Masoud Djuma: Wachezaji wa Simba SC wanaamini ushirikina

py thon

JF-Expert Member
Sep 11, 2016
2,471
4,424
Ubovu wa Gyan kumbe ulisababishwa na imani za kurogwa”-kocha Simba

Kaimu kocha mkuu wa Simba Masoud Djuma amesema, wakati anaingia Simba alikuwa haamini kama Nicholas Gyan ni mchezaji mzuri lakini baada ya kukaa na kuzungumza na mchezaji huyo alimwambia kwamba ameambiwa anarogwa ndio maana anashindwa kufanya vizuri.

Baada ya kocha huyo kukaa, kuzungumza na kumshauri Gyan kuachana na imani hizo za kurogwa, Gyan ameonesha kiwango cha hali ya juu.

Djuma pia amesema, hampangi mchezaji kwa sababu ya jina au undugu ndiyo maana Mavugo licha ya kuwa ni mburundi mwenzake lakini hachezi kwa sababu hayuko fiti, atakapokuwa sawa atapata nafasi ya kucheza.

“Nilivyokuja Simba nilimwambia Gyan wewe kwangu sio mchezaji, alikuwa hawezi kutuliza mpira wala kupiga pasi kwenye mpira kama huwezi kutuliza mpira wala kupiga pasi huwezi kuwa mchezaji.

“Nikajakujua kwamba ana matatizo kichwani aliambiwa amerogwa, nikamwambia kama ametoka Ghana akiwa mchezaji mzuri iweje ashindwe kucheza, nikamwambia aachane na hayo mambo yeye acheze mpira. Siku ya kwanza alipofanya mazoezi mazuri nilimwita nikamwambia tangu nifike Simba leo ndiyo nakuona umefanya mazoezi mazuri”-Masoud Djuma kuhusu Gyan kuamini katika ushirikina.”

eb96fa2c175e6fe9c6df2d65ee73eb7f.jpg
 
Asilimia kubwa ya watu wanaamini ndumba apa jiran yangu kuna kuna mama anauza mandazi juzi anambia anarogwa biashara haiendi
 
Nina banda la kuonyeshea mpira
Na projector clear kabisa ila watu hawawi wengi
Jirani yangu picha yake sio quality kama yangu anapata wengi kiasi
Mbali kidogo na Mimi wanatumia tv flat wanapata watu kibao
Wengi walinishauri niende kwa mganga nimekataa
Juzi kaja mzee akaniambia kumbe pazuri na projector ya maaana nilikua sijuwi nikamwambia hakuna watu akanishauri niende kwa mganga nimepotezea

Watu wengi wana iman za kishirikina
 
Ubovu wa Gyan kumbe ulisababishwa na imani za kurogwa”-kocha Simba

Kaimu kocha mkuu wa Simba Masoud Djuma amesema, wakati anaingia Simba alikuwa haamini kama Nicholas Gyan ni mchezaji mzuri lakini baada ya kukaa na kuzungumza na mchezaji huyo alimwambia kwamba ameambiwa anarogwa ndio maana anashindwa kufanya vizuri.

Baada ya kocha huyo kukaa, kuzungumza na kumshauri Gyan kuachana na imani hizo za kurogwa, Gyan ameonesha kiwango cha hali ya juu.

Djuma pia amesema, hampangi mchezaji kwa sababu ya jina au undugu ndiyo maana Mavugo licha ya kuwa ni mburundi mwenzake lakini hachezi kwa sababu hayuko fiti, atakapokuwa sawa atapata nafasi ya kucheza.

“Nilivyokuja Simba nilimwambia Gyan wewe kwangu sio mchezaji, alikuwa hawezi kutuliza mpira wala kupiga pasi kwenye mpira kama huwezi kutuliza mpira wala kupiga pasi huwezi kuwa mchezaji.

“Nikajakujua kwamba ana matatizo kichwani aliambiwa amerogwa, nikamwambia kama ametoka Ghana akiwa mchezaji mzuri iweje ashindwe kucheza, nikamwambia aachane na hayo mambo yeye acheze mpira. Siku ya kwanza alipofanya mazoezi mazuri nilimwita nikamwambia tangu nifike Simba leo ndiyo nakuona umefanya mazoezi mazuri”-Masoud Djuma kuhusu Gyan kuamini katika ushirikina.”

eb96fa2c175e6fe9c6df2d65ee73eb7f.jpg
Hilo ni jambo la kawaida sana sio wachezaji team zote zina kamati ya UFUNDI
 
Back
Top Bottom