Nilifuatilia kwa makini mjadala wa katiba ulioendeshwa mlimani siku ya jumamosi, mjadala ulikuwa mzuri lakini kati ya mambo ya kukumbukwa na kutosahaulika ni mzee mapesa kushushwa jukwaani na wasikilizaji ambao hawakuridhishwa na maneno na mwelekeo wa mzee Cheyo. inawezekana kuna sababu nyingi zilizowafanya wananchi kumpigia makofi ya kuondoka hata baada ya Dr Kitila Mkumbo kuwasihi wamsikilize amalizie anglau neno la mwisho, lakini moja ya mawazo niliyonayo mimi ni kwamba alianza kuimba mashairi yaliyozoeleka na yanayotumika kukandamiza haki za watu.
Mashairi haya moja ya hilo ni huu ubeti wa amani na utulivu, ubeti huu umekuwa ukitumika kuwanyamazisha watu wasidai haki zao katika nyanja mbalimbali. wakati wachangiaji wengi walikuwa wakikosoa muswada na kupendekeza marekebisho, yeye alijikita kwenye utetezi na msisitizo kwenye "amani na utulivu"
Nafikiri hii ni wake up call kwa wanasiasa wengine watafute namna ya ku - rephrase hii slogan la sivyo wananchi washatambua kwamba mashairi haya ya amani na utulivu bila haki ni upuuzi mtupu.
Naomba kuwasilisha wana JF
Mashairi haya moja ya hilo ni huu ubeti wa amani na utulivu, ubeti huu umekuwa ukitumika kuwanyamazisha watu wasidai haki zao katika nyanja mbalimbali. wakati wachangiaji wengi walikuwa wakikosoa muswada na kupendekeza marekebisho, yeye alijikita kwenye utetezi na msisitizo kwenye "amani na utulivu"
Nafikiri hii ni wake up call kwa wanasiasa wengine watafute namna ya ku - rephrase hii slogan la sivyo wananchi washatambua kwamba mashairi haya ya amani na utulivu bila haki ni upuuzi mtupu.
Naomba kuwasilisha wana JF