Maria Sarungi: Independent Candidate?

Maria Sarungi: Independent Candidate?

Kichuguu

Platinum Member
Joined
Oct 11, 2006
Posts
17,805
Reaction score
24,437
Maria Sarungi ni binti wa Mzee Profesa Philemon Sarungi aliyewahi kuwa mkurugenzi wa kitivo cha afya cha Muhimbili na baadaye kushika nyadhifa kadhaa serikalini kabla ya kusitaafu.

Mwanamama huyu ameolewa na mwanamme mwenye asili ya Ethiopia akiwa na maskani yake Dar es Salaama ambako ana biashara zake binafsi kadhaa, mojawapo ikiwa ya kutafuta warembo wa kushiriki mshindano ya Miss World ya Donald Trump. Mmoja wa warembo waliopitia katika mikono ya Maria Sarungi ni mrembo Flaviana Matata ambaye sasa hivi anang'aa sana kwenye anga za urembo huko New York Marekani.

Ingawa sijui undani wake binafsi, najua kuwa Maria Sarungi siyo mwanasiasa, bali aliteuliwa na Rais kuingia kwenye bunge la katiba ambalo limemaliza muda wake. Mchango wake kwenye bunge hilo la katiba uko wazi.

Kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja sasa, nimekuwa nafuatlia tweets zake, na kugundua kuwa ni mwanamama mwenye msimamo thabiti ambaye hajawa corrupted na party politics za vyama. Anachukua mazuri kutoka vyama vyote na kupinga mabovu ya vyama vyote.

Ingawa hatujaruhusu kuwa na independent candidates kwenye nchi hii, mtu wa aina hiyo ndiye nilikuwa ninataka ashike uskani wa kuingoza nchi hii.

Party politics zimechangia sana kuharibu nchi yetu na tunatakiwa kuachana nazo kuanzia sasa.
 
Huyu dada kusema kweli misimamo yake ya hali halisi ya nchi yetu kama ilivyo sasa na miaka ya hivi karibuni inanivutia sana (ila sijawahi kumuuliza yeye ni mwanachama wa chama kipi).

Nimejaribu kumshawishi mara nyingi agombee Ubunge jibu lake ni kwamba hilo nisahau kabisa kamwe halitatokea, ila sijakata tamaa labda anaweza kubadili mawazo.
 
Kuwa Rais wa nchi zetu hizi za kizandiki yakupasa kuwa mwanamtandao...

Hadi hapa tulipofikia sioni nchi ikiongozwa na candidate asiye na chama chochote cha siasa...
 
Kuongoza nchi bado sana huyu. Apewe wizara fulani, labda ya watoto na wanawake au ya vijana kama ipo.
 
Maria Sarungi ni binti wa Mzee Profesa Philemon Sarungi aliyewahi kuwa mkurugenzi wa kitivo cha afya cha Muhimbili na baadaye kushika nyadhifa kadhaa serikalini kabla ya kusitaafu.

Mwanamama huyu ameolewa na mwanamme mwenye asili ya Ethiopia akiwa na maskani yake Dar es Salaama ambako ana biashara zake binafsi kadhaa, mojawapo ikiwa ya kutafuta warembo wa kushiriki mshindano ya Miss World ya Donald Trump. Mmoja wa warembo waliopitia katika mikono ya Maria Sarungi ni mrembo Flaviana Matata ambaye sasa hivi anang'aa sana kwenye anga za urembo huko New York Marekani.

Ingawa sijui undani wake binafsi, najua kuwa Maria Sarungi siyo mwanasiasa, bali aliteuliwa na Rais kuingia kwenye bunge la katiba ambalo limemaliza muda wake. Mchango wake kwenye bunge hilo la katiba uko wazi.

Kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja sasa, nimekuwa nafuatlia tweets zake, na kugundua kuwa ni mwanamama mwenye msimamo thabiti ambaye hajawa corrupted na party politics za vyama. Anachukua mazuri kutoka vyama vyote na kupinga mabovu ya vyama vyote.

Ingawa hatujaruhusu kuwa na independent candidates kwenye nchi hii, mtu wa aina hiyo ndiye nilikuwa ninataka ashike uskani wa kuingoza nchi hii.

Party politics zimechangia sana kuharibu nchi yetu na tunatakiwa kuachana nazo kuanzia sasa.
Tuna mtaka RORYA kwa ticket ya ukawa.
 
Katika wanawake ninaowakubali huyu mama ni mmoja wapo,hana kashfa za kipuuzi kabisa na she is very independent, a great thinker, a patriot who put her country first before anything and she is very knowledgeable as well. Najua itakuwa ngumu kwake kushinda as independent but I admire her a lot, she is energetic woman
 
Huyu dada kusema kweli misimamo yake ya hali halisi ya nchi yetu kama ilivyo sasa na miaka ya hivi karibuni inanivutia sana (ila sijawahi kumuuliza yeye ni mwanachama wa chama kipi).

Nimejaribu kumshawishi mara nyingi agombee Ubunge jibu lake ni kwamba hilo nisahau kabisa kamwe halitatokea, ila sijakata tamaa labda anaweza kubadili mawazo.

Nakubaliana fika na Maria Sarungi,kuingia kwenye SIASA kwa nchi yetu hii ni kutafuta matusi tu.Utatafutwa undani wako mpaka kwenye chupi,badala ya watu kuangalia PERFORMANCE yako wanakuangalia maisha ya ndani.

Ni shidaaaaaaaaaaaaaaaaa kaka.
 
Hili linawezekana pia ingawaje sijawahi kumuuliza sababu ya kutotaka kufanya hivyo, maana siasa za Tanzania siku hizi zinatisha sana.

Nakubaliana fika na Maria Sarungi,kuingia kwenye SIASA kwa nchi yetu hii ni kutafuta matusi tu.Utatafutwa undani wako mpaka kwenye chupi,badala ya watu kuangalia PERFORMANCE yako wanakuangalia maisha ya ndani.

Ni shidaaaaaaaaaaaaaaaaa kaka.
 
Huyu ni another kid raised by pesa ya walalahoi she think babake alikuwa waziri na yeye anaweza kuwa nimeshawahi kutana naye IQ yake less than average. .....asitupotezee mda.
 
Katika wanawake ninaowakubali huyu mama ni mmoja wapo,hana kashfa za kipuuzi kabisa na she is very independent, a great thinker, a patriot who put her country first before anything and she is very knowledgeable as well. Najua itakuwa ngumu kwake kushinda as independent but I admire her a lot, she is energetic woman
Wengine ni wepi katika hiyo sample yako mkuu??!!!
 
Hafai hata siku moja, huyu dada namjua kindakindaki, pamoja na kwamba anapendelea kuvaa vichupi... ni swahiba mkubwa wa Zitto Kabwe na ndiye alikuwa anatembea kwenye mikoa kuomba viongozi wa CHADEMA kumkataa Mbowe.
 
Hili linawezekana pia ingawaje sijawahi kumuuliza sababu ya kutotaka kufanya hivyo, maana siasa za Tanzania siku hizi zinatisha sana.

Hii ndiyo sababu kubwa kwanini akina Mama wenye uwezo wa kuongoza wanaogopa kuingia kwenye chaguzi mbalimbali.Ukitaka kuingia huko lazima uwe na GUTS za Halima Mdee,vinginevyo utakufa kabla ya siku.

Pili yake USHIRIKINA napo ni kitu ambacho wengi wetu kinatufanya tuhofie hata kuingia kwenye uongozi wa vyama tu achilia mbali huu wa Taifa
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Sasa hivi Mkuu si akina Mama tu hata baadhi ya akina Baba wanaanza kuigwaya siasa kwa kuhofia maisha yao. Kumbuka kutaka kuharibiwa maisha yake (Lwakatare) ili tu kumchafua yeye na viongozi wengine wa juu kwa ushahidi usiokuwa na kichwa wala miguu. Angeweza kabisa kufua jela.

Hii ndiyo sababu kubwa kwanini akina Mama wenye uwezo wa kuongoza wanaogopa kuingia kwenye chaguzi mbalimbali.Ukitaka kuingia huko lazima uwe na GUTS za Halima Mdee,vinginevyo utakufa kabla ya siku.

Pili yake USHIRIKINA napo ni kitu ambacho wengi wetu kinatufanya tuhofie hata kuingia kwenye uongozi wa vyama tu achilia mbali huu wa Taifa
 
Maria Sarungi ni binti wa Mzee Profesa Philemon Sarungi aliyewahi kuwa mkurugenzi wa kitivo cha afya cha Muhimbili na baadaye kushika nyadhifa kadhaa serikalini kabla ya kusitaafu.

Mwanamama huyu ameolewa na mwanamme mwenye asili ya Ethiopia akiwa na maskani yake Dar es Salaama ambako ana biashara zake binafsi kadhaa, mojawapo ikiwa ya kutafuta warembo wa kushiriki mshindano ya Miss World ya Donald Trump. Mmoja wa warembo waliopitia katika mikono ya Maria Sarungi ni mrembo Flaviana Matata ambaye sasa hivi anang'aa sana kwenye anga za urembo huko New York Marekani.

Ingawa sijui undani wake binafsi, najua kuwa Maria Sarungi siyo mwanasiasa, bali aliteuliwa na Rais kuingia kwenye bunge la katiba ambalo limemaliza muda wake. Mchango wake kwenye bunge hilo la katiba uko wazi.

Kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja sasa, nimekuwa nafuatlia tweets zake, na kugundua kuwa ni mwanamama mwenye msimamo thabiti ambaye hajawa corrupted na party politics za vyama. Anachukua mazuri kutoka vyama vyote na kupinga mabovu ya vyama vyote.

Ingawa hatujaruhusu kuwa na independent candidates kwenye nchi hii, mtu wa aina hiyo ndiye nilikuwa ninataka ashike uskani wa kuingoza nchi hii.

Party politics zimechangia sana kuharibu nchi yetu na tunatakiwa kuachana nazo kuanzia sasa.
jamani mtu wa kusaka warembo anazungumziwa urais je mnaidharau Tanzania au mnadharau nafasi ya urais. mtu hupimwa kwa kazi yake na kwa muda mrefu sio kwenye facebook.hii mitandao ni ya wazi unafki ni mwingi. Hiii tz itajaongozwa na lundenga ama wema sepetu kama hatutajirekebisha
 
Kuongoza nchi bado sana huyu. Apewe wizara fulani, labda ya watoto na wanawake au ya vijana kama ipo.

Kumpa Wizara kwenye serikali zetu hizi za kizandiki kutamfanya abadilike kimsimamo. Atakuwa member kwenye baraza la mawaziri la kizandiki, hivyo atalazimika kushiriki kufanya maamuzi ya kizandiki. Huyu anatakiwa apate Ubunge tu ili aongeze joto kule.
 
Back
Top Bottom