Masih Alinejad ni Mange Kimambi wa Iran

Masih Alinejad ni Mange Kimambi wa Iran

Ertugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
13,244
Reaction score
26,521
Screenshot_20260103-104305_YouTube.jpg


My people,​

Huyu ni mwandishi wa habari na mwanaharakati wa Iran ambaye naye kama alivyo Kimambi anaishi Marekani

Akihojiwa na NBC News anasema familia nyingi za viongozi wakubwa wa Iran wanaishi Marekani,anahoji kama wanawatendea ubaya wananchi wa nchi hiyo basi na familia zao nao zirudi Iran ili wote wateseke

Anasema serikali ya kiislamu ya Iran ni kama Kansa ambayo inaitafuna dunia nzima,anaendelea kusema kwamba wananchi wa Iran sio kwamba tu wanajikomboa wenyewe bali wanaikomboa dunia nzima

Anafurahishwa sana na kauli ya Trump kwamba kama Iran itawaua wananchi wake basi Marekani haitasita kuchukua maamuzi magumu na kuichukulia hatua kali nchi hiyo

Kwa upande wa pili mwandishi wa makala haya Ertugrul bey naye anayakusema:

Pamoja na kwamba siungi mkono harakati nyingi zinavyofanywa na Serikali ya Iran,lakini je Marekani ina mapenzi makubwa na raia wa Iran?

Jibu hapana bali ni kile ambacho wamekuwa wakikipigania miaka yote kwamba Iran inatishia usalama wa mashariki ya Kati

Tena naona sasa ndio wamepata sababu ya uungwaji mkubwa wa wananchi wa Iran,watajifanya wanajali sana hali za wananchi wa Iran lakini behind the curtain wana ajenda yao

Swali ninalo jiuliza je,haya yakitokea hayawezi kuwa kama yaliyotokea Libya?

Hofu yangu huenda yakatokea machafuko makubwa sana na nchi inaweza isitawalike,ukichukulia kwamba bado kutakuwa na watu wenye kutaka IRAN iendelee kuwa na mlengo wa kidini na kuna ambao watataka kuwa nje ya mfumo wa dini au sheria za dini ya kiislamu na kuwa free zaidi

Kiukweli kabisa naona mbeleni huko Iran ambayo itakuwa haina utulivu na iliyojawa na vurugu tele,hapo ndipo wananchi wa Iran watatamani walau wangebakia na Iran yao waliyo izoea pamoja na mbanga zake

Mungu ibariki Mashariki ya Kati na Mungu ibariki Iran

Ni hayo tu!
 
Hapa siyo Iran ukileta ujinga wa kihalifu wizi na uharibifu wa mali za watu Mama yako atakuja kulia akitambaa mbele ya camera kuomba mwili wako akauzike au kukuombea msamaha usiende jela.

Hakuna huruma kwa wahalifu.
 
hapo ndipo wananchi wa Iran watatamani walau wangebakia na Iran yao waliyo izoea pamoja na mbanga zake

Unakosea kusema nchi WALIYOIZOEA

Unapokuwa huna jinsi haimaanishi UMEZOEA

Hata hapa TZ mfumo kandamizi uliopo toka Nyerere huwezi kusema TUMEZOEA

Matatizo unayazoe vipi ?? Njaa zako na umaskini uliozaliwa nao kwa nn miaka 30 baadae bado unau fight umaskini unatafuta utajiri ? Baki na shida zako ULIZOZIZOEA!!!

Na ndo maana watu hufika mahala wanachafukwa!

Ingekuwa watu WANAZOEA kukandamizwa kwa nn huwa wanakiwasha ????

Tunapinga na kulaani kuambiwa TUZOEE UKANDAMIZAJI
 
View attachment 3524510

My people,​

Huyu ni mwandishi wa habari na mwanaharakati wa Iran ambaye naye kama alivyo Kimambi anaishi Marekani

Akihojiwa na NBC News anasema familia nyingi za viongozi wakubwa wa Iran wanaishi Marekani,anahoji kama wanawatendea ubaya wananchi wa nchi hiyo basi na familia zao nao zirudi Iran ili wote wateseke

Anasema serikali ya kiislamu ya Iran ni kama Kansa ambayo inaitafuna dunia nzima,anaendelea kusema kwamba wananchi wa Iran sio kwamba tu wanajikomboa wenyewe bali wanaikomboa dunia nzima

Anafurahishwa sana na kauli ya Trump kwamba kama Iran itawaua wananchi wake basi Marekani haitasita kuchukua maamuzi magumu na kuichukulia hatua kali nchi hiyo

Kwa upande wa pili mwandishi wa makala haya Ertugrul bey naye anayakusema:

Pamoja na kwamba siungi mkono harakati nyingi zinavyofanywa na Serikali ya Iran,lakini je Marekani ina mapenzi makubwa na raia wa Iran?

Jibu hapana bali ni kile ambacho wamekuwa wakikipigania miaka yote kwamba Iran inatishia usalama wa mashariki ya Kati

Tena naona sasa ndio wamepata sababu ya uungwaji mkubwa wa wananchi wa Iran,watajifanya wanajali sana hali za wananchi wa Iran lakini behind the curtain wana ajenda yao

Swali ninalo jiuliza je,haya yakitokea hayawezi kuwa kama yaliyotokea Libya?

Hofu yangu huenda yakatokea machafuko makubwa sana na nchi inaweza isitawalike,ukichukulia kwamba bado kutakuwa na watu wenye kutaka IRAN iendelee kuwa na mlengo wa kidini na kuna ambao watataka kuwa nje ya mfumo wa dini au sheria za dini ya kiislamu na kuwa free zaidi

Kiukweli kabisa naona mbeleni huko Iran ambayo itakuwa haina utulivu na iliyojawa na vurugu tele,hapo ndipo wananchi wa Iran watatamani walau wangebakia na Iran yao waliyo izoea pamoja na mbanga zake

Mungu ibariki Mashariki ya Kati na Mungu ibariki Iran

Ni hayo tu!
Huu ndio mwisho ayatolah
 
Unakosea kusema nchi WALIYOIZOEA

Unapokuwa huna jinsi haimaanishi UMEZOEA

Hata hapa TZ mfumo kandamizi uliopo toka Nyerere huwezi kusema TUMEZOEA

Matatizo unayazoe vipi ?? Njaa zako na umaskini uliozaliwa nao kwa nn miaka 30 baadae bado unau fight umaskini unatafuta utajiri ? Baki na shida zako ULIZOZIZOEA!!!

Na ndo maana watu hufika mahala wanachafukwa!

Ingekuwa watu WANAZOEA.kukandamizwa kwa nn huwa wanakiwasha ????

Tunapinga na kulaani kuambiwa TUZOEE UKANDAMIZAJI
Upo sahihi lakini yakitokea mambo ambayo ni mabaya zaidi kuliko yale ambayo mmekuwa nayo zamani,lazima ujutie hilo
 
Back
Top Bottom