MasterCard vs. Visa: What’s the Difference?

MasterCard vs. Visa: What’s the Difference?

Jospina

JF-Expert Member
Joined
Apr 19, 2013
Posts
2,421
Reaction score
1,395
wadau,
naomba kujua tofauti ya hizi kadi za kibenki?? benefits au faida ya kuwa na aina fulani ya kadi kati ya hizo?
shukrani
 
Most mastercards are credit card, Visa Card can be Debit or Credit but benefits is u can withdrawal money anywhere worldwide
 
wadau,
naomba kujua tofauti ya hizi kadi za kibenki?? benefits au faida ya kuwa na aina fulani ya kadi kati ya hizo?
shukrani

Kimsingi hazina tofauti kabisa.

Zote zinakubalika sehemu nyingi sana duniani.

Sijawahi kukutana na sehemu ambayo inakubali matumizi ya Visa halafu ikatae matumizi ya MasterCard.

Nishawahi kutumia kadi (Visa na MasterCard) za Bank of America kwenye ATM ya CRDB, Bariadi, Simiyu!

Na zote hizo ni kampuni za Kimarekani.

EMT
, remember this debate?
 
Kimsingi hazina tofauti kabisa.

Zote zinakubalika sehemu nyingi sana duniani.

Sijawahi kukutana na sehemu ambayo inakubali matumizi ya Visa halafu ikatae matumizi ya MasterCard.

Nishawahi kutumia kadi (Visa na MasterCard) za Bank of America kwenye ATM ya CRDB, Bariadi, Simiyu!

Na zote hizo ni kampuni za Kimarekani.

EMT
, remember this debate?

labda VISA electron ndio ina limitations kidogo kuliko mastercard...lakini VISA na MASTERCARD zote unatumia vizuri tu sehemu nyingi duniani na ndio advantage ya dhidi ya card nyingine kama MAESTRO etc
 
watu wa mabenki na mahesabu mnaposema Debit card mnamaanisha nini au credit card maana yake kwa mimi mtoto wa Tandale Uzuri kwa Bibi Nyau?
 
watu wa mabenki na mahesabu mnaposema Debit card mnamaanisha nini au credit card maana yake kwa mimi mtoto wa Tandale Uzuri kwa Bibi Nyau?

Debit card inamaanisha kadi aitumiayo mtu ambapo pesa inatoka moja kwa moja kutoka kwenye akaunti yake.

Credit card ni kadi aitumiayo mtu ambapo pesa anayoitumia ni mkopo tu ambao unatakiwa ulipwe baadaye kulingana na makubaliano yaliyoafikiwa.
 
Debit card inamaanisha kadi aitumiayo mtu ambapo pesa inatoka moja kwa moja kutoka kwenye akaunti yake.

Credit card ni kadi aitumiayo mtu ambapo pesa anayoitumia ni mkopo tu ambao unatakiwa ulipwe baadaye kulingana na makubaliano yaliyoafikiwa.

Mkuu, huu mkopo una sura gani? Je, "overdraft" nayo ni mkopo? Maana kuna bank (nchi fulani) zinatoa "debit card" na mteja anavuta "overdraft"!!
 
Zote sawa kama tigo na voda au Nmb na crdb au benz na toyota au samsung na Sony au .... au ...
 
The question here is one of specificity.

Which Visa and which Mastercard?

The banal names have a myriad configurations, which makes the Mastercard vs.Visa question lacking specificity to give it a meaningful reply.
 
Mkuu, huu mkopo una sura gani?

Kwa sura unamaanisha nini? Mambo kama ya APR?

Je, "overdraft" nayo ni mkopo?

Overdraft si mkopo by definition.

Ingawa kwa baadhi ya mabenki uki-overdraw utalimwa overdraft fee(s) na kudaiwa kiasi ulicho-overdraw.

Maana kuna bank (nchi fulani) zinatoa "debit card" na mteja anavuta "overdraft"!!

Benki nyingi za majuu nizijuazo mimi huwa zinatoa huduma ya overdraft protection. Mara nyingi hii huduma huwa si ya moja kwa moja (automatic). Ni mpaka uiweke mwenyewe. Ukiwa nayo halafu tuseme utumie kadi yako sehemu kwa kiasi ambacho hakipo kwenye akaunti yako, kadi itagoma.

Ona haya maelezo machache kuhusu overdraft protection ya Bank of America:


  • [*]
    Bank of America offers Overdraft Protection which allows a checking account to be linked to another Bank of America account to help provide protection against returned items or overdrafts. During nightly posting, if there are insufficient funds to cover a transaction, funds are automatically transferred from the Available Balance in the linked account.

    [*]You can receive account Alerts to your mobile phone or email to notify you when your Available Balance falls below a threshold you determine.
    [*]
 
Nafikiri kuna mtu ameiba ID ya Nyani Ngabu huwa hatoi maelezo yasiyokwenda shule kama haya, pengine kazeeka siku hizi maana ukizeeka na akili inakuwa kama ya Mugabe.
 
APR, nimecheka usiku huu!!
Nyani Ngabu, hilo neno la sura nililiweka kuomba ufafanuzi wa hayahaya uliyoyaeleza! Umewasahau wazee wetu kule "Peripherals" kila kitu kwao ni kabila; akizoea Mirinda siku ukampa Pepsi, akionja atauliza "Hii soda kabila gani?"...Ndiyo maana na mimi nikatumia kichombezo cha neno "sura" kuomba huu ufafanuzi!
Btn, Pokea gwala kwa ufafanuzi



Kwa sura unamaanisha nini? Mambo kama ya APR?



Overdraft si mkopo by definition.

Ingawa kwa baadhi ya mabenki uki-overdraw utalimwa overdraft fee(s) na kudaiwa kiasi ulicho-overdraw.



Benki nyingi za majuu nizijuazo mimi huwa zinatoa huduma ya overdraft protection. Mara nyingi hii huduma huwa si ya moja kwa moja (automatic). Ni mpaka uiweke mwenyewe. Ukiwa nayo halafu tuseme utumie kadi yako sehemu kwa kiasi ambacho hakipo kwenye akaunti yako, kadi itagoma.

Ona haya maelezo machache kuhusu overdraft protection ya Bank of America:


 
Huh?

Kwa hiyo nilichoandika ni pumba au...?

Hukuandika pumba, hivi ni wewe kweli? Naona maelezo yako dhoofu kidogo mimi sitaki kuingilia... ... .. huku Alaska baridi imeanza bana.
 
Hukuandika pumba, hivi ni wewe kweli? Naona maelezo yako dhoofu kidogo mimi sitaki kuingilia... ... .. huku Alaska baridi imeanza bana.

Kaka, sijibu maswali ya mtihani hapa na wala siandiki research paper.

Lakini ningeshukuru kama ungenionyesha udhoofu wake, maana mimi nimejibu kwa kadri swali au maswali yalivyoulizwa na kwa uwezo wangu.

Au umeamua kunizingua tu wewe...?
 
Kimsingi hazina tofauti kabisa.

Zote zinakubalika sehemu nyingi sana duniani.

Sijawahi kukutana na sehemu ambayo inakubali matumizi ya Visa halafu ikatae matumizi ya MasterCard.

Nishawahi kutumia kadi (Visa na MasterCard) za Bank of America kwenye ATM ya CRDB, Bariadi, Simiyu!

Na zote hizo ni kampuni za Kimarekani.

EMT
, remember this debate?

mkuu mbona mimi Mara nyingi kuna sehemu huwa wanakataa master card ( credit)?
 
mkuu mbona mimi Mara nyingi kuna sehemu huwa wanakataa master card ( credit)?

Kwanza, sikuandika zinakubalika sehemu zote. Niliandika zinakubalika sehemu nyingi sana duniani. Jambo ambalo ni kweli. Sasa sehemu nyingi sana si sehemu zote.

Pili, kati ya sehemu wanazozikubali kadi zote mbili na zile ambazo wanakubali moja tu, zile unazozijua wewe, zipi ni nyingi kuliko?
 
Nafikiri kuna mtu ameiba ID ya Nyani Ngabu huwa hatoi maelezo yasiyokwenda shule kama haya, pengine kazeeka siku hizi maana ukizeeka na akili inakuwa kama ya Mugabe.

Te te teee ImageUploadedByJamiiForums1418338323.424333.jpg
 
Back
Top Bottom