Masaa 18 kabla ya kifo cha gaddaf

mtundu

Member
Oct 6, 2011
22
7

KUNA mvutano kuhusu mazishi ya marehemu Kanali Muammar Gaddafi, watu wa kabila la kiongozi huyo wa zamani wa Libya, wanadai mwili wa ndugu yao ili wauzike kwa heshima, wakati Baraza la Mpito linaweka ngumu na kusisitiza kwamba atazikwa kwa siri kubwa.

Tumefanikiwa kupata historia fupi ya maisha ya Gaddafi saa 18 kabla ya kifo chake pamoja na mateso ya mwili wa kiongozi huyo ambaye neno lake, harakati zake na fedha alizomwaga katika ufadhili, ndivyo viliwezesha kuundwa kwa Umoja wa Afrika.

Jumamosi iliyopita, Mwenyekiti wa Baraza la Mpito (NTC), Mustafa Mohammed Abdul Jalil alitarajiwa kwenda jijini Misrata kutoa tamko kuhusu mazishi hayo.

Kwa mujibu wa mtu anayedaiwa alikuwa mlinzi wa Gaddafi kabla ya kumgeuka dakika za mwisho, saa 18 kabla kiongozi huyo wa zamani wa Libya kufariki dunia, alizitumia kusali na kuweka mikakati ya kuhama Jiji la Sirte.


Saa 2:30 asubuhi (saa za Libya), vikosi vya Nato na Ufaransa viliyashambulia kwa mabomu magari ya msafara wa Gaddafi. Magari 15 yaliharibiwa kwenye mashambulizi hayo, Gaddafi na timu yake walikwenda kujificha kwenye daraja la mtaro.



5:05 asubuhi, NTC ilitangaza kuwa ngome ya Gaddafi imekwisha na kilichobaki ni kutafuta masalia.



NILIPOKUWA NAPERUZI MITANDAONI.NILIFANIKIWA PIA KUYANASA MAMBO MAZURI YALIYOFANYWA NA SERIKARI YA GADDAF

1. There is *no electricity bill* in Libya; electricity is free for all its citizens.

2. There is *no interest on loans*, banks in Libya are state-owned and loans given to all its citizens at 0% interest by law.

3. *Home* considered a human right in Libya – Gaddafi vowed that his parents would not get a house until everyone in Libya had a home. Gaddafi’s father has died while him, his wife and his mother are still living in a tent.

4. All newlyweds in Libya receive *$60,000 Dinar* (US$50,000) by the government to buy their first apartment so to help start up the family.


NASHINDWA KULINGANISHA KATI YA MAZURI NA MABAYA YALIYOPELEKEA KUTESWA KIASI HIKI.SORRY!!!

RIPOTI KAMILI: <<BOFYA HAPA>>
 
imebaki stori.kwani hayo mambo aliyoyafanya alikuwa anayafanya kwa hela yake au hela ya serikali?acheni hizo.mia
 
Waliona anatumia pesa kuwadanganya ili aendelee kubaki madarakani. Kama angekuwa na akili angestaafu na kuwa Baba wa Taifa la Libya na Heshima kubwa kuliko kung'ang'ania madaraka mpaka watu wake wakamchoka.
 
imebaki stori.kwani hayo mambo aliyoyafanya alikuwa anayafanya kwa hela yake au hela ya serikali?acheni hizo.mia

wanavyojinadi CCM kwani hela zao?cha kuangalia hapo ni kwamba alitumia hela za walibya kwa faida ya walibya,Tanzania viongozi wanatumia hela za walipa kodi watanzania kwa manufaa ya mafisadi wachache.Kilichofanya Gadafi auliwe ni kuwanyima haki ya kutoa mawazo raia wake.THINK GREAT NDUGU
 
Pesa alizotumia kufanya yote hayo ni mali ya watu wa Libya
Hakuna zuri alilofanya yote yanajificha ktk mauaji ya wenzake
 
Binadamu wengi shukurani hawana nakila unachowafanyia hawatosheki,niwachache sana wanao shukuru nakukumbuka fadhila,kwnye dunia mpaka ufe ndio mchango wako unajulikana sasa huyo Marehemu anamazuri yake hakua namabaya matupu.....
 
inasikitisha sana tena sana .................... yaani hata kama ana mabaya yapi ............ndio kufuatwa nchini kwake .............kuuliwa bila heshima........
ama kweli duniani kuna ukatili .............. hivi hao waliomuua - tena naona ni vijana tu .........wao wanadhani mwisho wao ni nini???? watakutana na Gadaffi siku moja huko AKHERA...........

sijui mkewe, watoto wake waliobaki wanajisikiaje????hasa kama alivyouwawa kikatili??? jamani kwani wangempiga tu risasi bila kumpiga kwanza kma "KIBAKA" wasingetosheka???? YAANI NIMEAMINI WAARABU NI WAKATILI - NO WONDER WALIFANYA UKATILI ENZI ZA UTUMWA KUWATESA BABU NA BIBI ZETU.

Ngoja Mungu atoe hukumu!!!!!!!!!!
 
watu wengine bwana eti pindi Gaddafi ajafa anasakwa akuna taifa lolote la Afrika au kiongozi Afrika aliyepaza sauti kumtetea sasa kashakufa sifa kibao tena nzuri anamwagiwa na masikitiko juu dhidi yake acheni hizo.
 

KUNA mvutano kuhusu mazishi ya marehemu Kanali Muammar Gaddafi, watu wa kabila la kiongozi huyo wa zamani wa Libya, wanadai mwili wa ndugu yao ili wauzike kwa heshima, wakati Baraza la Mpito linaweka ngumu na kusisitiza kwamba atazikwa kwa siri kubwa.

Tumefanikiwa kupata historia fupi ya maisha ya Gaddafi saa 18 kabla ya kifo chake pamoja na mateso ya mwili wa kiongozi huyo ambaye neno lake, harakati zake na fedha alizomwaga katika ufadhili, ndivyo viliwezesha kuundwa kwa Umoja wa Afrika.

Jumamosi iliyopita, Mwenyekiti wa Baraza la Mpito (NTC), Mustafa Mohammed Abdul Jalil alitarajiwa kwenda jijini Misrata kutoa tamko kuhusu mazishi hayo.

Kwa mujibu wa mtu anayedaiwa alikuwa mlinzi wa Gaddafi kabla ya kumgeuka dakika za mwisho, saa 18 kabla kiongozi huyo wa zamani wa Libya kufariki dunia, alizitumia kusali na kuweka mikakati ya kuhama Jiji la Sirte.


Saa 2:30 asubuhi (saa za Libya), vikosi vya Nato na Ufaransa viliyashambulia kwa mabomu magari ya msafara wa Gaddafi. Magari 15 yaliharibiwa kwenye mashambulizi hayo, Gaddafi na timu yake walikwenda kujificha kwenye daraja la mtaro.



5:05 asubuhi, NTC ilitangaza kuwa ngome ya Gaddafi imekwisha na kilichobaki ni kutafuta masalia.



NILIPOKUWA NAPERUZI MITANDAONI.NILIFANIKIWA PIA KUYANASA MAMBO MAZURI YALIYOFANYWA NA SERIKARI YA GADDAF

1. There is *no electricity bill* in Libya; electricity is free for all its citizens.

2. There is *no interest on loans*, banks in Libya are state-owned and loans given to all its citizens at 0% interest by law.

3. *Home* considered a human right in Libya &#8211; Gaddafi vowed that his parents would not get a house until everyone in Libya had a home. Gaddafi's father has died while him, his wife and his mother are still living in a tent.

4. All newlyweds in Libya receive *
$60,000 Dinar* (US$50,000) by the government to buy their first apartment so to help start up the family.

NASHINDWA KULINGANISHA KATI YA MAZURI NA MABAYA YALIYOPELEKEA KUTESWA KIASI HIKI.SORRY!!!

RIPOTI KAMILI: <<BOFYA HAPA>>

Hapo kwenye red, Gaddafi aliwafanya waLibya 'mazuzu', wanae walikuwa waishi nakutumbua pesa za nchi kama hawana akili nzuri. Hiyo risasi kichwani saizi yake.
 
Pesa alizotumia kufanya yote hayo ni mali ya watu wa Libya
Hakuna zuri alilofanya yote yanajificha ktk mauaji ya wenzake

Mkuu ulitaka atumie pesa za mfukoni mwake kwa manufaa ya Wa-Libya? Watu jamani sijuwi mnafikirije lol! Sisi na dhahabu zetu , mbuga za wanyama wetu, Bandari yetu, uranium yetu, Tanzanite yetu, tunapata nini kama Watanzania? Think about that! Walibya hawakuwa na shida ya maisha kama WaTZ wanavyotaabika katika nchi iliyojaa utajiri huku mafisadi wachache wakijilimbikizia mali. The country (Libya) is beautiful, miundo mbinu ni ya uhakika. Pamoja na mabaya yake jamaa aliijenga nchi yake.
 
Mara nyingi hata kama ulikuwa mtenda mema, ukitenda baya moja tu litakumbukwa kuliko mema mengi uliyofanya.
 
it's sad indeed to see Africans fall to a western trap under the umbrella of democracy. History will judge the greedy Libyans that decided to trade their dignity with the 1 time conditional office term. How can a leader that was respected and tireless work hard for 4decades to cling libya in the forefront of dvlpt in all indices be executed in such a tormenting and inhumane tradition. I mourn for you a true revolution guard, a real African that said no to the west and prove that it is possible to use our resources effectively to achieve 1st world development. Anyone with Gadhafi's green book, please I need a copy. The 'new Iraq' that they've just created will haunt them to their graves.
 
Kitendo cha kung'ang'ania mpaka afie mjengoni ndo kilicho mponza
though nato walivaa suti wakati harusi si yao
 
Sijui baada ya Gadafi wataenda wapi wapi tena? Eee Mungu tusaidie na tupiganie sisi wanyonge,naona westerners wanatamani wawe Mungu wetu.
 
Kwa kweli atakumbukwa kwa mengi kabla ya nusu mwaka kupita pengo litaonekana si kwa libya tu bali hata nchi za africa.
 
Kwa hakika nitamlilia milele gaddafi ewe kiongozi bora ambae uliwajali wananchi wako wakawa na maisha bora kuliko taifa lolote duniani,narudia tena walibya chini ya gaddafi ndio waliokua na maisha bora namazuri kuliko binaadamu yoyote anaeishi ktk dunia hii,ila sasa walibya wataanza kula vinyesi vyao,leo tripoli hata maji ya kuchamba hakuna sembuse majiyakunywa,pia sasa libya ni taifa litakaloongozwa kwa sharia zile sheria zakiislam,pia baada ya miezi3 tu africa yote na walibya watamkumbuka gadafi kwa hali ngumu itakayowakumba ya kiuchumi.utakumbukwa milele shujaa wa libya na africa colonel gaddafi.
 
Back
Top Bottom