Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 17,805
- 24,437
Maria Sarungi ni binti wa Mzee Profesa Philemon Sarungi aliyewahi kuwa mkurugenzi wa kitivo cha afya cha Muhimbili na baadaye kushika nyadhifa kadhaa serikalini kabla ya kusitaafu.
Mwanamama huyu ameolewa na mwanamme mwenye asili ya Ethiopia akiwa na maskani yake Dar es Salaama ambako ana biashara zake binafsi kadhaa, mojawapo ikiwa ya kutafuta warembo wa kushiriki mshindano ya Miss World ya Donald Trump. Mmoja wa warembo waliopitia katika mikono ya Maria Sarungi ni mrembo Flaviana Matata ambaye sasa hivi anang'aa sana kwenye anga za urembo huko New York Marekani.
Ingawa sijui undani wake binafsi, najua kuwa Maria Sarungi siyo mwanasiasa, bali aliteuliwa na Rais kuingia kwenye bunge la katiba ambalo limemaliza muda wake. Mchango wake kwenye bunge hilo la katiba uko wazi.
Kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja sasa, nimekuwa nafuatlia tweets zake, na kugundua kuwa ni mwanamama mwenye msimamo thabiti ambaye hajawa corrupted na party politics za vyama. Anachukua mazuri kutoka vyama vyote na kupinga mabovu ya vyama vyote.
Ingawa hatujaruhusu kuwa na independent candidates kwenye nchi hii, mtu wa aina hiyo ndiye nilikuwa ninataka ashike uskani wa kuingoza nchi hii.
Party politics zimechangia sana kuharibu nchi yetu na tunatakiwa kuachana nazo kuanzia sasa.
Mwanamama huyu ameolewa na mwanamme mwenye asili ya Ethiopia akiwa na maskani yake Dar es Salaama ambako ana biashara zake binafsi kadhaa, mojawapo ikiwa ya kutafuta warembo wa kushiriki mshindano ya Miss World ya Donald Trump. Mmoja wa warembo waliopitia katika mikono ya Maria Sarungi ni mrembo Flaviana Matata ambaye sasa hivi anang'aa sana kwenye anga za urembo huko New York Marekani.
Ingawa sijui undani wake binafsi, najua kuwa Maria Sarungi siyo mwanasiasa, bali aliteuliwa na Rais kuingia kwenye bunge la katiba ambalo limemaliza muda wake. Mchango wake kwenye bunge hilo la katiba uko wazi.
Kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja sasa, nimekuwa nafuatlia tweets zake, na kugundua kuwa ni mwanamama mwenye msimamo thabiti ambaye hajawa corrupted na party politics za vyama. Anachukua mazuri kutoka vyama vyote na kupinga mabovu ya vyama vyote.
Ingawa hatujaruhusu kuwa na independent candidates kwenye nchi hii, mtu wa aina hiyo ndiye nilikuwa ninataka ashike uskani wa kuingoza nchi hii.
Party politics zimechangia sana kuharibu nchi yetu na tunatakiwa kuachana nazo kuanzia sasa.