Hatimaye ngome ya Chadema imevunjwa na waliokuwa viongozi wa chadema jimbo la Kahama kutokana na kutokubaliana na ujio wa James Lembeli katika jimbo hilo huku wazawa, wazalendo na waanzilishi wa chadema katika jimbo hilo wakitupiliwa mbali. Wanachama na viongozi hao wamesema hawako tayari kubuluzwa na wameamua kufanya maamuzi magumu kwa maslahi mapana ya Taifa.