Marufuku Kujadili Katiba Mtaani Huko Dodoma.

Marufuku Kujadili Katiba Mtaani Huko Dodoma.

PakaJimmy

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2009
Posts
16,202
Reaction score
8,788
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr. Rehema Nchimbi amepiga marufuku mijadala yoyote inayohusu Katiba na rasimu yake katika maeneo na viunga vyote vya mji wa Dodoma.

Aidha amepiga marufuku mikutano ya hadhara au makongamano yoyote ya Katiba kwa maelezo kwamba vitendo hivyo vitawavuruga wabunge wa Bunge la Katiba linalotarajia kuanza kesho mkoani Dodoma.

Nimejiuliza sana kuhusu marufuku hii...hivi wabunge wetu kumbe hawana hoja na misimamo kiasi kwamba wanaweza kuvurugwa na mijadala ya nje ya bunge!

Inakuwaje dola kupitia kwa Mkuu wa Mkoa inawafunga midomo waTanzania kuongelea katiba,kisa makazi yao ni Dodoma?

Je kwa enzi na miongo hii,
marufuku hii ina impact anayotarajia Mkuu huyu wa Mkoa??
Chanzo: Taarifa ya Habari ITV usiku huu.
 
Mkuu heb tulitee alichokizungumza, maana kukataza watu kujadili katiba yao ni jambo lisilo la kawaida
 
Naamini kuwa marufuku hii haijaanzia kichwani mwake, lazima kuna mtu au kundi la watu nyuma yake, ambao wamemwagiza au kumshinikiza atamke maagizo mazito kiasi hiki.
Uoga huu wa serikali dhidi ya raia wake utatufikisha?
 
Huyu mama huwa anahangaika, ningekuwa sina nidham ningesema nimwehu
 
Duuh ccm wanaweweseka.KATIBA NI YETU WATANZANIA HALAFU TUSIIJADILI.haingii akilini hata kidogo.CCM wameshafanya mchakato kuwa ni SIRI
 
Ni kati ya Wakuu wa Mikoa mashabiki na wanazi wa kutupwa wa kutupwa wa CCM. Hata kama hajatumwa anaweza kujipendekeza!
 
Natarajia kuwepo Dodoma siku chache zijazo, nitajadili rasimu ya katiba kila nitakapopata nafasi tena hadharani!
 
haya ndio matatizo ya vyeo vya kipu.mbavu, vya kupeana, vya kulipana fadhila
 
Huyu mama anataka promo kwa mwenyekiti wa chama. Basi na wabunge wasiijadili itawachanganya wananchi kwenye kura za maoni
 
Safi sana dodoma ni bunge tu ujinga mwingine marufuku.
 
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr. Rehema Nchimbi amepiga marufuku mijadala yoyote inayohusu Katiba na rasimu yake katika maeneo na viunga vyote vya mji wa Dodoma.

Aidha amepiga marufuku mikutano ya hadhara au makongamano yoyote ya Katiba kwa maelezo kwamba vitendo hivyo vitawavuruga wabunge wa Bunge la Katiba linalotarajia kuanza kesho mkoani Dodoma.

Nimejiuliza sana kuhusu marufuku hii...hivi wabunge wetu kumbe hawana hoja na misimamo kiasi kwamba wanaweza kuvurugwa na mijadala ya nje ya bunge!

Inakuwaje dola kupitia kwa Mkuu wa Mkoa inawafunga midomo waTanzania kuongelea katiba,kisa makazi yao ni Dodoma?

Je kwa enzi na miongo hii,
marufuku hii ina impact anayotarajia Mkuu huyu wa Mkoa??
Chanzo: Taarifa ya Habari ITV usiku huu.

wamelewa madaraka
 
Nafikiri amesahau kuwa huwa tunaangalia tulipojikwaa na si tulipoangukia. Wanafanya kazi bila ku reason kama mbwa kwa mabosi wao!
 
Nimeambiwa kujadili UKAWA warudi bungeni ruksa.
 
Huyu mama anataka promo kwa mwenyekiti wa chama. Basi na wabunge wasiijadili itawachanganya wananchi kwenye kura za maoni
Katiba inajadiliwa bungeni acha mibangi yako.
 
Back
Top Bottom