Tembulukoje
JF-Expert Member
- Jun 14, 2014
- 397
- 143
Nimekaa nikatafakari sana, nikajiuliza sana, nikaamua na mimi kutoa maoni yangu juu ya mwenendo wa siasa hapa nchini Tanzania hasa kwa kipindi hiki tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu. Nimejiuliza maswali muhimu mawili (2) magumu ambayo nimeshindwa kupata majibu kusuhu huyu mgombea wa uraisi kupitia umoja wa vyama vya UKAWA.
1. Kwa nini vijana wengi hasa wasiokuwa na ajira, walalahoi na mamalishe humshabikia sana Lowassa wakati wasomi, wazee makini na kiujumla watu "MAKINI" wakimpinga? Je ni kwa sababu Lowassa "ANAUCHUKIA" umasikini? Je Lowassa akiwa raisi ataoneshaje kuwa ni kwel unauchukia umasikini kwa hawa mamalishe na hawa vijana wasiokuwa na kazi? Atafanya nini hasa kwa haya makundi anayopenda "KUJIOSHEA" wakati wa hoja zake za kutafuta kura? Nachokijua mimi hizo ni kauli za kisiasa tu katika kutafuta kura. Nasema hivyo kwa sabubu zifuatazo:-
a) Kwanza mimi siamini kama kuna urafiki kati ya "TAJIRI" na "MASIKINI". Hakuna huo urafiki, haupo.
b) Nyuma ya Lowassa kuna watu kama Lostam, Kalamagi ambao wote ni matajiri. Lowassa anatumia umasiki wa haya makundi kuyalaghai akijua pia kuwa ni ‘MASIKINI WA KUFIKIRI' na wasiokuwa na uwezo wa kutafakari mambo.
c) Tatizo la ajira kwa vijana kwa sasa halitatuliki kwa njia yoyote, hata kama ni kujenga viwanda kila kata. Vijana wanaohitimu vyuo ni wengi sana kila mwaka. Uwiano wa kila kazi moja inayotangazwa kwa sasa ni 1:90. Na bado watu tunazaa kama hatuna akili nzuri. Tatizo la ajira kwa sasa sio tena kusema utajenga viwanda. Hebu kama kweli unataka kuwa raisi njoo na hoja tofauti ili watu "MAKINI" tukuelewe.
2. Kwa nini Lowassa ameng'ang'ania sana uraisi? Kuna biashara gani pale ikulu? Hadi kufikia hatua ya kukisaliti na kukihama chama? Ana ajenda gani? Na kama ameweza kukisaliti chama kilichomlea tangu mwaka 1977 takribani miaka 38 atashindwa kuisaliti nchi kweli kwa miaka 5?
Lowassa kiujumla yuko na uroho wa madaraka, uraisi kwake ni kufa na kupona. Na mbaya zaidi anatumia kundi la vijana hasa wasiokuwa na ajira (wasiokuwa na uwezo wa kufikiria na kudadavua mambo) ambao ndo wengi kuwalaghai na kauli ya "NACHUKIA UMASIKI" wakati hakuna urafiki kati yake yeye tajiri na umasikini.
1. Kwa nini vijana wengi hasa wasiokuwa na ajira, walalahoi na mamalishe humshabikia sana Lowassa wakati wasomi, wazee makini na kiujumla watu "MAKINI" wakimpinga? Je ni kwa sababu Lowassa "ANAUCHUKIA" umasikini? Je Lowassa akiwa raisi ataoneshaje kuwa ni kwel unauchukia umasikini kwa hawa mamalishe na hawa vijana wasiokuwa na kazi? Atafanya nini hasa kwa haya makundi anayopenda "KUJIOSHEA" wakati wa hoja zake za kutafuta kura? Nachokijua mimi hizo ni kauli za kisiasa tu katika kutafuta kura. Nasema hivyo kwa sabubu zifuatazo:-
a) Kwanza mimi siamini kama kuna urafiki kati ya "TAJIRI" na "MASIKINI". Hakuna huo urafiki, haupo.
b) Nyuma ya Lowassa kuna watu kama Lostam, Kalamagi ambao wote ni matajiri. Lowassa anatumia umasiki wa haya makundi kuyalaghai akijua pia kuwa ni ‘MASIKINI WA KUFIKIRI' na wasiokuwa na uwezo wa kutafakari mambo.
c) Tatizo la ajira kwa vijana kwa sasa halitatuliki kwa njia yoyote, hata kama ni kujenga viwanda kila kata. Vijana wanaohitimu vyuo ni wengi sana kila mwaka. Uwiano wa kila kazi moja inayotangazwa kwa sasa ni 1:90. Na bado watu tunazaa kama hatuna akili nzuri. Tatizo la ajira kwa sasa sio tena kusema utajenga viwanda. Hebu kama kweli unataka kuwa raisi njoo na hoja tofauti ili watu "MAKINI" tukuelewe.
2. Kwa nini Lowassa ameng'ang'ania sana uraisi? Kuna biashara gani pale ikulu? Hadi kufikia hatua ya kukisaliti na kukihama chama? Ana ajenda gani? Na kama ameweza kukisaliti chama kilichomlea tangu mwaka 1977 takribani miaka 38 atashindwa kuisaliti nchi kweli kwa miaka 5?
Lowassa kiujumla yuko na uroho wa madaraka, uraisi kwake ni kufa na kupona. Na mbaya zaidi anatumia kundi la vijana hasa wasiokuwa na ajira (wasiokuwa na uwezo wa kufikiria na kudadavua mambo) ambao ndo wengi kuwalaghai na kauli ya "NACHUKIA UMASIKI" wakati hakuna urafiki kati yake yeye tajiri na umasikini.