Mashahidi Wakwamisha Kesi Ya Vigogo Wa CHADEMA

babalao 2

JF-Expert Member
Apr 6, 2012
5,400
3,245
KESI inayowakabili vigogo wawili wa CHADEMA kwa tuhuma ya kumtolea lugha ya matusi Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi, Mwigullu Nchemba imeshindwa kuendelea kusikilizwa baada ya mashahidi wa upande wa mashitaka kushindwa kufika mahakamani.

Hiyo ni mara ya pili mfululizo mashahidi yao kushindwa kufika mahakamani.

Mara ya kwanza mashahidi hao wa upande wa mashitaka kushindwa kufika mahakamani, hakimu anayeisikiliza kesi hiyo, Flora Ndale aliagiza kuwa juhudi zifanyike kuhakikisha kuwa mashahidi hao wanafika mahakamani bila kukosa waweze kutoa ushahidi wao.

Ndale alisema kitendo cha mashahidi wa upande wa mashitaka kutokufika mahakamani wakati washitakiwa kutoka Dar es Salaam wanafika, ni usumbufu mkubwa kwa washitakiwa, mawakili wao na wasikilizaji.

Kesi hiyo sasa itaendelea kuunguruma Aprili 8 mwaka huu.

Vigogo hao ambao wanatuhumiwa kumtolea lugha ya matusi Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi, Mwigulu Chemba ni Waitara Mwikwabe (37) ofisa sera na utafiti makao makuu na Dk.Kitila Mkumbo mhadhiri wa Chuo.

Source: Mtanzania
 
Kwa tunavyomjua Dr Kitila Mkumbo ni kweli anaweza kumtukana Mwigulu Nchemba?

Au hawa mashahidi ni akina Shonza
 
hapa ilikuwa ni mashahidi wa 'kutengeneza' tu. au basi wanaweza kuwa wameogopa kuja kubanwa kama yule shahidi wa kwenye kesi ya Tundu Lissu aliyesema wazi kawa alipewa pesa na kuelekeza cha kuongea.
Wanafikiri wanampotezea Dr. Mkumbo muda kumbe hawajui wanapoteza muda wa ujenzi wa taifa kwa ujmla, Mungu atawaumbiua tu!
 
Mtu anaefanya siasa za matusi ni yule aliefilisika ki fikra, Dr.Kitila ni mtu anayejenga hoja nzuri na zenye nguvu, hivyo Kitila hawezi kufanya siasa za matusi.
 
CCM inakimbiwa mpaka na mashahidi lol!tatizo kesi zao ni za kuunga unga wanapoteza muda wa mahakama na watu na huku wanajua hakuna ccm inachotumikia wananchi
 
KESI inayowakabili vigogo wawili wa CHADEMA kwa tuhuma ya kumtolea lugha ya matusi Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi, Mwigullu Nchemba imeshindwa kuendelea kusikilizwa baada ya mashahidi wa upande wa mashitaka kushindwa kufika mahakamani.

Hiyo ni mara ya pili mfululizo mashahidi yao kushindwa kufika mahakamani.

Mara ya kwanza mashahidi hao wa upande wa mashitaka kushindwa kufika mahakamani, hakimu anayeisikiliza kesi hiyo, Flora Ndale aliagiza kuwa juhudi zifanyike kuhakikisha kuwa mashahidi hao wanafika mahakamani bila kukosa waweze kutoa ushahidi wao.

Ndale alisema kitendo cha mashahidi wa upande wa mashitaka kutokufika mahakamani wakati washitakiwa kutoka Dar es Salaam wanafika, ni usumbufu mkubwa kwa washitakiwa, mawakili wao na wasikilizaji.

Kesi hiyo sasa itaendelea kuunguruma Aprili 8 mwaka huu.

Vigogo hao ambao wanatuhumiwa kumtolea lugha ya matusi Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi, Mwigulu Chemba ni Waitara Mwikwabe (37) ofisa sera na utafiti makao makuu na Dk.Kitila Mkumbo mhadhiri wa Chuo.

Source: Mtanzania
Kesi ya kitoto kabisa eti nimetukanwa, nimefinywa, kanikanyaga na pengine matusi yenyewe yanayodaiwa ni kupewa tu sifa kama vile HUNA AKILI,nk.

Mwisho wa yote ni AIBU ngoja tuone
 
Kesi zingine huwa zipo zipo tu. Next time si ajabu ikafutwa!
 
Hii ndiyo ile kesi ya Mwigulu kupeleka vijana singida kwenda kuleta fujo kwenye mkutano wa CDM?
 
Mwigulu baada ya ile ishu ya Ndago kubainika aliyapanga mauaji akashitaki kuwa alitukanwa kwenye mkutano wa hadhara wa chadema.
 
Waliofungua kesi wajiandae tu kuwalipa cdm ili iwe fundisho kwa vikojozi wengine wenye tabia za mwigulu
 
Kenge wanafungua kesi za kutunga mwisho wa siku anaibika.
Hivi CCM ina uhusiano gani na umbumbumbu?

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 


JUMATATU, MACHI 18, 2013 06:43 NA NATHANIEL LIMU, SINGIDA

KESI inayowakabili vigogo wawili wa CHADEMA kwa tuhuma ya kumtolea lugha ya matusi Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi, Mwigullu Chemba imeshindwa kuendelea kusikilizwa baada ya mashahidi wa upande wa mashitaka kushindwa kufika mahakamani.

Hiyo ni mara ya pili mfululizo mashahidi yao kushindwa kufika mahakamani.

Mara ya kwanza mashahidi hao wa upande wa mashitaka kushindwa kufika mahakamani, hakimu anayeisikiliza kesi hiyo, Flora Ndale aliagiza kuwa juhudi zifanyike kuhakikisha kuwa mashahidi hao wanafika mahakamani bila kukosa waweze kutoa ushahidi wao.

Ndale alisema kitendo cha mashahidi wa upande wa mashitaka kutokufika mahakamani wakati washitakiwa kutoka Dar es Salaam wanafika, ni usumbufu mkubwa kwa washitakiwa, mawakili wao na wasikilizaji.

Kesi hiyo sasa itaendelea kuunguruma Aprili 8 mwaka huu.

Vigogo hao ambao wanatuhumiwa kumtolea lugha ya matusi Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi, Mwigulu Chemba ni Waitara Mwikwabe (37) ofisa sera na utafiti makao makuu na Dk.Kitila Mkumbo mhadhiri wa Chuo Kikuu Dar es Salaam na mshauri wa CHADEMA.

Vigogo hao wanatuhumiwa kutenda kosa hilo Julai 14 mwaka jana.

Kwa mujibu wa Mwanasheria wa Serikali, Seif Ahmed washitakiwa bila halali, walimtusi Mbunge Mwigullu kuwa ni malaya, mzinzi na mpumbavu.

Seif alidai washitakiwa hao alitenda kosa hilo kwenye mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Nguvumali.

 
Back
Top Bottom