Kila siku mimi ninadhani kwa jinsi siasa za bara la africa zilivyo mfumo wake uliridhiwa au
kupokelewa kinafki , ki usaliti , kizandiki na kiubinafsi yaani kwakujipendekeza pendekeza na ndivyo
tume uchukulia ni mfumo hata mashuleni na maishani maranyingi. Mara nyingi hata tukiona ujinga tunafunga mdomo ili tuu ajue tumemuelewa kafanya sawa na atakae fungua mdomo atatengwa kwa
ukweli wake.
Sasa kwa jinsi hiyo kwa maoni yangu mimi siungi mkono kwa wasomi wa hadhi ya juu na wenye
uwelewa wa mambo kuzungumzia siasa za afrika kwasababu mfumo sio salama kwao,
nina ushahidi wa watu fulani kupoteza vyeo au hadhi zao kisa walisimamia ukweli wao au
maslahi ya jamii na hivyo kupingana na wakubwa au wanasiasa. Na pia nina ushahidi wakutosha
kwamba kuna watu walipandishwa vyeo au hadhi kisa tuu aliugeuza ukweli kuwa uwongo na
uku akijua ninaangamiza jamii kubwa kwa maslahii ya mkubwa mmoja au wanasiasa.
Hinyo kitila mkumbo, dr banna na wengineo ni kwa ushauri wangu tuuu kama
huwezi kuuzungumzia ukweli wa moyoni mwako ni bora mkae mbali na vyombo vya habari
au msiseme kitu, kwasababu mara nyingi baada ya kukipata unachokitafuta nafsi
itakutafuna na itakutesa mpaka kaburini kwasababu tuuu uligeuza ukweli kuwa
uwongo kisa tumbo au madaraka.
Na pia mna wakatisha tamaa vijana wenye hari ya kusoma mpaka kuwa kamanyinyi
kwasababu unachokiongea na jinsi ulivyo inakatisha tamaa, na pia sikuhizi hadi
mtu wa darasa la saba anawatukana wasomi kwa sababu ya mawazo yao mabovu
kwa hiyo tutumie akili zetu vizuri jamani.
Asanteni