Bravo Mike
JF-Expert Member
- Apr 14, 2014
- 576
- 671
Trump ni mfanyabiashara mahiri , bado ana instincts na mentality ya kibiashara na sio ya kisiasa.. Alivyosema "America first" ina maana watu hawakumuelewa ? Hayuko tayari kupambana kuimarisha uchumi wake halafu wakati huohuo aone rasilimali ikipotea hivihivi katika kupeleka majeshi sehemu zisizomhusu kichwa wala mguu, ndio maana hotuba zake zote anafocus masuala ya kiuchumi...Saudia ni mshirika wake mkubwa lakini kamwambia usipolipia kukutunza utaporomoka in 2 weeks, so maamuzi yake yote yanalenga kuokoa gharama na kuongeza kipato, masuala ya kisiasa sijui ya uhusiano wa kimataifa usiokuwa na tija kiuchumi huwa haelewi kabisa , hajali ya jirani wala ya mshirika, refer kodi alizowaongezea washirika wake Canada, Japan, China, UK, ukuta wa Mexico, yeye anachoangalia ni pesa ( America first ) ngonjera za mahusiano ya kimataifa ni lugha asiyoielewa kabisaaaa.