Linyakalumbi
JF-Expert Member
- Jul 28, 2011
- 263
- 107
Laiti mngejua mnachojadili ni mfumo,walahi msingepoteza muda.Lakini kuwaelewesha magamba sio mbaya sana maana nchi ni yetu sote,tukiwaacha wapotee zaidi tutapata tabu huko tuendako.Jibu sahihi la Hesabu huwa na formula moja tu,kama ni simultaneous method basi iwe hivyo na kama ni Integration iwe hivyo,au differentiation sawa,Quadratic equation Okay.Ukijichanganya tu umekwisha.Formula tuliyo nayo ni hiyo ya Magamba tufanyeje?Wao na Serikali yao Wanatoa mil.90/= Mkopo(ambao ni haki miliki ya Mkopaji) hata akinunua Bajaji au Vitz lakini kachukua 90/=.Tatizo tunalopaswa kulitambua ni Thamani ya Mali iliyoidhinishwa ambayo Ndio Dr.Slaa alitaka kuja kuifanyia kazi!Na ndio ataifanyia kazi 2015. Kwani Mnyika hiyo Vitz muulizeni alikopa m.90/= au hakukopa? Na kama alikopa je,Vitz inauzwa m.90/=?Utasikia alizitumia kwenye maendeleo ya Walipa Kodi,sawa na vema,Ndio wajibu wake?Ni nini kazi ya Serikali ya JK? Kwa hiyo nayetwishwa lawama hapa ni Serikali anaye wakopesha hawa mihela yote hii.Mfano:Wanafunzi wa Elimu ya Juu kwenye Mkopo wao kuna Pesa ya Stationary 250,000/=,ulishawahi fanya utafiti ukaona wanachoifanyia hii pesa?Je,Bodi inawalazimisha au inawakagua Stationary walizonunua?Ni mkopo,mkopaji anauhuru wa Kutumia apendavyo,mwingine Kiti Moto,mwingine "Lulu's" n.k.Lakini hii hii Body Inatoa Accomodation Fee kama 300,000/=,wengine wanaishi majumbani mwao kwa wazazi wao,wengine wanapanga uswazi na kulipia 150000/=Tu.So kuweni na akili.tatizo sio Chadema na halitakuwa tatizo lao,Hata Mh.Mbowe lile Koko ni haki yake kabisa,anayetakiwa kuona ni gharama na hasara ili azuie ni Serikali!!Ngoja nifute machozi kwanza kuwalilia kina Rejao,Ritz,Katiba Mpya,Ngongo kwa kukosa Elimu Dunia na kujifanya vipofu japo wanaona ukweli.Mimi binafsi ningedhani hata Posho wangegonga tu maana Formula yenyewe imeshindwa kusolve hesabu,Tutapobadili Formula 2015 Ndio Jibu Litapatikana.Unajua hata Dr.Slaa alipokuwa anatangaza kwamba Mashangingi kwa Serikali ni anasa na mzigo kwa Walipa kodi alimaanisha Magari ya Serikali kama vile ya wabunge,mawaziri & Naibu wao,Wakuu wa Mikoa,wilaya na Wakurugenzi n.k. LAKINI hakumaanisha kwamba Lowassa usinunue Shangingi,Rejao Usinunue Shangingi,Kipeke Usinunue Shangingi.Why?Wakati ni Pesa yako na Unayo!Iwe kwa mkopo wa Ubunge au whatever is excellent.TATIZO ni Kwanini Hiyo Dolla yaani Serikali Isiwakopeshe wabunge Pesa za Kutosha Bajaji?Kwa sababu mimi namwambia Mke wangu sina pesa usinunue Nyama,lakini Nilishamwambia matumizi ya pesa ninayokupa unauhuru wa kununua upendacho tule hapa ndani sio.Sasa nimempa 10,000/=,unataka anunue bamia na mkunungu?mpe 2000/= uone kama atanunua hizo pochozi!!!