Yaani naonekana mimi mbaya kwa kukataa mke wangu kwenda Machame? Nilileta nyuzi juzi kati hapa, na ninavyoandika hapa wife yupo Masasi anarudi Jumatano. Sasa kuna kaka zake wamenipigia simu wamenitusi, nikatumia uungwana nikauliza kwa nini natukanwa kiasi hiki? Wakasema "wewe ni mjinga kwa nini sister umemzuia asije?" Wanadai nimedharau mila zao.
Hawa huwa wanakuja home mara nyingi sana na nawakaribisha vizuri, kifupi sina gubu ila nachukia sana matusi, hawa kaka nimekuwa nikiwaheshimu mno, ila kwa hili hapana. Mke wangu hajui chochote mpaka sasa.
Sasa uamuzi wangu ni kupiga marufuku ndugu yeyote wa mke wangu kutoka Machame kukanyaga kwangu, isipokuwa wazazi wake pekee.
Kwa ujumla ndugu zake wote wa Moshi wameungana na kaka zao kunishutumu kwa suala hili. Sasa nawaonesha rangi zangu halisi.