shadow recruit
JF-Expert Member
- Dec 28, 2011
- 1,844
- 384
Baada ya kufuatilia na kushiriki mjadala huu mpana wenye maslahi kwa taifa letu nimepata maswali kumi ambayo ndugu yangu david kafulila anaweza kunisaidia kuyajibu kuhusu iptl na escrow.
1.JE Anaijua historia ya iptl vizuri au anaifahamu kwa kupitia kusoma raia mwema na machapisho ya zitto kabwe
2.JE Anafahamu mchakato wa mauziano ya hisa ulivyofanyika kati ya mechmar corporation (malaysia)berhard kwenda pap,anajua kwamba seth aliomba kuuziwa sehemu ya hisa za iptl tanzania yaani 70% za iptl zilizokuwa chini ya mechmar lakini akakataliwa kutokana na sheria za biashara kimataifa kutoruhusu mwangalizi kununua hisa za kampuni anayoisimamia,na hivyo hisa kuuzwa kwa kampuni ya piper link,hivyo seth singh alilazimika kuomba piperlink imuuzie hisa zake ndani ya iptl tanzania,na manunuzi hayo yalifuata taratibu zote za kisheria ikiwa pamoja na kununua madeni yote ya kampuni,je analijua hili?
3.JE Kafulila anafahamu masuala yote yalioleta utata kuhusu capacity charges za kuzalisha umeme kati ya iptl na tanesko yaliamriwa na kupatiwa ufumbuzi katika mahakama ya kimataifa ya biashara,na masuala ya mgawanyo wa mapato kati ya wanahisa yaani vip na mechmar yalipatiwa ufumbuzi katika mahakama kuu tanzania chini ya jaji ukama,hukumu iliyopelekea kuanzishwa kwa akaunti ya escrow ambayo kimsingi ilikua inatunza malipo ya wanahisa yanayotokana na mauzo ya umeme wanaozalisha na kuizia taneko baada ya usuluhishi wao mahakama ya kibiashara kuhusu capacity charges.
4.JE Kafulila anafamu kuwa vip iliuza hisa zake kwa pap baada ya kufikia makubaliano ya bei ya hisa zote 30% za vip?,Na kumfanya harbinder seth singh kuwa mmiliki halali wa asilimia zote mia za iptl
5.JE Kafulila anafahamu kuwa mmiliki wa vip bwana rugemalira sio mtumishi wa umma na hivyo kama raia wengine ana haki ya kutumia fedha zake alizopata kwa njia halali ya kuuza hisa zake ndani ya kampuni anavyotaka bila kuvunja sheria,bila kuingiliwa na mtu yeyote hata kama amehonga mwanamke,ametupa jalalani,amekunywa pombe au ametoa msikitini/kanisani/shuleni/ametoa msaada kwenye kwaya/kumpa mchepuko hata bilioni mbili,maana ni zake na kafulila hatakiwi kufuatilia maisha ya mtu binafsi maana hata rugemalira afuatilii maisha ya kafulila.
6.JE Kafulila anafahamu kuwa iptl ndio kampuni pekee inayookoa fedha za watanzania kwenye nishati kwasababu ya kuwauzia umeme kwa bei nafuu kuliko kampuni anayoipigia debe na iliyomtuma kuichafua iptl yaani symbioon ambayo inaiuzia tanesco umeme unit moja kwa zaidi ya elfu moja wakati iptl inaiuzia umeme tanesco chini ya shiling mia tano kwa unit na imeanza mazungumzo kushusha umeme hadi sh 90 kwa unit,je haoni anatumika vibaya na kampuni yenye wivu wa kibiashara kuchafua iptl ambayo ni mkombozi wa tanzania
7.JE Kafulila ana majibu gani baada ya kulidanganya bunge kuhusu mmiliki wa iptl harbinder seth singh kufukuzwa na kutotakiwa kufanya biashara kenya kwa sababu ya ufisadi wakati wiki iliyopita iptl ilikabidhiwa barua na waziri wa nishati kenya kupewa tender ya kuzalisha umeme mw 2000.?
8.JE Kafulila anazungumziaje tuhuma za yeye kupokea milioni tisini kutoka kwa wafanyabiashara wakubwa walioathirika na kitendo cha waziri mpya wa nishati na madini sospeter muhongo kufunga mirija ya kifisadi waliyokuwa wanatumia kujinufaisha na kuifilisi nchi (rostam,mengi,mkono) ili awachafue na kuwakomoa muhongo na katibu wake maswi?
9.JE Kafulila haoni ni muda sahihi wa yeye kuwataka radhi iptl na watanzania kwa kutumika na mafisadi ili kurudisha heshima yake kwa watanzania.
10.JE Kafulila anataka tumtambuaje baada ya haya yote,mpigaji?/Mzalendo/mtu wa kutumia fursa/au mtumikaji?
Naomba kuwasilisha ili mkuu kafulila aweze kuyajibu,karibuni kwenye mjadala
1.JE Anaijua historia ya iptl vizuri au anaifahamu kwa kupitia kusoma raia mwema na machapisho ya zitto kabwe
2.JE Anafahamu mchakato wa mauziano ya hisa ulivyofanyika kati ya mechmar corporation (malaysia)berhard kwenda pap,anajua kwamba seth aliomba kuuziwa sehemu ya hisa za iptl tanzania yaani 70% za iptl zilizokuwa chini ya mechmar lakini akakataliwa kutokana na sheria za biashara kimataifa kutoruhusu mwangalizi kununua hisa za kampuni anayoisimamia,na hivyo hisa kuuzwa kwa kampuni ya piper link,hivyo seth singh alilazimika kuomba piperlink imuuzie hisa zake ndani ya iptl tanzania,na manunuzi hayo yalifuata taratibu zote za kisheria ikiwa pamoja na kununua madeni yote ya kampuni,je analijua hili?
3.JE Kafulila anafahamu masuala yote yalioleta utata kuhusu capacity charges za kuzalisha umeme kati ya iptl na tanesko yaliamriwa na kupatiwa ufumbuzi katika mahakama ya kimataifa ya biashara,na masuala ya mgawanyo wa mapato kati ya wanahisa yaani vip na mechmar yalipatiwa ufumbuzi katika mahakama kuu tanzania chini ya jaji ukama,hukumu iliyopelekea kuanzishwa kwa akaunti ya escrow ambayo kimsingi ilikua inatunza malipo ya wanahisa yanayotokana na mauzo ya umeme wanaozalisha na kuizia taneko baada ya usuluhishi wao mahakama ya kibiashara kuhusu capacity charges.
4.JE Kafulila anafamu kuwa vip iliuza hisa zake kwa pap baada ya kufikia makubaliano ya bei ya hisa zote 30% za vip?,Na kumfanya harbinder seth singh kuwa mmiliki halali wa asilimia zote mia za iptl
5.JE Kafulila anafahamu kuwa mmiliki wa vip bwana rugemalira sio mtumishi wa umma na hivyo kama raia wengine ana haki ya kutumia fedha zake alizopata kwa njia halali ya kuuza hisa zake ndani ya kampuni anavyotaka bila kuvunja sheria,bila kuingiliwa na mtu yeyote hata kama amehonga mwanamke,ametupa jalalani,amekunywa pombe au ametoa msikitini/kanisani/shuleni/ametoa msaada kwenye kwaya/kumpa mchepuko hata bilioni mbili,maana ni zake na kafulila hatakiwi kufuatilia maisha ya mtu binafsi maana hata rugemalira afuatilii maisha ya kafulila.
6.JE Kafulila anafahamu kuwa iptl ndio kampuni pekee inayookoa fedha za watanzania kwenye nishati kwasababu ya kuwauzia umeme kwa bei nafuu kuliko kampuni anayoipigia debe na iliyomtuma kuichafua iptl yaani symbioon ambayo inaiuzia tanesco umeme unit moja kwa zaidi ya elfu moja wakati iptl inaiuzia umeme tanesco chini ya shiling mia tano kwa unit na imeanza mazungumzo kushusha umeme hadi sh 90 kwa unit,je haoni anatumika vibaya na kampuni yenye wivu wa kibiashara kuchafua iptl ambayo ni mkombozi wa tanzania
7.JE Kafulila ana majibu gani baada ya kulidanganya bunge kuhusu mmiliki wa iptl harbinder seth singh kufukuzwa na kutotakiwa kufanya biashara kenya kwa sababu ya ufisadi wakati wiki iliyopita iptl ilikabidhiwa barua na waziri wa nishati kenya kupewa tender ya kuzalisha umeme mw 2000.?
8.JE Kafulila anazungumziaje tuhuma za yeye kupokea milioni tisini kutoka kwa wafanyabiashara wakubwa walioathirika na kitendo cha waziri mpya wa nishati na madini sospeter muhongo kufunga mirija ya kifisadi waliyokuwa wanatumia kujinufaisha na kuifilisi nchi (rostam,mengi,mkono) ili awachafue na kuwakomoa muhongo na katibu wake maswi?
9.JE Kafulila haoni ni muda sahihi wa yeye kuwataka radhi iptl na watanzania kwa kutumika na mafisadi ili kurudisha heshima yake kwa watanzania.
10.JE Kafulila anataka tumtambuaje baada ya haya yote,mpigaji?/Mzalendo/mtu wa kutumia fursa/au mtumikaji?
Naomba kuwasilisha ili mkuu kafulila aweze kuyajibu,karibuni kwenye mjadala