permanides
JF-Expert Member
- May 18, 2013
- 10,025
- 11,216
Hii Simba ni overrated, timu nzima ili paralyse. Defense hakuna kitu, tena refa angekuwa mkali kuna penalties mbili kazifumbia macho, kiungo kilijifia kabisa, washambuliaji wamekosa mbinu kabisa za kupasua ule ukuta. Kaizer waliwaacha Simba wacheze mpira wa kishamba wa pasi nyingi zisizokuwa na athari, wao pasi tatu tayari wako golini. Mpira ni akili ndio lakini fitness na maumbile ya wachezaji wa Kaizer yamewapa Simba shida pia. Mipira ya juu wako njema kabisa, Mikson ile jezi akiichomoa anakuwa kama kavaa gauni, kwa kimo hicho utarajie anaweza kushinda mipira ya juu?? Yule chizi wa Ghana angekuwepo, pengine mngeweza pata hata la kufutia machozi.Tupo tu.
Lawama kwanza zimuendee kocha kwa kupanga kikosi kibovu. Hakujuwa mahitaji ya mchezo na maumbile ya wachezaji wa Kaizer Chiefs.
Mechi hii haikumstahili Mkude na badala yake angecheza Nyoni au Muzamiru. Lengo lingekuwa ni kuzuia sana na mashambulizi machache ya kushtukiza. Katikati palikufa kabisa na wala hakufanya mabadiliko.
Kumkosa Morrison limekuwa ni pigo kubwa kwani hii ndio ilikuwa mechi yake kwani angejaribu kuifungua defense ya Kaizer.
Udhaifu wa mabeki simba kwenye mipira ya juu ulijidhihirika wazi kabisa na ma-forward kutokurudi kukaba.
Manula ajifunze ku-intercept cross na sio kusubiri tu mpira upigwe kichwa ndio aokoe.
Na haya madiliko ya ma- stiker wawili kwa mpigo mimi sijawahi kuyaona faida yake na mara nyingi yanadhoofisha timu tu. Striker anaweza kuwa mchezaji mwenye umbile lolote ilimradi tu awe tactical and clinical. Baada ya kumtoa Bwalya angempanga Ndemla ili aje ajaribu ma-shoot ya mbali. Na sijui ni kwa nini hajawahi kumpanga Ndemla hata mara moja.
Simba wajaribu kumpata Dube kwa bei yoyote na ndiye anayefaa kuwa striker wa Simba. Hawa wengine kusema ukweli ni miyayusho tu.
Simba waliwachukulia poa Kaizer na matokeo yake yamekuwa ni huzuni kubwa kwa mashabiki wa Simba laukama watani wamefurahia. Nao pia ubingwa ndio imetoka hiyo, wasubiri tu mbeleko. Hasira zetu tutazimalizia kwao.
Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app