Marekani kuitikisa Tanzania kwa vikwazo

Marekani kuitikisa Tanzania kwa vikwazo

Kwani MCC hawakujua kuhusu Dowans na Richmond ? Au shida ni uchaguzi sio ufisadi ? Mradi wa Symbion walitoa pesa wakati nchi inanuka na Ufisadi. Hatutaki vyama vya dini vyenye agenda ya kutugawanya na kuvunja Muungano wetu. CUF can burn in hell
Hiyo ni hatua ya mwanzo. Hiyo ni MCC.
Hatua ya pili itafuata ya "siri-kali" ya Marekani. Kama una mapepo, kimbilia kwa Maxkitimoto akusaidie.
Hasira unamalizia kwa CUF? Viongozi wake mmewakamata , wengine mnawalipia pango ya "hoteli", hivi wana ubavu wa kuwaumiza?
Rungu la EU halijashuka bado unaanza kuweweseka.
MCC vs CCM

Wakwere husema - Ukikubali kula, ukubali kuliwa.

Kwa hisani ya watu wa Marekani.
 
kwan bila marekani tutakufa njaa
japo siafik ubakaji wa demokrasia uko ZNZ lkn shobo za kuwashobokea WHITE FORKS sizipendi kinoma mbna KOREAKASKAZINI wameweza bila marekani japo wakati wanaanza kukaza uzi walibezwa sana najua HATUWEZI KUJIFANANISHA NA KOREA KASKAZINI ila zama za sasa tujitengenezee mazingila ya kujitegemea wenyewe muda ndo huu wa kujenga nchi yetu TANZANIA afrca kwa ujumla tufufuke tuache uchu wa MADALAKA wangapi wababe walikuwapo leo awapo duniani
koba
MOBUTU SESESEKO JONAS SAVIMBI SANKARA wako wapi wamefukiwa na Bado maisha yanaendelea dunia tunapita tu
Ungejua maisha wanayoishi wana nchi wa North Korea ungelia p the country is hell on earth
 
nitaona ajabu nchi kama marekani kutokufuata katiba kanuni sheria za nchi husika
Kwa nini hujaona ajabu kwa nchi kutofata katiba yake na kuamua kuikanyaga !! Toa boriti iliyo katika jicho lako kwanza kisha kibanzi katika jicho la jirani !
 
Ndio wanaweza Na wakituwekea.. Hata wanaoshabikia wataathirika, kama ni Jambo liwezekanalo lazima tujiandae, lazima tuuache ushabiki wa HapaKaziTu Na tuanze kufikiria namna gani tutaboresha Teknolojia yetu Na jamii zetu otherwise tutajutia siasa.
 
Matonya jeuri
Unalala nyumba ya tembe unakataa msaada wa bati kisa umeambiwa umtendee haki ndugu yako kwanza
Akili ya nguruwe pori
Kuku wa Zabanga....mtu baki ndio akwambie mtendee haki ndugu yako na wewe unachekelea tu...Kwenye tembe ndipo maskani mwetu twenzetu!!
 
Sasa ni kujifunga mkanda tu,maana tulizoeleshwa kuishi kibepari.

Kuishi kijamaa na kutumia vya kwetu ndio dawa ya bepari ingawa
hali hii itawaumiza sana wajamaa waliozoeshwa kuishi kibepari.

Kwa nchi huru kama Tanzania kuwekewa vikwazo na wazungu, huo
uhuru tunaouimba kila siku ni danganya toto.

Kuiwekea vikwazo nchi kama Tanzania ni sawa na kuziwekea
nchi majirani zipatazo nane.

Ninachokiona hapa ni uchokozi tu wa wazungu kwa nchi yetu
ili wasikie Mh.Rais Dr.JPM anasemaje/ana maoni gani? a.k.a
kupima upepo wa Amiri Jeshi Mkuu.





Hizi ni dalili za mwisho kabisa za kuparaganyika kwa mifumo yote inayoutegemeza mwili wako ili kuuwezesha kuwa na urari sawa wa kimwili na kiakiri.

Mmarekani hajakurupuka kufikia maamuzi ya kuinyima Tanzania misaada,maamuzi yake ni zao la kiburi cha watawala wetu waliojiapisha kubaki madarakani kwa ghalama yoyote hata kwa kuutoa uhai wa Watanzania.

CCM na serikali yake haipaswi kukimbia kivuli chake,leo hii tunadharirishwa ulimwenguni kwa kuwekwa kwenye kundi la mataifa yasiyofaa kwa sababu tu ya kiumbe kiitwacho shein,eti hicho ni mwiko kwake kuwa nje ya Ikulu.Kwamba ni bora Taifa zima liadhibiwe kuliko mahafidhina na manyang'au ya ccm kupoteza mamlaka za kuikalia Zanzibar kimabavu.

Baada ya MCC kushusha rungu lake,mmeibuka watetezi wengi mkilaani uamuzi wa MCC huku mkijitia upofu na kiburi cha kifisadi kujisahaulisha sababu zilizopelekea Taifa linyimwe huo msaada.

Kwani ni nani kati ya wapumbavu wote waliopo huko serikalini asiyejuwa kuwa ccm imepora haki ya wazanzibar kujichagulia viongozi wanaowataka?Ifike mahali tuache itikadi na tuungane kupinga jeuri za wanasiasa.Bila hofu eti zezeta moja linathubutu kutamka kuwa eti bora tule nyasi kuliko Kupokea misaada yenye masharti?Yaani mbaki madarakani kwa ghalama za Watanzania kula nyasi?

Tuwe wakweli,waliotufikisha hapa ni mainterahamwe wa ccm walioamua kujivika umungumtu na kujimilikisha Taifa letu.

Mliamua kuuminya Uhuru wa habari kwa kisingizio cha makosa ya Mtandao,kama mliona kosa la kimtandao kwa waliokuwa wanafanya Kazi ya kukusanya matokeo ya UKAWA,kwa nini hamkuliona kosa hilo kwa vijana wa IT Masaki waliokuwa wanafanya Kazi ileile iliyokuwa inafanywa na vijana wa ngome wa UKAWA?

Double standard za vyombo vya usalama ndiyo vilivyotufikisha hapa tulipo.Tusimlaumu Mmarekani kwa mapungufu yetu wenyewe,ni maamuzi ya kijinga na kipumbavu kabisa yaliyofanywa na wapumbavu wanaoongoza serikali ndiyo yaliyotufikisha hapa.

Waliopewa dhamana walipigiwa kelele watumie mamlaka waliyonayo kikatiba kuzuia uvunjaji wa demokrasia Zanzibar,lakini kwa kiburi chao na upumbavu wao,walisema kwa dharau kuwa hawaingilii ya Zanzibar,bali wapo tayari kumsambaratisha yeyote atakayeleta fyokofyoko zinazoweza kuathiri chama chao.

Tusipige kelele na kuelekeza chuki zetu kwa Mmarekani,tuangalie wapi tulipojikwaa na si pale tulipoangukia.Kigingi kilichotukwaa na kutusababishia anguko la kunyimwa msaada na Wamarekani ni ccm.Ndiyo,ni ccm kupitia kada wake Jeicher ndiyo waliotufikisha hapa tulipo.

NB:Maneno "ujinga,upumbavu na ulofa" nimeyaazima toka kwa Mh.B.W.Mkapa.Rais mstaafu wa JMT.
 
Kuku wa Zabanga....mtu baki ndio akwambie mtendee haki ndugu yako na wewe unachekelea tu...Kwenye tembe ndipo maskani mwetu twenzetu!!
a defeated person with no hope whatsoever
 
Wewe ni nani taka taka tuu...Hii nchi itasonga hata bila misaada yao..! Nendeni muishi huko marekani sasa na leo mkafanye sherehe

Mkuu jenga hoja acha viroja!! Vumilia mawazo ya wenzako na si kuwaita taka taka...
 
Sipo tayari kuvaa koti la uzalendo wa kipuuzi linalotangazwa na CCM! MCC haiuzi uhuru wa Tanzania bali inapambana na uhuni wa CCM na watu wake! Mimi simo kwa wana CCM wanaoungana kujifariji na matokeo ya uhuni wao kule Zanzibar! Hilo ni la wana CCM na kamwe msihusishe watanzania wengine!
 
Naona Tanzania imechukua nafasi ya Iliyokuwa inashikiliwa na Iran...... Viburi vingine ni Majanga.... Sasa wananchi tupate shida kisa mtu kukaa white House???????? kama najiona vile tumepigwa Pouse la Maendeleo.... Iran walibisha mwishowe wakaona Ujinga sasa na Tanzania tunaiga Ujinga kazi ipo huku Wananchi wengi elimu hatuna tunazoea kuajiliwa... na wenye elimu karibu wote wameiba mitihani... degree za pichu n.k ila tumeamua wenyewe viongozi si wakulaumiwa..... wacha tuchezee kichapo kama Zimbabwe... tutakuwa tunaenda na mabegi yaliyojaa pesa kununua mboga sokoni... Ni zaidi ya Ujinga...
 
Hizi ni dalili za mwisho kabisa za kuparaganyika kwa mifumo yote inayoutegemeza mwili wako ili kuuwezesha kuwa na urari sawa wa kimwili na kiakiri.

Mmarekani hajakurupuka kufikia maamuzi ya kuinyima Tanzania misaada,maamuzi yake ni zao la kiburi cha watawala wetu waliojiapisha kubaki madarakani kwa ghalama yoyote hata kwa kuutoa uhai wa Watanzania.

CCM na serikali yake haipaswi kukimbia kivuli chake,leo hii tunadharirishwa ulimwenguni kwa kuwekwa kwenye kundi la mataifa yasiyofaa kwa sababu tu ya kiumbe kiitwacho shein,eti hicho ni mwiko kwake kuwa nje ya Ikulu.Kwamba ni bora Taifa zima liadhibiwe kuliko mahafidhina na manyang'au ya ccm kupoteza mamlaka za kuikalia Zanzibar kimabavu.

Baada ya MCC kushusha rungu lake,mmeibuka watetezi wengi mkilaani uamuzi wa MCC huku mkijitia upofu na kiburi cha kifisadi kujisahaulisha sababu zilizopelekea Taifa linyimwe huo msaada.

Kwani ni nani kati ya wapumbavu wote waliopo huko serikalini asiyejuwa kuwa ccm imepora haki ya wazanzibar kujichagulia viongozi wanaowataka?Ifike mahali tuache itikadi na tuungane kupinga jeuri za wanasiasa.Bila hofu eti zezeta moja linathubutu kutamka kuwa eti bora tule nyasi kuliko Kupokea misaada yenye masharti?Yaani mbaki madarakani kwa ghalama za Watanzania kula nyasi?

Tuwe wakweli,waliotufikisha hapa ni mainterahamwe wa ccm walioamua kujivika umungumtu na kujimilikisha Taifa letu.

Mliamua kuuminya Uhuru wa habari kwa kisingizio cha makosa ya Mtandao,kama mliona kosa la kimtandao kwa waliokuwa wanafanya Kazi ya kukusanya matokeo ya UKAWA,kwa nini hamkuliona kosa hilo kwa vijana wa IT Masaki waliokuwa wanafanya Kazi ileile iliyokuwa inafanywa na vijana wa ngome wa UKAWA?

Double standard za vyombo vya usalama ndiyo vilivyotufikisha hapa tulipo.Tusimlaumu Mmarekani kwa mapungufu yetu wenyewe,ni maamuzi ya kijinga na kipumbavu kabisa yaliyofanywa na wapumbavu wanaoongoza serikali ndiyo yaliyotufikisha hapa.

Waliopewa dhamana walipigiwa kelele watumie mamlaka waliyonayo kikatiba kuzuia uvunjaji wa demokrasia Zanzibar,lakini kwa kiburi chao na upumbavu wao,walisema kwa dharau kuwa hawaingilii ya Zanzibar,bali wapo tayari kumsambaratisha yeyote atakayeleta fyokofyoko zinazoweza kuathiri chama chao.

Tusipige kelele na kuelekeza chuki zetu kwa Mmarekani,tuangalie wapi tulipojikwaa na si pale tulipoangukia.Kigingi kilichotukwaa na kutusababishia anguko la kunyimwa msaada na Wamarekani ni ccm.Ndiyo,ni ccm kupitia kada wake Jeicher ndiyo waliotufikisha hapa tulipo.

NB:Maneno "ujinga,upumbavu na ulofa" nimeyaazima toka kwa Mh.B.W.Mkapa.Rais mstaafu wa JMT.

Tatizo uwa sichanganyi siasa na matukio,kwanza angalia nilipost lini hilo bandiko langu.
Suala la uchaguzi wa Zanzibar kila mtu anajua na hata Mzee Maaalim Seifu Sharifu anajua ya
kuwa ilikuwa vigumu sana kwa wao kuwaondoa madarakani wanamapinduzi kupitia box la kura.

Wanachokifanya Waamerika ni kuudanganya tu ulimwengu kwamba na wao wana sauti juu ya kile
kinachoitwa demokrasia,lakini ukweli ni kuwa hakuna demokrasia katika nchi zilizopata uhuru wake
kupitia mapinduzi.

Sio lazima tukubali misaada ya kutugawa na kuingiza demokrasia ambayo kwa miaka zaidi ya 20
imezidi kutuletea shida na kutujengea chuki baina yetu.

Ukoloni mamboleo isiwe tatizo la kuwanyenyekea mabepari,kwani sio lazima kuishi kibepari wakati
mwingine hata kuishi kijima ni sawa tu ili mradi utu na heshima yetu tunailinda.

Tatizo mswahili ukimzoesha dezo/misaada kutwa kucha yeye ni kukenua meno nje na kujisahau nini
wajibu wake,na matokeo yake ni kubweteka na hata pale anapopata dezo/misaada hiyo uwasahau
wenye njaa,maskini na wanyonge na kuishia kuifuja.

Misaada kwa nchi za Afrika ni aibu,kamwe tusiishabikie kwani inatushushie heshima na utu wetu.
 
MAREKANI INATARAJIWA KUTANGAZA VIKWAZO ZAIDI KWA ZANZIBAR IKIWA NI PAMOJA NA "TRAVEL BAN" KWA VIONGOZI WA SERIKALI YA ZANZIBAR NA KUZUILIWA NA MALI ZA ZANZIBAR ZILIZOPO MAREKANI (ACCOUNT ZA PBZ).

Taifa la Marekani linatarajia kushusha rungu la aina yake kwa serikali ya Tanzania kufuatia hali ya sintofahamu inayoendelea nchini kutokana na sakata la uchaguzi mkuu wa Zanzibar.

Habari zinadokeza kuwa taifa hilo kubwa duniani litaweka vikwazo vya kiuchumi kwa Tanzania hali itakayopelekea Tanzania kuandika historia nyingine mbaya mbele ya uso wa dunia.
Serikali ya Marekani tayari imezuia misaada mbalimbali kwa Tanzania na pia ndiyo iliyoshinikiza Tanzania kunyimwa fedha za MCC. Hata hivyo serikali ya Tanzania bado haijatilia maanani jambo hilo huku ikioneknana kupuuza juhudi za kimataifa kuitaka kuumaliza kwa haraka mgogoro wa Zanzibar unaofukuta kwa kuacha haki ichukue mkondo wake.

Habari zinadokeza kuwa balozi wa Marekani nchini atatoa msimamo unaoelezwa kuwa 'mkali' ili kuishinikiza serikali ya Tanzania kuheshimu maamuzi ya wananchi kwenye uchaguzi mkuu wa Zanzibar uliofanyika mwezi october mwaka jana ambao ulielezwa kuwa huru na wa haki.

Chanzo : Mwandishi Wetu-AF
 
Badala ya kutukwaza wata kwazika wao.....njia yao imejaa giza na utelezi...hii ni era nyingine dunia inaenda kushuhudia jinsi tutakavyoenda kuendelea pasipo usaidizi na badala ya kuomba watatuomba wao wawe washirika wetu....

The power hand is changed kama wanadhani ni hadith let them be!
 
mkuu huwezi ifananisha Korea kaskazini na TZ, korea asilimia kubwa ya bidhaa zao wanazalisha wenyewee, ni vitu vichache sana wanaagiza toka nje.

Sisi chakula chenyewe tunacholima hakitoshi kutulisha wote.

Dola ikianza kupaa kwa hivi vikwazo ndipo utajua uchumi wa dunia umeshikiliwa na mataifa makubwaa

Hivi more than 80% ambao hawana hakika na kula yao ya kesho wanatikiswa na nini, wao hawana pa kwenda zaodi ya hapo walipo.....tutatikisika sisi cry babies (elites tuliosoma bila kuelimika ( mpaka akili zikae sawa tujikute tunatumia akili kujenga uchumi wetu badala ya kuwa tegemezi.
 
Hiyo ni hatua ya mwanzo. Hiyo ni MCC.
Hatua ya pili itafuata ya "siri-kali" ya Marekani. Kama una mapepo, kimbilia kwa Maxkitimoto akusaidie.
Hasira unamalizia kwa CUF? Viongozi wake mmewakamata , wengine mnawalipia pango ya "hoteli", hivi wana ubavu wa kuwaumiza?
Rungu la EU halijashuka bado unaanza kuweweseka.
MCC vs CCM

Wakwere husema - Ukikubali kula, ukubali kuliwa.

Kwa hisani ya watu wa Marekani.
Kama ni misaada tushapewa sana nchi ndio kwanza inazidi kuwa maskini. Nchi haina maji umeme dawa watoto wetu wanakaa chini mashuleni hio misaada inatusaidia nini ? Wamerakani washaweka wazi wala hawafichi nia yao ni kuhakikisha makampuni yao yanatawala sector ya energy Africa. Nenda website ya MCC yote yameandikwa. Kina Kagame wanaua watu Congo na misaada bado wanapewa ndio sembuse sisi ? CUF chama cha kidini nia yao ni kuvunja muungano watuletee mambo ya Libya. Hawana sera za Maendeleo kazi kulaumu Muungano
 
Back
Top Bottom