Maswali ya msingi kwa tume ya warioba

Maswali ya msingi kwa tume ya warioba

Kunamambo mawili moja wakati unaandika ulikuwa unakunywa viloba au ulikuwa umelewa hata hujuwi nikitugani unataka kuuliza.
1. Ilipelekwa bungeni kwa mujibu washeria
2. Mahakama ya kadhi sijambo la kikatiba maana katiba haizungumzii kundi moja katika jamii
3. Kudumisha muungano nilazima nchi washiriki tufanye mambo yanayofanana kuiruhusu Zanzibar kuwa na serikali kamili tayari muungano unanyufa kuziba nyufa nikuweka serikali 3 haiepukiki
4. Hitimisho lako halina maana. Kisheria bunge lililopo kwa ujumla wake halikuwa na maana kwakuwa waliopo walichaguliwa kutetea na kulinda katiba iliyopo ( hicho nikiapo chao)
 
1. Ikiwa Rasimu ya pili iliyoandikwa na TUME
YA WARIOBA ndio maoni ya wananchi na
iliandikwa kwa ustadi mkubwa na wataalamu
wa masuala ya uandishi wa katiba na wenye
uzoefu ilipelekwa bungeni kufanya nini?

2. Ikiwa muundo wa Serikali 3 ni
mapendekezo ya wananchi japo idadi ya
waliotoa maoni hayo haikuwa kubwa
ukilinganisha na waliotaka mahakama ya
KADHI kwanini uliuweka muundo huo na
mhakama ya KADHI hamkuiweka au
hayakuwa maoni ya wananchi, na ikiwa
mliona yanaweza kuleta mtafaruku kidini,
kwanini mliweka muundo wa serikali 3 ikiwa
nao mlijua utaleta mtafaruku? Au yale maoni
yaliyotolewa ya kuwepo mahakama ya kadhi
yalikuwa sio ya wanchi? Na yawananchi ni
yale ya muundo wa serikali 3?

3. Wapo ambao hawakutaja muundo wa
serikali ila mkasema eti kwa namna
walivyokuwa wakitoa maoni yao mliona
kabisa muelekeo wao ni waserikali 3, hivi
mlikuwa na kipaji gani cha kujua kilicho
kichwani kwa mtu aidha serikali 3 au 4 nk?

4. Kwanini mnalazimisha wananchi waipende
rasimu mliyoiwasilisha ninyi, na utashi wa
kweli ni upi kwa mwananchi, ni juu ya rasimu
mliyoitoa nyinyi au iliyorekebiswa na BUNGE,
na kama ni hivyo nani mwenye uhalali wa
kusema hii ndiyo ya wananchi ikiwa
wananchi wenyewe ni sisi, na mwananchi
yupi ambaye huesabika huyu ndie
mwananchi halali wa kuipitisha katiba na
wale watakao ikubali sio wananchi, na kama
sio wananchi wanaruhusiwa kupiga kura ya
maoni hayo?

5. Kwanini unapinga uwepo wa baraza la
vijana inamaana hupendi vijana wawe na
baraza? Ulitaka wawe na kaibara kamoja
kama ...............

6. MWISHO tambua wapo wanaoamini na
kuiona RASIMU ya WARIOBA ndio nzuri kwao
na wapo wanaiona KATIBA
INAYOPENDEKEZWA ya CHENGE ndio nzuri
kwao. Kamwe wanaadamu hawawezi kuwa
na muono wa aina moja.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...ayopendekezwa-na-bunge-maalumu-ya-katiba.html
 
Kamwe Tume (WAJUMBE 30) haiwezi kuwa juu ya BMK... (WAJUMBE 630: naundwa na Bunge la JMT, baraza la wawakilishi + 201 kutoka Makundi Maalamu ya jamii)...This will never happen on earth!!!

Waangalie wajumbe wa Tume kwa vigezo tofauti na wingi. Kwanza ni weredi na uzoefu. Nadhani hakuna hata mmoja utakaye wekea shaka hilo. Kule bungeni kuna waliofikapo kwa kuwa nyumba ndogo za watu au kuwa watunzi wa nyimbo za mipasho. Kuna walio honga au kununua nafasi hizo. Pili. Tume ilikua na uwakilishi sawa wa vyama vya siasa. Bungeni ccm ni wengi na uwakilishi kukosa mshiko. Tatu. Tume, Iliendesha utoaji mawazo wananchi. Wabunge hawakufanya hilo. Mwisho sio issue ya mmoja kuwa juu mwingine bali ni juu ya ni yupi ana mawazo ya wananchi kuliko mwingine. Of course hapo ni tume.
 
Ni ujinga kufikiri kuwa katiba inatungwa na wataalam wa sheria. Katiba inatungwa na wananchi moja kwa moja ama kwa kutumia wawakilishi kama hawa wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba japo UKAWA walisusa

Hawo wananchi wanaotunga hiyo katiba ndio wale Sitta aliowaita bungeni kwenda kuchukua maoni mapya?? mkatengeneza hiyo katiba iitwayo Katiba ya Chenge?
 
von Meshak,

kwa heshima na taadhima naomba nimsaidie Mzee Warioba kujiba maswali yako. mimi ni miongoni mwa wale ambao tunaunga mkono rasimu iliyowasilishwa na Tume ya Katiba.

1. rasimu imepelekwa bunge maalum la katiba kwasababu sheria ya uandishi wa katiba mpya imeelekeza hivyo. sheria pia imeelekeza kwamba maoni ya wananchi kama yalivyoratibiwa na tume ya katiba ni lazima yaheshimiwe. pia bunge la katiba halina mamlaka ya kubadili msingi wa rasimu iliyowasilishwa na bunge.

2. Tume ilielekeza suala la kadhi lishughulikiwe wakati wa uandishi wa katiba ya Tanganyika. Nadhani tume ilielekeza hivyo kwasababu suala hilo siyo la muungano. Zanzibar tayari wana mahakama yao ya Kadhi bila kuhusisha serikali ya muungano.

3. Kwanza Tume ilielekezwa kwamba lazima udumishe MUUNGANO. Sasa ktk mazingira hayo ikitokea mtoa maoni akapendekeza kuwe na Raisi wa Tanganyika, au bunge la Tanganyika, huyo moja kwa moja kwa kuzingatia hadidu rejea za Tume ya Wariona ataangukia ktk waliopendekeza muungano wa serikali 3.

4. Wajumbe wa Tume ya Warioba wana haki ya kutetea rasimu yao. Wabunge wa bunge maalum ya Katiba nao wana haki ya kutetea rasimu yao. Lakini wote wanatakiwa kutetea rasimu zao kwa weledi na lugha za kistaarabu. Hakuna mwenye haki dhidi ya mwingine. Mwamuzi wa mwisho kuhusu suala hili ni wapiga kura wa Tanzania. Lakini wapiga kura wanatakiwa kufikia maamuzi baada ya kusikiliza kwa makini hoja za pande zote.

5.Binafsi sioni mantiki ya kuwa na baraza la vijana la taifa. Sidhani kama tunahitaji baraza lolote lile la taifa kwa kuzingatia vigezo vya rika au jinsia. Kwa msingi huo siungi mkono baraza pia uwepo wa baraza la wanawake, watoto, wazee, etc etc.

6. Serikali ingezingatia ushauri wa kambi ya upinzani, kama ulivyowasilishwa na Tundu Lissu, kwamba iitishwe kura ya maoni kuhusu suala la muungano na idadi ya serikali kabla ya kuanza uandishi wa katiba, hakika tusingetumbukia ktk mkwamo huu. Kwasababu watawala walikataa ushauri huo mzuri, ndiyo maana zoezi hili limeingia "ukakasi" wa malumbano kati ya wajumbe wa Tume ya Warioba, na wajumbe wa bunge la Katiba.
Well said, huu ndio u great thinker: hoja nzito zilizotolewa kiistaarabu!!
 
Last edited by a moderator:
1. Ikiwa Rasimu ya pili iliyoandikwa na TUME
YA WARIOBA ndio maoni ya wananchi na
iliandikwa kwa ustadi mkubwa na wataalamu
wa masuala ya uandishi wa katiba na wenye
uzoefu ilipelekwa bungeni kufanya nini?

2. Ikiwa muundo wa Serikali 3 ni
mapendekezo ya wananchi japo idadi ya
waliotoa maoni hayo haikuwa kubwa
ukilinganisha na waliotaka mahakama ya
KADHI kwanini uliuweka muundo huo na
mhakama ya KADHI hamkuiweka au
hayakuwa maoni ya wananchi, na ikiwa
mliona yanaweza kuleta mtafaruku kidini,
kwanini mliweka muundo wa serikali 3 ikiwa
nao mlijua utaleta mtafaruku? Au yale maoni
yaliyotolewa ya kuwepo mahakama ya kadhi
yalikuwa sio ya wanchi? Na yawananchi ni
yale ya muundo wa serikali 3?

3. Wapo ambao hawakutaja muundo wa
serikali ila mkasema eti kwa namna
walivyokuwa wakitoa maoni yao mliona
kabisa muelekeo wao ni waserikali 3, hivi
mlikuwa na kipaji gani cha kujua kilicho
kichwani kwa mtu aidha serikali 3 au 4 nk?

4. Kwanini mnalazimisha wananchi waipende
rasimu mliyoiwasilisha ninyi, na utashi wa
kweli ni upi kwa mwananchi, ni juu ya rasimu
mliyoitoa nyinyi au iliyorekebiswa na BUNGE,
na kama ni hivyo nani mwenye uhalali wa
kusema hii ndiyo ya wananchi ikiwa
wananchi wenyewe ni sisi, na mwananchi
yupi ambaye huesabika huyu ndie
mwananchi halali wa kuipitisha katiba na
wale watakao ikubali sio wananchi, na kama
sio wananchi wanaruhusiwa kupiga kura ya
maoni hayo?

5. Kwanini unapinga uwepo wa baraza la
vijana inamaana hupendi vijana wawe na
baraza? Ulitaka wawe na kaibara kamoja
kama ...............

6. MWISHO tambua wapo wanaoamini na
kuiona RASIMU ya WARIOBA ndio nzuri kwao
na wapo wanaiona KATIBA
INAYOPENDEKEZWA ya CHENGE ndio nzuri
kwao. Kamwe wanaadamu hawawezi kuwa
na muono wa aina moja.

Kwa ufupi kama wewe ni mtanzania na unaishi Tz hayo maswali yk yamekuwa yakichambuliwa kupitia vyombo mbali mbali na Tume iliyopewa mamlaka kisheria, Lakini kwa kuongezea naomba ukumbuke kwamba Ile Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilikuwepo kisheria, ambayo Rais naye alipewa mamlaka kisheria kufanya uteuzi na mamlaka ikaruhusu ile tume ichukue, kukusanya na kuchambua maoni ya Watanzania.

Ile Tume haikuwa ni mtu mmoja tu ilikuwa ni watu wenye misimamo tofauti kama anavyopiga kelele Warioba kila siku kuufahamisha uuma na isitoshe ilikuwa na wajumbe kutoka kila kada.

Lakni baada ya tume hii kumaliza kazi yake ya kuchukua maoni ilikaa na kuyafanyia uchambuzi maoni ya Watanzania na kuja na suluhisho au muarobaini wa S3, na kweli Ile Rasimu 2 imeungwa mkono na Watanzania wengi tofauti na hii ya Sitta ama ya Chenge ambayo inaungwa mkono na CCM tu bunge maalum la katiba.

Kuhusu BMK kama ni hivyo usemavyo kwamba liwe na mamlaka kufuta na kubadilisha sidhani kama kungekuwa na haja Rais kuiteuwa ile tume kupita nchin kote kukusanya maoni, hela chungumzima na mishahara ya hiyo kazi karibu miaka miwili sasa unapokuja na kujifanya mtaalamu wa sharia na kuibeza ile Tume na kuanza kujifungia ndani Chenge na Sitta wakatoa ya moyoni mwao na kusema hii ndio katiba wananchi waipigie kura kuikubali ni kama vile kutwanga maji kwenye kinu. Watanzania hatuwezi kukubali.

Sasa kuja hapa na kujaribu ku-challange hii tume na Rasimu iliyopendekezwa kutokana na maoni ya wananchi ni kama vile unajificha mvua wakati mwili mzima usharoa maji.

CCM wanajuwa dhati kwamba mara tu mfumo wa Muungano wa S2 utakapobadilika kuwa shirikisho chama cha Mapinduzi kitapoteza uhai wake, lakini pia watu waliodumu kwenye madaraka miaka nenda miaka rudi watakosa nafasi hizo kutokana na ile Rasimu ilivyojengwa kutokana uwajibikaji wa viongozi kwa umma.

Sasa ukijaribu kuleta vihoja kama hivi ni kama vile munajitekenya na kujishekesha wenyewe hazina msingi wowote ni kama vile munajitia pamba za masikio lakini tayri mumeshasikia. Na sasa napenda nikwambie kitu kimoja hili la Katiba CCM imejitoa thamani zaidi mbele ya macho ya Watanzania walio wengi na matokeo yake ni kuanguka kuliko kuanguka kwenye uchaguzi mkuu ujao 2015.
 
Lizibon na. MSALANI mgekuwa watoto wangu nilishawakana hadharani hamna akili hata ya kujitabua sidhani kama mnajua hata kutawadha
 
Last edited by a moderator:
Kwa ufupi kama wewe ni mtanzania na unaishi Tz hayo maswali yk yamekuwa yakichambuliwa kupitia vyombo mbali mbali na Tume iliyopewa mamlaka kisheria, Lakini kwa kuongezea naomba ukumbuke kwamba Ile Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilikuwepo kisheria, ambayo Rais naye alipewa mamlaka kisheria kufanya uteuzi na mamlaka ikaruhusu ile tume ichukue, kukusanya na kuchambua maoni ya Watanzania.

Ile Tume haikuwa ni mtu mmoja tu ilikuwa ni watu wenye misimamo tofauti kama anavyopiga kelele Warioba kila siku kuufahamisha uuma na isitoshe ilikuwa na wajumbe kutoka kila kada.

Lakni baada ya tume hii kumaliza kazi yake ya kuchukua maoni ilikaa na kuyafanyia uchambuzi maoni ya Watanzania na kuja na suluhisho au muarobaini wa S3, na kweli Ile Rasimu 2 imeungwa mkono na Watanzania wengi tofauti na hii ya Sitta ama ya Chenge ambayo inaungwa mkono na CCM tu bunge maalum la katiba.

Sasa kuja hapa na kujaribu ku-challange hii tume na Rasimu iliyopendekezwa kutokana na maoni ya wananchi ni kama vile unajificha mvua wakati mwili mzima usharoa maji.

CCM wanajuwa dhati kwamba mara tu mfumo wa Muungano wa S2 utakapobadilika kuwa shirikisho chama cha Mapinduzi kitapoteza uhai wake, lakini pia watu waliodumu kwenye madaraka miaka nenda miaka rudi watakosa nafasi hizo kutokana na ile Rasimu ilivyojengwa kutokana uwajibikaji wa viongozi kwa umma.

Sasa ukijaribu kuleta vihoja kama hivi ni kama vile munajitekenya na kujishekesha wenyewe hazina msingi wowote ni kama vile munajitia pamba za masikio lakini tayri mumeshasikia.

hoja kama hizi hawa kula kulala watoto wa ccm hawawezi kusema chochote na ikiwa watakujibu nipi radhi wanifute jf
waje hapa
Ritz
Lizibon
MSALANI
na NAPE MOSES NAUYE
 
Last edited by a moderator:
Kamwe Tume (WAJUMBE 30) haiwezi kuwa juu ya BMK... (WAJUMBE 630: naundwa na Bunge la JMT, baraza la wawakilishi + 201 kutoka Makundi Maalamu ya jamii)...This will never happen on earth!!!


Mkuu...so do you think kulikua na umuhimu wa kuundwa kwa tume ya Warioba? Au raisi alivunja katiba?
 
Kamwe Tume (WAJUMBE 30) haiwezi kuwa juu ya BMK... (WAJUMBE 630: naundwa na Bunge la JMT, baraza la wawakilishi + 201 kutoka Makundi Maalamu ya jamii)...This will never happen on earth!!!

..nadhani zoezi la uandishi wa katiba ni tofauti kidogo na hivyo unavyofikiria.

..tume ya katiba imezunguka nchi nzima kuchukua maoni ya wananchi kuhusu muundo wa katiba.

..wajumbe wa bunge la katiba hawajauliza wananchi kuhusu suala hili, kwa hivyo huwezi kusema kwa uhakika kuwa wanawasilisha maoni ya wananchi huko bungeni. pia huwezi kusema wao wako "juu" ya wajumbe wa tume ya katiba.

..mtizamo wangu ni kwamba wajumbe wa bunge maalum wanawakilisha maoni au mawazo ya MAKUNDI[ccm,cdm,cuf,nccr, etc etc..] yao ni siyo mawazo ya wananchi.
 
Ni ujinga kufikiri kuwa katiba inatungwa na wataalam wa sheria. Katiba inatungwa na wananchi moja kwa moja ama kwa kutumia wawakilishi kama hawa wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba japo UKAWA walisusa

Hii kitu umesoma wapi, au ndo kukaririshwa na Nape, poleni sana msiojitambua kiakili. Japo? nini maana yake hapo kama unaelewa ulokiandika?
 
1.
5. Kwanini unapinga uwepo wa baraza la
vijana inamaana hupendi vijana wawe na
baraza? Ulitaka wawe na kaibara kamoja
kama ...............

Mambo ya vijana sio jambo la muungano...Zanzibari wanalao..sasa hilo la kwenye hiyo kitu ya CHENGE ni ya watanganyika pekee.....katika JOHO refu la MUUNGANO....
 
Hasira walizo nazo wananchi MWishoe HII NCHI ITAINGIA VITANI TU
 
Kamwe Tume (WAJUMBE 30) haiwezi kuwa juu ya BMK... (WAJUMBE 630: naundwa na Bunge la JMT, baraza la wawakilishi + 201 kutoka Makundi Maalamu ya jamii)...This will never happen on earth!!!

Nawe ukumbuke pia Tume ilifanya kazi yake kwa miezi 20 lakini Bunge halijapata hata miezi sita. kwa hiyo tume ilifanya kazi yake ikiwa imetulia zaidi ukilinganisha na bunge linalofanya kwa papara.
 
Mkuu...so do you think kulikua na umuhimu wa kuundwa kwa tume ya Warioba? Au raisi alivunja katiba?
1. Wananchi kutoa maoni
2. Mabaraza ya kata kupitia Rasimu/Draft 1
3. Tume kutoa Rasimu/Draft 2
4. Bunge la Katiba kujadili /kuchambua na kutoka na Katiba inayopendekezwa/Proposed Constituion.
5. Wananchi ku-Approve via referendum ( Kura ya maoni)

HATUA ZOTE HIZO ZILIKUWA NI MIHUMU... Na zinaenda Kwa mtiririko huo.

Kama ni nani Ana Nguvu zaidi ni 5 hapo juu... Kushuka chini ... Ni UHUNI kusema hatua no. 3 ndio alikuwa kinara wa KILA kitu!
 
Back
Top Bottom