Mashairi ya CCM yamemponza Cheyo?

emalau

JF-Expert Member
Apr 25, 2009
2,775
3,100
Nilifuatilia kwa makini mjadala wa katiba ulioendeshwa mlimani siku ya jumamosi, mjadala ulikuwa mzuri lakini kati ya mambo ya kukumbukwa na kutosahaulika ni mzee mapesa kushushwa jukwaani na wasikilizaji ambao hawakuridhishwa na maneno na mwelekeo wa mzee Cheyo. inawezekana kuna sababu nyingi zilizowafanya wananchi kumpigia makofi ya kuondoka hata baada ya Dr Kitila Mkumbo kuwasihi wamsikilize amalizie anglau neno la mwisho, lakini moja ya mawazo niliyonayo mimi ni kwamba alianza kuimba mashairi yaliyozoeleka na yanayotumika kukandamiza haki za watu.

Mashairi haya moja ya hilo ni huu ubeti wa amani na utulivu, ubeti huu umekuwa ukitumika kuwanyamazisha watu wasidai haki zao katika nyanja mbalimbali. wakati wachangiaji wengi walikuwa wakikosoa muswada na kupendekeza marekebisho, yeye alijikita kwenye utetezi na msisitizo kwenye "amani na utulivu"

Nafikiri hii ni wake up call kwa wanasiasa wengine watafute namna ya ku - rephrase hii slogan la sivyo wananchi washatambua kwamba mashairi haya ya amani na utulivu bila haki ni upuuzi mtupu.

Naomba kuwasilisha wana JF
 
Yes nakumbuka hata Prince Bagenda alichemsha na wasomi walikuwa wanawashusha kistaarabu kwa kukupigia makofi bila kuchoka
 
Mbona ni dhahiri, na labda unasahau kwamba Mzee Mapesa yeye ndiye aliyebaki ktk chama chake lazima atafute mahali pa kuegamia. Mkague na Profesa pia, ana kipi sasa? Prince alikuwa mpinzani, ni nini walichobadilisha CCM mpaka ikufanye ururdi kule? Kama ulikimbia watu wakiiba 50/- sasa wanaiba 500/- unawakubali vp? Hawa wamebaki kuwa waganga njaa.
Asante kwa hoja yako.
 
huyo cheyo mbinafsi sana nakumbuka wakati ule wa kujiongezea mishahara wabunge alikuwa anatetea sana karibia kutoa chozi,..sielewi wanaomchagua ubunge wawazaga nini,..lakini huyo si mmoja wa wale ccm B
 
Alikuwa analipa fadhila za kuchaguliwa u-enyekiti wa kamati ya bunge.....Huyu mzee keshachanyikiwa...Binafsi nilifurahishwa sana na Mtatiro alivyopresent mada.
 
Alikuwa analipa fadhila za kuchaguliwa u-enyekiti wa kamati ya bunge.....Huyu mzee keshachanyikiwa...Binafsi nilifurahishwa sana na Mtatiro alivyopresent mada.[/QUOTE]

Alisoma moods... watu walikuwa wanataka kitu halisi sio propaganda, asingekuwa makini angetolewa nje kama CCM na Cheyo. Namshauri afanye mpango wa kuwaeleza viongozi wenzake ndani ya CUF kwamba watu wameamka, wao kama chama cha upinzani wanatakiwa kudeal na chama tawala katika kukikosoa na mengineyo sio kukiandama CHADEMA.
 
Alikuwa analipa fadhila za kuchaguliwa u-enyekiti wa kamati ya bunge.....Huyu mzee keshachanyikiwa...Binafsi nilifurahishwa sana na Mtatiro alivyopresent mada.[/QUOTE]

Alisoma moods... watu walikuwa wanataka kitu halisi sio propaganda, asingekuwa makini angetolewa nje kama CCM na Cheyo. Namshauri afanye mpango wa kuwaeleza viongozi wenzake ndani ya CUF kwamba watu wameamka, wao kama chama cha upinzani wanatakiwa kudeal na chama tawala katika kukikosoa na mengineyo sio kukiandama CHADEMA.


Mzee wa Kiraracha alipokuwa anawalalamikia CDM kwamba wanavua samaki walio kwenye kapu badala ya wale waliopo ziwani mlimuona hamnazo. Sasa nyie mnawalalamikia CUF kwa lipi? Najua mtakasirika laini potelea mbali



 
Mbunge wa zamani wa Vunjo Bwana Kimario aliwambia UVCCM kwamba kama wanafikiri bado wapo relevant wajaribu kwenda kuhutubia UDSM waone kama hawatazomewa. Nadhani zomea zomea ya Price Bagenda na Cheyo ni fundisho tosha. Hata hivyo CCM walikosea sana kumtuma Bagenda maana ni mamluki kama alivyo Tambwe Hizza. Huwezi kueshimiwa kama ukiwa mamaluki.
 
Serikali ya JK iwe makini na maamuzi yake, kama haina nia ya Katiba mpya ni bora iseme mapema kuliko kuwatia hamasa wananchi na mwishowe wakaamua kudai katiba ya kweli! Na yeyote atakayesimama kutetea usanii katika suala la katiba mpya atakumbana na wananchi ambao ndiyo wenye nchi!
 
[/COLOR]

Mzee wa Kiraracha alipokuwa anawalalamikia CDM kwamba wanavua samaki walio kwenye kapu badala ya wale waliopo ziwani mlimuona hamnazo. Sasa nyie mnawalalamikia CUF kwa lipi? Najua mtakasirika laini potelea mbali



Potelea mbali mbali ya nini sasa? Kwani uko hapa kumfurahisha nani?
 
Nilifuatilia kwa makini mjadala wa katiba ulioendeshwa mlimani siku ya jumamosi, mjadala ulikuwa mzuri lakini kati ya mambo ya kukumbukwa na kutosahaulika ni mzee mapesa kushushwa jukwaani na wasikilizaji ambao hawakuridhishwa na maneno na mwelekeo wa mzee Cheyo. inawezekana kuna sababu nyingi zilizowafanya wananchi kumpigia makofi ya kuondoka hata baada ya Dr Kitila Mkumbo kuwasihi wamsikilize amalizie anglau neno la mwisho, lakini moja ya mawazo niliyonayo mimi ni kwamba alianza kuimba mashairi yaliyozoeleka na yanayotumika kukandamiza haki za watu.

Mashairi haya moja ya hilo ni huu ubeti wa amani na utulivu, ubeti huu umekuwa ukitumika kuwanyamazisha watu wasidai haki zao katika nyanja mbalimbali. wakati wachangiaji wengi walikuwa wakikosoa muswada na kupendekeza marekebisho, yeye alijikita kwenye utetezi na msisitizo kwenye "amani na utulivu"

Nafikiri hii ni wake up call kwa wanasiasa wengine watafute namna ya ku - rephrase hii slogan la sivyo wananchi washatambua kwamba mashairi haya ya amani na utulivu bila haki ni upuuzi mtupu.

Naomba kuwasilisha wana JF


Yale yale ya ccm.. eti amani! amani my foot tuna amani gani na maisha haya? unajua watu kama cheyo ni wa kuogopa sana kwani wanafaidika na mfumo uliopo ndio maaana wanakesha wakinywa bia pale Q bar! hawaoni hata wananchi wanateseka kiasi gani huku mitaani, wananunua mkate mary brown wakati pale tandale watu wnanunua mkate kwa mangi tena kwa kuhesabiwa slices!!!
 
Nilifuatilia kwa makini mjadala wa katiba ulioendeshwa mlimani siku ya jumamosi, mjadala ulikuwa mzuri lakini kati ya mambo ya kukumbukwa na kutosahaulika ni mzee mapesa kushushwa jukwaani na wasikilizaji ambao hawakuridhishwa na maneno na mwelekeo wa mzee Cheyo. inawezekana kuna sababu nyingi zilizowafanya wananchi kumpigia makofi ya kuondoka hata baada ya Dr Kitila Mkumbo kuwasihi wamsikilize amalizie anglau neno la mwisho, lakini moja ya mawazo niliyonayo mimi ni kwamba alianza kuimba mashairi yaliyozoeleka na yanayotumika kukandamiza haki za watu.

Mashairi haya moja ya hilo ni huu ubeti wa amani na utulivu, ubeti huu umekuwa ukitumika kuwanyamazisha watu wasidai haki zao katika nyanja mbalimbali. wakati wachangiaji wengi walikuwa wakikosoa muswada na kupendekeza marekebisho, yeye alijikita kwenye utetezi na msisitizo kwenye "amani na utulivu"

Nafikiri hii ni wake up call kwa wanasiasa wengine watafute namna ya ku - rephrase hii slogan la sivyo wananchi washatambua kwamba mashairi haya ya amani na utulivu bila haki ni upuuzi mtupu.

Naomba kuwasilisha wana JF
cHEYO NI MZANDIKI, MNAFIKI NA MTU ASIYEJUA AFANYACHO... :bored: Yeye hufuata upepo unaompeleka kwenye ulaji, basi!!!
 
Nilifuatilia kwa makini mjadala wa katiba ulioendeshwa mlimani siku ya jumamosi, mjadala ulikuwa mzuri lakini kati ya mambo ya kukumbukwa na kutosahaulika ni mzee mapesa kushushwa jukwaani na wasikilizaji ambao hawakuridhishwa na maneno na mwelekeo wa mzee Cheyo. inawezekana kuna sababu nyingi zilizowafanya wananchi kumpigia makofi ya kuondoka hata baada ya Dr Kitila Mkumbo kuwasihi wamsikilize amalizie anglau neno la mwisho, lakini moja ya mawazo niliyonayo mimi ni kwamba alianza kuimba mashairi yaliyozoeleka na yanayotumika kukandamiza haki za watu.

Mashairi haya moja ya hilo ni huu ubeti wa amani na utulivu, ubeti huu umekuwa ukitumika kuwanyamazisha watu wasidai haki zao katika nyanja mbalimbali. wakati wachangiaji wengi walikuwa wakikosoa muswada na kupendekeza marekebisho, yeye alijikita kwenye utetezi na msisitizo kwenye "amani na utulivu"

Nafikiri hii ni wake up call kwa wanasiasa wengine watafute namna ya ku - rephrase hii slogan la sivyo wananchi washatambua kwamba mashairi haya ya amani na utulivu bila haki ni upuuzi mtupu.

Naomba kuwasilisha wana JF

Ninachongoja ni kuona jinsi watakavyoimba mashairi hayo huko bungeni kuanzia kesho na hasa muswada utakapowasilishwa rasmi. Je, wataendeleza uzandiki wao wa kuiandama CDM au watasimama kwenye hoja yenye maslahi kwa Tanzania ya kesho?
 
Wanasiasa wa aina ya cheyo ni hatari sana. Huyu mzee alikuwa maarufu enzi za 1995 wote tunajua hili. Sasa hivi hana lolote, nadhani hata biashara zake zote zimesha -collapse, hana pa kushika kabaki mpambe wa ccm. hana jipya huyo. Yeye ndo mwenyekiti wa UDP na ndo mbunge pekee wa chama chake. Sijui wananchi wa Bariadi walitumia kigezo gani kumrudisaha bungeni tena awamu hii. Nadhani kosa hili watalijutia sana.

Namshauri mzee Cheyo kama hakubaliani na nguvu ya umma, ni afadhali kunyamaza kuliko kuchangia kwa kuegemea kwenye serikali iliyoko madarakani, ni aibu, lazima akubali waTZ wamebadirika sana, wameshajua haki zao zote.

Ni afadhali kusinzia bungeni kama anavyofanya John Komba kuliko kuchangia utumbo.
 
Serikali ya kikwete kama ina dhamira ya dhati ya kupatikana kwa katiba mpya ni sharti izingatie mawazo ya watz na sio mawazo ya serikali yao ambayo haina mvuto kwa watz,serikali yake ielewe watz wa leo wanaelewa kinachoendelea ndani ya serikali yake.angalizo "endapo watafikiri ccm ndo yenye nchi hii na kusahau watz basi wategemee kuondoka kwa gharama yoyote kwani watz tumechoshwa na staili hii ya uongozi usioangalia maslahi ya watz".
 
Tuache ushabiki wa ccm kwa kwa masuala yanayolihusu taifa hili kwani TANZANIA itakuwepo hata bila ccm, hivyo zama za kutishana zimepitwa na wakati kwa wale wote walioshiriki kuaandaa mswada wenye mapungufu ya wazi ya kutaka kubeba ccm na serikali yake.
 
Back
Top Bottom