Kwanza kwa aliyekuwa waziri kusema anaelimisha wanae nje bila hofu niishara kwamba hajali maslahi ya wananchi.
Out of touch.
CCM sio TANU
Masha anapaswa kushukuru kuwa kutokana na Elimu kuwa chini chuki kwa CCM ni ndogo maana kama vijana kama wangepatiwa elimu iliyobora zaidi na kuelewa tumetoka wapi na kwanini tuko hapa basi chuki ingekuwa kubwa zaidi.Na sio ajabu wangeiondoa CCM kwa style ya TunisiaCandid Scope,
Unataka kuniambia kuwa tungekuwa na elimu bora kuliko tuliyo nayo hivi sasa vijana wetu wangeshabikia CCM? I think there is more to it than simply blaming it on education. CCM imewapoteza vijana kwa sababu kimegeuka kuwa chama cha kulaghai. Angalia ahadi alizozitoa Kikwete katika uchaguzi wa 2010. Hivi kweli unaamini Kigoma itageuzwa kuwa Dubai wakati wa utawala wa Kikwete, ambao amebakiwa na miaka mitatu tu?