Jannatul Firdaus
JF-Expert Member
- Aug 4, 2026
- 341
- 748
Kukaa bila kufanya chochote kwa dakika 90 kunaweza kuonekana kuwa jambo rahisi. Lakini kwa baadhi ya watu, hilo limegeuka kuwa changamoto inayohitaji nidhamu kubwa.
Nchini Korea Kusini, mashindano ya Space-out yamekuwa yakifanyika kila mwaka, ambapo washiriki hutakiwa kutofanya chochote kwa dakika 90; Hawatakiwa kulala, kutumia simu au kuzungumza.
Lengo la mashindano ni kuangalia nani hajishughulishi au nani anayeweza kutulia zaidi.
Washiriki hufuatiliwa pia mapigo yao ya moyo, huku watazamaji wakipiga kura kuwachagua washiriki 10 wanaowapenda zaidi. Mshindi huchaguliwa miongoni mwao kwa kuangalia nani aliyekuwa na mapigo ya moyo yaliyotulia zaidi.
Mashindano hayo yalianzishwa Seoul mwaka 2014 na msanii wa maonyesho anayejulikana kwa jina la Woopsyang, baada ya yeye mwenyewe kukumbwa na uchovu mkubwa wa akili na mwili.
Kwa mujibu wa Woopsyang, alijiuliza kwa nini alihisi wasiwasi kila alipokuwa ametulia na hafanyi chochote. Baadaye aligundua kuwa wasiwasi huo ulihusishwa na kujilinganisha na watu wengine waliokuwa na shughuli nyingi.
Ndipo akapata wazo la kugeuza hali hiyo ya kutofanya chochote ambao wengine wanaita 'uzembe' kuwa mashindano.
Zaidi ya watu 4,000 waliomba kushiriki katika mashindano ya mwaka 2024 mjini Seoul, huku washiriki 117 wakichaguliwa. Walitoka katika makundi mbalimbali ya umri, kuanzia mtoto wa darasa la pili hadi watu wenye umri wa zaidi ya miaka 60.
Nchini Korea Kusini, mashindano ya Space-out yamekuwa yakifanyika kila mwaka, ambapo washiriki hutakiwa kutofanya chochote kwa dakika 90; Hawatakiwa kulala, kutumia simu au kuzungumza.
Lengo la mashindano ni kuangalia nani hajishughulishi au nani anayeweza kutulia zaidi.
Washiriki hufuatiliwa pia mapigo yao ya moyo, huku watazamaji wakipiga kura kuwachagua washiriki 10 wanaowapenda zaidi. Mshindi huchaguliwa miongoni mwao kwa kuangalia nani aliyekuwa na mapigo ya moyo yaliyotulia zaidi.
Mashindano hayo yalianzishwa Seoul mwaka 2014 na msanii wa maonyesho anayejulikana kwa jina la Woopsyang, baada ya yeye mwenyewe kukumbwa na uchovu mkubwa wa akili na mwili.
Kwa mujibu wa Woopsyang, alijiuliza kwa nini alihisi wasiwasi kila alipokuwa ametulia na hafanyi chochote. Baadaye aligundua kuwa wasiwasi huo ulihusishwa na kujilinganisha na watu wengine waliokuwa na shughuli nyingi.
Ndipo akapata wazo la kugeuza hali hiyo ya kutofanya chochote ambao wengine wanaita 'uzembe' kuwa mashindano.
Zaidi ya watu 4,000 waliomba kushiriki katika mashindano ya mwaka 2024 mjini Seoul, huku washiriki 117 wakichaguliwa. Walitoka katika makundi mbalimbali ya umri, kuanzia mtoto wa darasa la pili hadi watu wenye umri wa zaidi ya miaka 60.