini nilichowaambia japo maishani mwangu sijawahi kufanya utapili kwa mtu. Ila ilisaidia kuwaondoa haraka kwangu.
 
Hao sijakutana nao ila kuna wale wanalinipigia simu nakumbuka nilikua chuo mwanza eti wapo na wazungu kuna dawa wanazitaka so nikanunue mahali halafu wakifika na hao wazungu watainunua kwa bei ya mara tatu niliyonunulia mimi halafu ile faida nagawana nao nilisumbuana nao sana siku hiyo sintasahau

Juzi wamenikosa baada ya kuwaambia siwezi kufanya hivyo bila kumshirikisha Mr
 
wwalinikuta ubungo siku moja eti wananiuliza ofisi za stamico.
 
Ubungo terminal na darajani pale jirani na river side, al manusra nipige mtu ngumi manake nilikuwa na uchovu wa safari afu natafuta usafiri wa kunifikisha ghetto wakahisi huyu wa kuja nikawatoa nishai.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom