Masikini Mange Kimambi

Masikini Mange Kimambi

Hance Mtanashati

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2016
Posts
23,877
Reaction score
31,632
Namuhurumia sana Mange Kimambi kwa aibu atakayopata kutoka kwa Watanzania.

Binafsi natamani maandamano ya amani yawepo reforms zifanyike kusudi huko kupiga kura kuwe na maana kuliko maigizo haya ya kila siku ya kwenda kupiga kura wakati mshindi anajulikana tayari.

Kwa nguvu alizotumia Mange Kimambi nasikitika kusema watanzania wata mdisappoint na hatokaa aamini macho yake.

Kwa hali ilivyo huku uraiani hakuna mwenye nia ya kuandamana na ila kuna asilimia ndogo sana ya watu ambao watapiga kura.

Asilimia zaidi ya 70 tumeshakubaliana na hali ,na hiyo siku watu tutaichukulia kama zilivyo siku nyingine, hatupigi kura ila kuhusu kuandamana itategemea pia japo si rahisi kufanyika.

Nikikumbuka maandamano ya UKUTA yalivyotikisa kipindi kile na hakuna Mtanzania hata mmoja aliyejitokeza kuandamana licha ya kujazana upepo wa kuandamana ninadhani hata hii tarehe 29 mambo yatakuwa ni yaleyale.

Watu hatuwazi kabisa kuhusu uchaguzi kila mmoja yupo busy na shughuli yake na hatuna habari kabisa kuhusu huo uchaguzi feki.

Pole sana Mange, watanzania sisi ni kama kenge hatusikii mpaka damu zitutoke masikioni .
 
Kama ni huruma wahurumie watanzania. Mangi sio maskini kama wengi waliopo nchini. Yeye ni mtanzania anayechukuzwa na haya yanayotokea na kuendelea hapa nchini.

Kama wewe unafurahishwa na hali tulionayo hongera lakini kwa vyovyote iwavyo lazima tubadilishe hii hali
 
Utafanyaje sasa?
Wote mimi na wewe tunajukumu la kutoka na kuwainua wengine. Hakuna aliye salama ni vile tuu hujaingia kwenye rada zao.

Kuna sheria na taratibu lakini hazifuatwi. Unashtukia gari haina namba imekukwapua sasa hatuwezi kwenda kwa namba hiyo lazima tuseme hapana kwa sauti moja. Ukinyamaza maana yake umewaunga mkono
 
Mtanzania average ambaye ni part of the majority asiyejua kesho anakula nini. Atajiona na atakuwa ni mpuuzi mkubwa duniani kwa kusikiliza maneno ya kidada kinacholia kitanda size ya chumba chake, kinakula na kulala hoteli zenye bei kuzidi budget yake ya mwaka mzima. Kwamba atoke akaandamane, ahatarishe afya na maisha yake kisa kidada hicho kutoka mtandaoni kimesema hivyo.
 
Mtanzania average ambaye ni part of the majority asiyejua kesho anakula atajiona na atakuwa ni mpuuzi mkubwa duniani kwa kusikiliza maneno ya kidada kinacholia kitanda size ya chumba chake, kinakula na kulala hoteli zenye bei kuzidi budget yake ya mwaka mzima. Kwamba atoke akaandamane, ahatarishe afya na maisha yake kisa kidada hicho kimesema hivyo.
Nakuona muuza Uoga umekuja kutuuzia uoga
 
Wote mimi na wewe tunajukumu la kutoka na kuwainua wengine. Hakuna aliye salama ni vile tuu hujaingia kwenye rada zao.

Kuna sheria na taratibu lakini hazifuatwi. Unashtukia gari haina namba imekukwapua sasa hatuwezi kwenda kwa namba hiyo lazima tuseme hapana kwa sauti moja. Ukinyamaza maana yake umewaunga mkono
Ngoja tuone itakavyokuwa
 
Mtanzania average ambaye ni part of the majority asiyejua kesho anakula nini. Atajiona na atakuwa ni mpuuzi mkubwa duniani kwa kusikiliza maneno ya kidada kinacholia kitanda size ya chumba chake, kinakula na kulala hoteli zenye bei kuzidi budget yake ya mwaka mzima. Kwamba atoke akaandamane, ahatarishe afya na maisha yake kisa kidada hicho kutoka mtandaoni kimesema hivyo.
Wewe ni mpuuzi.
 
Mtanzania average ambaye ni part of the majority asiyejua kesho anakula nini. Atajiona na atakuwa ni mpuuzi mkubwa duniani kwa kusikiliza maneno ya kidada kinacholia kitanda size ya chumba chake, kinakula na kulala hoteli zenye bei kuzidi budget yake ya mwaka mzima. Kwamba atoke akaandamane, ahatarishe afya na maisha yake kisa kidada hicho kutoka mtandaoni kimesema hivyo.
Hakuna ambaye hayupo kwenye hatari ni vile hujaingia kwenye kumi na nane za wahuni. Yule Niffer ameposti kama kichekesho wakamteka.

Unadhani kesho sio kwako? Unaweza kutoa mawazo ambayo kwako unaoma ya kawaida lakini kwao wakahisi ni hatari nakuhakikishia hutaamini.

Lazima kama jamii tuwe na taratibu za kukubaliana na kukosoana huku kutekana hakuna aliyesalama hata kama sasa hivi unanufaika.

Maandamano yetu ni tuwajue wasiojulikana watupe watu wetu wengi waliowapoteza
 
Back
Top Bottom