Jamani kwa heshima na taadhima, naomba kuwasihi viongozi wa kanisa Katoliki Parokia ya Sinza, wapunguze matangazo. Matangazo mara baada ya ibada hasa za jumapili ni marefu mnoooo, Wazungumzaji kibao na matangazo ni yale yale, kila mzungumzaji anayatoa kwa ufundi wake.
Kila kitu kifanyike kwa kiasi. Ubao wa matangazo utumike, watangazaji wajipange, mtu mmoja abebe hoja zote muhimu badala ya kila kiongozi kwenda mbele kusema lake.
Matangazo ya miezi mingi ijayo yasubiri muda wake au yaanzie ngazi ya jumuia badala ya ibada kuwa kama mkutano.
Kila kitu kifanyike kwa kiasi. Ubao wa matangazo utumike, watangazaji wajipange, mtu mmoja abebe hoja zote muhimu badala ya kila kiongozi kwenda mbele kusema lake.
Matangazo ya miezi mingi ijayo yasubiri muda wake au yaanzie ngazi ya jumuia badala ya ibada kuwa kama mkutano.