Marekani yaishauri CCM itafute mwafaka na CUF Zanzibar

Marekani yaishauri CCM itafute mwafaka na CUF Zanzibar

Hao Wamarekani waache unafiki

Sasa hivi Seif Yuko Bize kupigania Ukatibu Mkuu wake alioporwa kwa utoro kazini sio Urais wa Znz
 
Hao Wamarekani waache unafiki

Sasa hivi Seif Yuko Bize kupigania Ukatibu Mkuu wake alioporwa kwa utoro kazini sio Urais wa Znz
Tuombe Mungu Trump asije kututwanga kama Syria
 
Serikali ya Marekani imeishauri CCM kukaa mezani na chama cha CUF ili kumaliza mzozo wa Kisiasa uliotokana na UCHAGUZI MKUU WA OCTOBER 25 , 2015 .

Hayo yamesemwa na GREGORY SIMPKIMS , ofisa wa Masuala ya sera za kijamii na kisiasa katika ukanda wa nchi za kiafrica zilizo kusini mwa jangwa la sahara , alipoongoza ujumbe wa watu watatu kukutana na Naibu katibu mkuu wa ccm , Abdalla Juma ofisini kwake Kisiwandui .

Chanzo - Mwananchi .

Mytake - Hili suala la Dhuluma ya uchaguzi wa Zanzibar si la kitoto kama tunavyodanganywa .
Hivi hata Marekani haijui nani yuko nyuma ya migogoro ya Zanzibar na yupi wa kumuona? Kuonana na Naibu katibu mkuu wa ccm , Abdalla Juma,Kada ambae yeye mwenyewe hajitambui ambae hawashi hazimi, haongezi wala hapunguzi ni sawa na kudanganya toto. Tatizo sio CCM Zanzibar, tatizo ni mtawala Tanganyika. Kumbuka aliekuwa Naibu katibu mkuu wa ccm Ali Vuai amepoteza nafasi yake kwa kukiri tu, kuwa Maalim Seif ameshinda na apewe Serikali. Kauli hiyo ilimponza na Mtawala Tanganyika ikamsubiri akanyage ardhi ya Dodoma,machinjioni ya wana CCM Zanzibar na kumalizwa.

Kama kweli Bwana GREGORY SIMPKIMS,ofisa wa Masuala ya sera za kijamii na kisiasa au Serikali ya Trump ina utashi wa kutatua migogoro hii ya kila uchaguzi Zanzibar, basi angeonana na Rais JPM na wazo la kuitisha kura ya maoni kama wazanzibari wangependa kuendelea kubaki kwenye ukoloni wa Tanganyika au kujitenga nayo.
 
Hivi hata Marekani haijui nani yuko nyuma ya migogoro ya Zanzibar na yupi wa kumuona? Kuonana na Naibu katibu mkuu wa ccm , Abdalla Juma,Kada ambae yeye mwenyewe hajitambui ambae hawashi hazimi, haongezi wala hapunguzi ni sawa na kudanganya toto. Tatizo sio CCM Zanzibar, tatizo ni mtawala Tanganyika. Kumbuka aliekuwa Naibu katibu mkuu wa ccm Ali Vuai amepoteza nafasi yake kwa kukiri tu, kuwa Maalim Seif ameshinda na apewe Serikali. Kauli hiyo ilimponza na Mtawala Tanganyika ikamsubiri akanyage ardhi ya Dodoma,machinjioni ya wana CCM Zanzibar na kumalizwa.

Kama kweli Bwana GREGORY SIMPKIMS,ofisa wa Masuala ya sera za kijamii na kisiasa au Serikali ya Trump ina utashi wa kutatua migogoro hii ya kila uchaguzi Zanzibar, basi angeonana na Rais JPM na wazo la kuitisha kura ya maoni kama wazanzibari wangependa kuendelea kubaki kwenye ukoloni wa Tanganyika au kujitenga nayo.
Nakushukuru mkuu , na nakuahidi kuufikisha ujumbe wako huu kwa wahusika kabla ya saa 1 jioni hii .
 
Mbona Zimbabwe wameshidwa?Harakati zinadumaza maendeleo yetu pambana na maendeleo siku hazigandi huyo jamaa hawezi kuleta maendeleo hata akipewa miaka kumi
 
Seifu ndio rais wa Zanzibar
Bring back Tanganyika

Swissme
Kwa kweli Mzee Maalimu Seif kachanganyikiwa kabisa. Anaamini kabisa yeye ndiye rais wa Zanzibar na kwamba ataapishwa siku chake zijazo. Sawa sawa? Huu ni ugonjwa - psychopathic delusions. Wanaomwamini watakuwa amewaambukiza huo ugonjwa. Mzee amepata hali hii baada ya Dr Shein kufuata maelekezo aliyopewa na JPM alipotembelea Unguja baada ya Seif kumnyima mkono Shein kwenye msiba. Fedha ya ruzuku haipo tena kufuatia ugomvi wake na Lipumba. Mzee Seif hana tena pa kushika, hata safari zake za kila mwezi kwenda kutibiwa nje ya nchi zimekuwa ngumu. Kachanganyikiwa kweli kweli. Anahitaji msaada wa counselling na kumchangia gharama za matibabu yake ya nje ya nchi aliyokuwa anayapata kwa kulipiwa na serikali au kwa kutumia ruzuku ya CUF.
 
We huwa naonaga unaletaga vitu vya kinafiki sana na huwa havitokei.

Ile ya Mahakama ya ICJ-Uholanzi iliishia wapi?

Pole kwa kujidanganya na maneno yako ya mitandaoni.
Hii ni moja ya laana nchi yetu imeikumbatia,na sifikirii kama itakwisha,Mungu hapendi dhuluma
 
Kwa kweli Mzee Maalimu Seif kachanganyikiwa kabisa. Anaamini kabisa yeye ndiye rais wa Zanzibar na kwamba ataapishwa siku chake zijazo. Sawa sawa? Huu ni ugonjwa - psychopathic delusions. Wanaomwamini watakuwa amewaambukiza huo ugonjwa. Mzee amepata hali hii baada ya Dr Shein kufuata maelekezo aliyopewa na JPM alipotembelea Unguja baada ya Seif kumnyima mkono Shein kwenye msiba. Fedha ya ruzuku haipo tena kufuatia ugomvi wake na Lipumba. Mzee Seif hana tena pa kushika, hata safari zake za kila mwezi kwenda kutibiwa nje ya nchi zimekuwa ngumu. Kachanganyikiwa kweli kweli. Anahitaji msaada wa counselling na kumchangia gharama za matibabu yake ya nje ya nchi aliyokuwa anayapata kwa kulipiwa na serikali au kwa kutumia ruzuku ya CUF.
Wafuasi wa yahya Jammeh walikuwa na matusi kuliko wewe .
 
Serikali ya Marekani imeishauri CCM kukaa mezani na chama cha CUF ili kumaliza mzozo wa Kisiasa uliotokana na UCHAGUZI MKUU WA OCTOBER 25 , 2015 .

Hayo yamesemwa na GREGORY SIMPKIMS , ofisa wa Masuala ya sera za kijamii na kisiasa katika ukanda wa nchi za kiafrica zilizo kusini mwa jangwa la sahara , alipoongoza ujumbe wa watu watatu kukutana na Naibu katibu mkuu wa ccm , Abdalla Juma ofisini kwake Kisiwandui .

Chanzo - Mwananchi .

Mytake - Hili suala la Dhuluma ya uchaguzi wa Zanzibar si la kitoto kama tunavyodanganywa .
Mazungumzo yanaendelea vizuri baina CCM na CUF (Lipumba) tena yanatuma matumaini waambie hao Wamarekani
 
Back
Top Bottom