mollel arusha
Member
- Apr 26, 2013
- 19
- 8
Matangazo ya pombe yanayotangazwa kila mahali kupitia runinga, internet, magazeti, face book, jamii forum, radio, n.k yamekuwa kero kwangu. hii inaonyesha wazi jinsi gani taifa linahamasishwa kuwa walevi. ni ukweli kwamba ulevi unaenda sambamba na vitendo viovu kama vile: uasherati, uzinzi, wizi n.k kiasi kwamba ndiyo chanzo cha magonjwa ya zinaa. serikali inatumia a lot of money kuwatibu, na wakati mwingine kutumia gharama kubwa sana kuweka matangazo ya kujikinga. kwangu mimi naona serikali inajimaliza yenyewe kwa kuruhusu matangazo ya aina hiyo kila mahali na hapo hapo inatuumia pesa za watanzania kwa matumizi yasiyo ya lazima. pombe ina madhara makubwa sana kama vile ajali tunazoona za barabarani nyingi zinatokana na pombe. waendesha bodaboda wengi ni wanywaji wa pombe na ndiyo wanao maliza watu kwa sababu ya ulevi wa pombe. hivyo ninacho washauri watanzania tumieni hizo fursa kwa matangazo ya maendeleo na kuhamasisha maendeleo na zaidi sana watu wamrudie Mungu na kumpokea Bwana Yesu awe Bwana na mwokozi wa maisha yao. Mungu awabariki sana.