real G
JF-Expert Member
- Feb 7, 2013
- 5,227
- 5,302
Habari wanaJF?
Lowassa alikua amepanga kuwa rais wa hii nchi tangia miaka angalau mitatu hivi nadhani hivyo ni mtu ambaye alikua anasoma na kupanga mipango mikubwa jinsi ya kuleta maendeleo kwenye hii nchi tofauti na Magufuli ambaye inaonekana ni kama alishtukizwa tu.
Ila kwenye kampeni zake nikisikiliza na nikitafuta kwenye mitandao mi sijaona akitoa mipango ya jinsi ya kuibadilisha hii nchi ki ukweli ukweli
mi nasikia akitoa ahadi ndogo ndogo tu kama vile kusaidia mama ntilie, bodaboda, wachimbaji wadogowadogo, sijaona namna ambavyo atatatua matatizo makuu kwenye hii nchi kama vile ukosefu wa ajira, shilingi kuporomoka, usimamizi mzuri wa rasilimali zetu kama gesi, bandari , vyanzo vya maji, miji kukua bila mpangilio {foleni}, kilimo duni, ufisadi na rushwa n.k.
Mimi nataka mabadiliko lakini kwa mtu sahihi, naomba mnisaidie hapa..
Lowassa alikua amepanga kuwa rais wa hii nchi tangia miaka angalau mitatu hivi nadhani hivyo ni mtu ambaye alikua anasoma na kupanga mipango mikubwa jinsi ya kuleta maendeleo kwenye hii nchi tofauti na Magufuli ambaye inaonekana ni kama alishtukizwa tu.
Ila kwenye kampeni zake nikisikiliza na nikitafuta kwenye mitandao mi sijaona akitoa mipango ya jinsi ya kuibadilisha hii nchi ki ukweli ukweli
mi nasikia akitoa ahadi ndogo ndogo tu kama vile kusaidia mama ntilie, bodaboda, wachimbaji wadogowadogo, sijaona namna ambavyo atatatua matatizo makuu kwenye hii nchi kama vile ukosefu wa ajira, shilingi kuporomoka, usimamizi mzuri wa rasilimali zetu kama gesi, bandari , vyanzo vya maji, miji kukua bila mpangilio {foleni}, kilimo duni, ufisadi na rushwa n.k.
Mimi nataka mabadiliko lakini kwa mtu sahihi, naomba mnisaidie hapa..