Massawe ateuliwa Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu TPSF

Massawe ateuliwa Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu TPSF

Mafyangula

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2025
Posts
515
Reaction score
916
Shirikisho la Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) limeutaarifu umma, wanachama wake, washirika, na wadau kuhusu mabadiliko ya uongozi wa Shirikisho.

Oktoba 3, 2025, Baraza la Uongozi la TPSF lilimsimamisha kazi Afisa Mtendaji Mkuu, Bw. Raphael Maganga, na kuagiza kufanyika kwa ukaguzi wa kiuchunguzi (forensic audit) kufuatia wasiwasi uliobainika kuhusu masuala ya utawala na taratibu za ndani.

Baada ya kukamilika, ripoti ya ukaguzi wa kiuchunguzi ilipitiwa kupitia mifumo ya utawala na nidhamu ya Shirikisho.

Kwa kuzingatia mapendekezo yaliyotokana na mchakato huo, Baraza la Uongozi liliamua kusitisha mkataba wa ajira wa Bw. Raphael Maganga kwa misingi ya utovu wa nidhamu, kuanzia Disemba 29, 2025.

Ili kuhakikisha mwendelezo wa uongozi na uendeshaji usiokatizwa wa shughuli za Shirikisho, Baraza la Uongozi limemteua Bw. Deogratius Massawe kuwa Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TPSF, kuanzia Disemba 29, 2025, hadi hapo itakapotangazwa vinginevyo.

TPSF inaendelea kushikamana kikamilifu na misingi ya utawala bora, uwajibikaji, uwazi, na uadilifu, na itaendelea kushirikiana kwa karibu na Wanachama wake, Serikali, Washirika wa Maendeleo, na sekta binafsi kwa ujumla ili kuendeleza maslahi ya sekta binafsi nchini Tanzania.
 
Kwanini ni muhimu? TPSF kuna hela sana? Hicho cheo kina faida gani? Mi huwa naona TPSF ni taasisi tu ya kawaida, au kuna umate umate?

Maana kwa sisi wabongo, penye hela hapakosi fitina.
 
Umate mate upo sana tu pale TPSF
Wacha wee, basi fitina hizo. Halafu hiyo nafasi ina exposure nzuri sana. Huyo Maganga kule Linkedin alikuwa kila mara anaenda kujumuika vikao na wazito wa serikali. Itakuwa ni ka cheo kazuri
 
Taarifa kwa umma.
 

Attachments

  • IMG-20260108-WA0060.jpg
    IMG-20260108-WA0060.jpg
    53.2 KB · Views: 6
Back
Top Bottom