KWELI Mashine za Kunyolea nywele zinaweza kusambaza VVU

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Kisayansi na kibaiolojia virusi wanasifa ya kutokuwa hai pale wanapokuwa nje ya seli ya kiumbe mwingine(host) na wanaweza kukaa muda mrefu bila kuwa na dalili zote za viumbe hai mpaka pale watapoingia kwenye seli ya kiumbe.

Inakuwaje sasa tunaambiwa HIV haambukizwi kwa mashine za kunyolea saloon kwa kigezo cha kwamba hawawezi kuishi katika mashine na ilihali wao ni vijidudu visivyo hai wanapokua nje ya host?

804A5D72-8B77-4730-A582-E3B90D52FE9A.jpeg
 
Tunachokijua
HIV ama Human Immunodeficiency Virus ni kirusi kinachoshambulia mfumo wa kinga mwili, ambacho baada kuishi mwilini kwa kipindi fulani kinaweza kusababisha upungufu wa kinga mwilini (UKIMWI).

Virusi hawa wanaweza kumwingia mtu kupitia ushiriki wa tendo la ndoa ambapo majimaji ya uke, uume au shahawa ndiyo hubeba virusi hawa, kushirikiana vitu vyenye ncha kali, kubadilishana damu na mazao yake au maambukizi ya mama na mtoto wakati wa ujauzito, kujifungua na kunyonyesha.

Virusi hawa wenye sifa ya RNA, hubeba aina 15 za protini pia huzungukwa na kuta mbili za mafuta. Hushambulia seli hai zenye vipokeo vya CD4 pekee, hubadilika mara kwa mara pamoja na kupoteza sifa ya kuishi kikiwa kwenye mazingira yasiyo rafiki.

Ili virusi viweze kuingia mwilini na kusababisha madhara huhitaji mambo matatu ya msingi-
  1. Damu au Majimaji ya mwili
  2. Kitendo hatarishi
  3. Upatikanaji wa moja kwa moja wa mishipa ya damu
Kunyoa salon ni kitendo hatarishi, lakini hukosa sifa mbili za ziada za kutoa mazingira yenye majimaji ya mwili pamoja na upatikanaji wa moja kwa moja wa mishipa ya damu ili virusi waingie.

Hii ndiyo sababu inayofanya watu wengi wasiambukizwe VVU kupitia salon na siyo kutokuishi kwa virusi kwenye mashine kama hoja ya mdau ilivyo.

Hata hivyo, JamiiForums inatambua kuwa hali hii haitoi maana kuwa salon haziwezi kabisa kuambukiza VVU hasa katika hali ambazo mazingira yote matatu yatakuwepo.

Ni muhimu kwa wamiliki wa salon kutakasa mashine zao kila mara pamoja na kuchukua tahadhari zote za kulinda wateja ikiwemo kutowakwangua sana ili kuepusha uwezekano wa kuichubua mishipa ya damu, kitendo kinachoweza kutoa nafasi ya kuingia kwa virusi mwilini.
Uwezekano utakuwepo kama chombo kitakuwa contaminated na maji maji au damu kutoka kwa mtu mwenye VVU na kutumika kwa mtu asiye na maambukizi ya VVU lakini na yeye awe na vidonda au open cut wounds au mikwaruzo.

Risk ya maambukizi itapungua kama chombo kikipata sterilization ipasavyo.

Risk ya maambukizi itapungua ikiwa kuna muda wa kutosha kutoka chombo kinachotumika kwa mtu mmoja hadi mwingine, umuhimu wa kuwa na mashine zaidi ya moja, yaani mashine ilkishatumika isafishwe vizuri ifanyiwe sterilization.
 
Kwa kuongezea, kuna watu wanakuja kunyoa wanamapele kichwabi ama ya ndevu na wanataka wakwanguliwe, sometimes hadi damu na mikato hutokea. Sasa ukija na wewe unanyoa na kuchongwa, utakuta unachongwa hadi unataka kusimama na kiti vile jamaa anakata,azingira hayo kweli kuna usalama hapo?
 
Kwa kuongezea, kuna watu wanakuja kunyoa wanamapele kichwabi ama ya ndevu na wanataka wakwanguliwe, sometimes hadi damu na mikato hutokea. Sasa ukija na wewe unanyoa na kuchongwa, utakuta unachongwa hadi unataka kusimama na kiti vile jamaa anakata,azingira hayo kweli kuna usalama hapo?
Watu wa saloon uwq ni wajinga sana ata mi washanikata sana wanavyonyoa😀😀wanatakiwa wapitie mafunzo
 
MADAI
Kisayansi na kibaiolojia virusi wanasifa ya kutokuwa hai pale wanapokuwa nje ya seli ya kiumbe mwingine(host) na wanaweza kukaa muda mrefu bila kuwa na dalili zote za viumbe hai mpaka pale watapoingia kwenye seli ya kiumbe.

Inakuwaje sasa tunaambiwa HIV haambukizwi kwa mashine za kunyolea saloon kwa kigezo cha kwamba hawawezi kuishi katika mashine na ilihali wao ni vijidudu visivyo hai wanapokua nje ya host?

View attachment 2391953
Somo zuri Sana.
 
We upate popote ila watu watajua ulinanilii. Unadhani kuna mtu siku hizi ataamini hadithi ya mashine ya kunyolea sijui wembe?
 
MADAI
Kisayansi na kibaiolojia virusi wanasifa ya kutokuwa hai pale wanapokuwa nje ya seli ya kiumbe mwingine(host) na wanaweza kukaa muda mrefu bila kuwa na dalili zote za viumbe hai mpaka pale watapoingia kwenye seli ya kiumbe.

Inakuwaje sasa tunaambiwa HIV haambukizwi kwa mashine za kunyolea saloon kwa kigezo cha kwamba hawawezi kuishi katika mashine na ilihali wao ni vijidudu visivyo hai wanapokua nje ya host?

View attachment 2391953
Mashine ya kunyolea kama itamkata mtu mwenye HIV na ikatumika tena kwako bila kusafishwa vzr maambukizi yapo pale pale kwakwel
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom