Mfumo kristo ni nini? Mfumo wa damu umeitwa mfumo kwa sababu damu imeenea kote mwilini. Watu wa dini ya kikristo imehodhi asassi zote za nyeti za uongozi na mamlaka katika nchi hii, sehemu zote za nguvu/maamuzi ya dola zimeshikwa na wakristo tangu uongozi wa juu ikulu mpaka kiongozi wa mtaa uongozi wote umeshikwa na mfumo kristo. Na hao walioshika hizo nyadhifa wanazitumia kuuendeleza ukristo na kukandamiza uislamu.
Friday, December 21, 2012Waislamu wamesalitiwa-Ilunga
Na Bakari Mwakangwale
Waislamu, wametakiwa kujipanga upya na kuendesha darsa za kuamshana kifikra ili kupata njia mbadala ya kujiletea maendeleo yao wenyewe. Hayo yamebainishwa na Sheikh Ilunga Hassan Kapungu, akiongea na Waislamu katika Msikiti wa Mtambani, Ijumaa ya wiki iliyopita, akizungumzia hali ya Waislamu wa Tanzania na changamoto za sasa. Alisema, maendeleo ya Waislamu yapo katika juhudi zao wenyewe, pamoja na kusalitiwa na hata kupata misukosuko ya mara kwa mara ndani na nje ya Uislamu. Sheikh Ilunga alifananisha hali ya Waislamu wa Tanzania na kisa cha Muamerika mmoja aliyepeleka kesi ya binti yake aliyebakwa katika Mahakama ya nchi hiyo, kisha ikamsaliti.
Alisema, kisa hicho kilieza kuwa wabakaji wale walihukumiwa kifungo cha siku 3, ambapo Muamerika huyo, hakuridhika na alihisi kutotendewa haki.
Alisema, Muamerika huyo aliyejulikana kwa jina la Amerigo Bonassera, aliiamini mno Serikali yake, Serikali ambayo, baada ya kujitolea mali zake na nafsi yake kuipigania na kuijenga dola yake ya Amerika, alitegemea itamtendea haki lakini badala yake ilimsaliti katika kutenda haki kwa mwanae. "Leo Waislamu Tanzania, tunasema kama alivyosema Amerigo Bonasera, Tanzania imewasaliti Waislamu kama Amerika ilivyomsaliti rai wake aliyejitolea, mali na nafsi yake lakini ilimsaliti, na kusababisha Amerigo, kuamua kuitafuta haki kwa njia ingine." Alisema.
Ilunga alisema ameleta kisa hicho kisha kuwataka Waislamu kujipanga na kuamshana kifikra kufatia historia yao nchini kuonyesha kuwa wazee wa Kiislamu walipigania Uhuru kwa kutoa mali na nafsi zao, wakitaraji kufaidi matunda ya Uhuru. Lakini badala yake tokea kupatika kwa Uhuru, Serikali zao kuanzia utawala wa awamu ya kwanza hadi sasa imekuwa haiwatendei haki Waislamu na kuonekana kama wao ni tatizo ndani ya nchi.
Akimzungumzia Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, kama kinara wa Serikali ya Tanganyika kisha Tanzania, kwa kuwasaliti Waislamu nchini, pamoja na kujitolea mali zao, muda wao na kumlea (Nyerere) Jijini Dar es Salaam, alisema mwaka 1952, kwa mara ya kwanza Nyerere, anakutana na wazee wa Dar es Salaam, akina Jumbe Tambaza, Haidari Mwinyimvua, Sheikh Suleiman Takadir, akitokea Sekondari ya Pugu. Alisema, Nyerere, wakati huo akisomesha Pugu Sekondari, alichukuliwa na Joseph Kasela Bantu, kisha kutambulishwa kwa wazee wa Dar es Salaam, kwa sababu Wazee hao muda huo, tayari walikuwa na Chama chao cha siasa, cha TAA.
"Viongozi hawa wa TAA, walimpokea kijana Nyerere, aliye Mkristo Mkatoliki, kutoka Butiama, Musoma. Tangu hapo Nyerere akawa mtoto wa Waislamu. Mshume Kiate, mbali ya kumlipa mshahara pia alitoa Nyumba yake nzima ili Nyerere akae." Alisema Ilunga.
Alisema, Nyerere mwaka 1985, alikiri moyoni kwamba, alikuwa Mkristo peke yake na hakuwa na nyumba Dar es Salaam, isipokuwa ni zile za Waislamu wa TAA. "Dossa Azizi, alinijia akaniambia Julius, wazee wanakuita, nimeenda nyumbani kwa Mzee Jumbe Tambaza, nikakuta kweli wazee wa Kiislamu watupu wananisubiri, wakaniambia tumekuita tufanye dua. Siku ya pili nafatwa tena naambiwa naitwa na Sheikh Ramia Bagamoyo." Alisema Sheikh Ilunga akinukuu maneno ya Julius Nyerere. Alisema, hutuba hiyo ambayo aliitoa Nyerere wakati anang'atuka, imefungiwa na wala hakuna chombo cha habari kinairejea hotuba hiyo, kama zinavyorejewa zingine, ikiwa ni njama za kuficha ukweli na kuharibu historia.
Sheikh Ilunga alisema kuwa, Mwalimu Nyerere akiwa Tabora, Waislamu wa mkoa huo akina Amina Bint Chande, walimpisha katika nyumba zao, huku akitumia gari ya Mzee Bilali Waikera, katika shughuli za kisiasa mkoani humo.
Alisema, maisha yote ya Nyerere na harakati zote za Uhuru, alizifanya akiwa na Waislamu, ambapo kwa Jijini Dar es Salaa, gari ya kwanza ya TANU, ilitolewa na Marehem Dossa Azizi, akimkabidhi Nyerere, kwa ajili ya harakati za Siasa.
"Muda wote wa kupigania Uhuru usalama wa Nyerere ulikuwa chini ya Waislamu, hata kudiriki kuingia naye Kanisani katika ibada zake ili kumlinda (maana Maaskofu walikuwa wakitumikia wakoloni)". Alisema Ilunga.
Sheikh Ilunga aliwataja Bw. Yusuph Chembela na Rashid Salum Mpunga, ambao walikuwa walinzi wake katika mikoa ya Kusini, na hata kudiriki kuingia nae Kanisani kumlinda, lakini alidai baada ya Uhuru, mwaka 1964, Nyerere, aliwatia kizuizini mwaka mmoja na miezi tisa. Alisema, Waislamu walitoa nafsi zao, mali zao yakiwemo majumba, magari kuzifanya kuwa mali za TANU, wakitegemea haki baada ya utawala wa mkoloni, lakini baada ya Uhuru na Nyerere kutengeneza Serikali, Waislamu wakasalitiwa.
Alisema, leo Waislamu hawajulikani hata kama wapo ndani ya nchini hii, kwani hata pale Serikali inapopanga mambo yake pamoja na kudai kuwa yenyewe haina dini, lakini pia haijali kuwa miongoni mwa makundi ya raia wake Waislamu wamo.
"Waislamu leo wanaishi kama raia wa daraja la nne katika nchi ambayo kwa sehemu kubwa wazee wao wamejitolea mali na nafsi zao, lakini Serikali haijali kama wapo na kuwa ni kikwazo cha kuyaendea mambo yao hususani ya kiibada." Alisema Ilunga. Akirejea hoja ya Askofu Gamanywa aliye ongea na kituo cha TBC 1, siku chache kabla ya sensa, kufuatia msimamo wa Waislamu kutaka kipengele cha dini kiwemo, alidai kuwa barabara zikijengwa watatumia Waislamu na Wakristo, Ilunga alisema hoja sio nani atatumia barabara hizo, bali hoja ni kwamba huduma hizo zimeelekezwa katika maeneo yapi tokea nchi hii ipate Uhuru wake. Alisema, tatizo si barabara za Waislamu au za Wakristo, bali tatizo barabara za lami na huduma bora za miundo mbinu kwa muda mrefu zipo katika mikoa yenye Wakristo wengi na hili lipo wazi halihitaji darubini.
Alisema, angalia mikoa ya Kigoma, Tabora na Kusini (Mtwara na Lindi), miaka yote hakuna barabara za uhakika, hakuna huduma bora kwa watu hao ambao wengi wao ni Waislamu, na huko kote, walikuwa bega kwa bega na Nyerere katika kupigania Uhuru, lakini alidai baada ya Uhuru wamesalitiwa.
Alisema, hivi sasa miongoni mwa walipa kodi wakubwa nchini, ni Waislamu, lakini kodi hiyo ikishalipwa, sehemu kubwa huenda kuimarisha Taasisi za Kikristo, pamoja na kuimarisha Mfumokristo
Source: AnNuur
Posted by Admin at 8:39 PM Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookNo comments:
Post a Comment
Newer Post Older Post Home
Subscribe to: Post Comments (Atom)
Zilizopendwa sana
Kitabu-Nyerere, Kanisa Katoliki na Uislam"Dola na Tatizo la udini Tanzania"
Mwalimu Julius K. Nyerere, Kanisa Katoliki na Uislam Dola na Tatizo la Udini Tanzania By Mohamed Said Utangulizi Baada ya k...
Aliyeanzisha Udini Tanzania ni Nyerere
Aliyeanzisha Udini Tanzania ni Nyerere Sheikh Hassan bin Amir katika waraka wake kwa Waislamu mwaka 1963 aliutaja udini uliokuwa unajengw...
Tujukumbushe-Waraka Maalum Kwa Wakristo Zanzibar
Ndugu zetu, Wazee wetu, Assalaam Alaaykum, UMOJA, UHURU, UADILIFU Waraka Maalum Kwa Wakristo Za...
Mauaji ya mwaka 2001-Zanzibar
Sehemu ya kwanza UTANGULIZI Utangulizi wetu unahusu mambo ya kihistoria kwa ufupi. Tunatanguliza historia kutokana na umuhimu wake wa...
Waislamu wamesalitiwa-Ilunga
Na Bakari Mwakangwale Waislamu, wametakiwa kujipanga upya na kuendesha darsa za kuamshana kifikra ili kupata njia mbadala ya kujiletea maend...
Islamic Movement and Christian Hegemony
Islamic Movement and Christian Hegemony The Rise of Muslim Militancy in Tanzania 1970 - 2000 Mohamed Said Contents Prologue ...
Rais Aboud Jumbe: Ilikuwaje chama kikampindua?PART 1
WAKATI alipokubali kuunganisha chama chake cha Afro-Shirazi (ASP) na chama cha Tanganyika African Union, Oktoba 1976, Rais wa Zanzibar, Al...
Mwembechai Killings
CHAPTER ONE Introduction Mwembechai killings: "Difficult problems, Easy answers" In every man's past there are things whic...
KITABU-SHEIKH HASSAN B. AMEIR ASH-SHIRAZI (1880-1979): HIS CONTRIBUTION TO ISLAMIC EDUCATION IN EAST AFRICA
SHEIKH HASSAN B. AMEIR ASH-SHIRAZI (1880-1979): HIS CONTRIBUTION TO ISLAMIC EDUCATION IN EAST AFRICA. Dr. Issa Haj.i Ziddy, University...
Tamko la Tanzania Christian Forum (TCF)
TANZANIA CHRISTIAN FORUM (TCF) MKUTANO MKUU WA NNE WA JUKWAA LA WAKRISTO TANZANIA (TCF) TAMKO RASMI "ATUKUZWE MUNGU JUU MBINGUNI, NA ...
Blog Archive
► 2013 (1)
► April (1)
▼ 2012 (114)
▼ December (12)
Tamko la Tanzania Christian Forum (TCF)
Matatizo ya Waislamu ni historia ya Kanisa kuishin...
Dhana ya Udugu wa kiislamu
Tufuate Uislamu kwa vitendo na siyo kwa maneno
HAKI YA KUABUDU MASHULENI
Kwa nini walengwa ni Marekani?
Tujikwamue na janga la utwaghuti
Nini Jihad na nani Mujahidina?
Jinsi Nyerere alivyotawala kimabavu
Salim, Butiku wakiri kuwepo udini nchini
Waislamu wamesalitiwa-Ilunga
Dola inavyolisaidia Kanisa kuuangamiza Uislamu
► October (3)
► August (6)
► July (10)
► June (9)
► May (5)
► April (12)
► February (57)
Wafuatiliaji
Followers
Ethereal template. Powered by Blogger.
Report photo