CHAMA Cha Matabibu wa Tiba Asili nchini (ATME). Kimesema kuendelea kuwepo kwa mabango ya waganga wa kienyeji wanaopaswa kulaumiwa ni Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa Kushindwa kuchukua hatua.
Akizungumza na Tanzania Daima Jana Jijini Dar, Mratibu wa Chama hicho Taifa Boniventure Mwalongo, alisema wizara hizi zinapaswa kulaumiwa kwa kuwa tangu kulipotolewa tamko la Uondoaji wa mabango hayo hakuna kilichofanyika.
''Kifungu cha 23 tiba asili kimeweka wazi watu wanaoweka matangazo ya kutibu kuchukuliwa sheria, lakini haifanyi hivyo, na tulitegemea baada ya tamko bungeni tungekaa pamoja na wizara husika tukajua tunashirikianaje katika kulitekeleza hili, lakini mpaka leo kimya'' alisema.
Msemaji wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Nsachris Mwamaja, alisema waliyonayo ni kutengeneza miongozo na sheria, na usimamiaji unashuka katika ngazi za halmashauri.
Source; Tanzania Daima.