Sheria Ajira na Mahusiano Kazini, 2004 inatoa haki kwa mwanamke anapokuwa mjamzito kupata likizo ya uzazi yenye malipo (paid maternity leave) ya siku 84, au siku 100 kama utajifungua zaidi ya mtoto mmoja, ndani ya mzunguko mmoja wa likizo. Hata hivyo anaweza kupata siku nyingingine 84 ndani ya mzunguko mmoja endapo mtoto amekufa kabla ya kufikisha mwaka mmoja.
Suala la mwanamke anayenyonyesha kupewa nusu siku sijawahi kulisikia, ila sheria ya kazi inamtaka mwajiri kumpa mwajiriwa anayenyonyesha muda usiozidi saa mbili kila siku ili aweze kumnyonyesha mtoto. Pia mwanamke anyenyonyesha hatakiwi kufanya kazi muda wa usiku kabla ya kutimia miezi miwili tangu alipojifungua.