Mathanzua
JF-Expert Member
- Jan 4, 2017
- 15,866
- 20,723
COMMISSION TO EXPOSE EVIL
So do not be afraid of them, for there is nothing concealed that will not be disclosed or hidden that will not be made known. What I tell you in the dark, speak in the daylight; what is whispered in your ear, proclaim from the roofs. Do not be afraid of those who kill the body but cannot kill the soul. Rather, be afraid of the One who can destroy both soul and body in hell”. Jesus Christ – Gospel of Mathew, 10,26-28
Urusi inaishutumu Marekani kwa kuwatumia watu wa Afrika kufanya utafiti wa kibiolojia
07 November 2023
Wizara ya Ulinzi ya Urusi imeishutumu Marekani kwa kufanya utafiti haramu wa kibiolojia kwa kutumia watu wa Afrika kama Guineapigs au "rasilimali ya kliniki isiyo na malipo."Mkuu wa Kikosi cha wanajeshi wa kikosi cha silaha za kijeshi cha ulinzi wa kinga ya nyuklia, kemikali na kibayolojia Luteni Gavana Igor Kirillov alisema kuwa majaribio haya "haramu" yanafanyika nchini Nigeria na nchi zingine za Kiafrika.Kirillov pia alishutumu Marekani kwa kuhamisha miradi ya utafiti was silaha za kibiolojia kutoka Ukrainia hadi Afrika, Ulaya Mashariki na Kusini Mashariki mwa Asia,kwa kisingizio cha mipango ya afya ya umma.
Alisema kuwa mkataba wa miaka mitatu kati ya Shirika la Kupunguza Tishio la Ulinzi la Marekani (DTRA) na Shirika Lisilo la Kibiashara la RTI International uliotiwa saini Agosti iliyopita kwa ajili ya kufuatilia magonjwa ya kuambukiza nchini Nigeria, kwa kweli ni sehemu ya shughuli pana zaidi za "kijasusi za kibayolojia".
Miongoni mwa shughuli ambazo Wizara hiyo inashutumu Marekani ni "kuchambua hali ya janga la silaha za kibayolojia kwenye mipaka ya wapinzani wa kijiografia na katika maeneo yanayotarajiwa kupelekwa wanajeshi."
Krillov ameendelea kudai kuwa Urusi ina uthibitisho kwamba Marekani inachunguza hali ya "tishio la silaha za kibayolojia
Iraq, Afghanistan,China, Türkiye, Pakistan na Saudi Arabia," lakini hii ni kisingizio tu cha kupanga uharibifu.
Kulingana na Kirillov, mradi wa kibayolojia ambao lengo lake lilitajwa kuwa ni kupambana na VVU na UKIMWI nchini Nigeria.Lengo hili linawaweka Waafrika katika hatari kubwa.Utafiti huu unaelekezwa kwa wale ambao wamepewa tiba ya kuzuia virusi kutoka kwa kampuni ya dawa ya Gilead Sciences. Alisema kuwa Gileadi ina uhusiano na Pentagon na imejaribu dawa kwa Waukraine hapo awali na kusema kuwa kwa sasa wanafanya vivyo hivyo kwa watu wa Afrika. Alisema kuwa asilimia 60 ya Wanigeria walio na VVU na UKIMWI wanapokea dawa hizo, lakini hazifanyi kazi,ikithibisha kuwa lengo lake ni lingine kabisa.
"Pamoja na ongezeko la ufadhili wa kila mwaka wa takriban dola milioni 100, kiwango cha maambukizi ya VVU kimebakia bila kubadilika kulingana na takwimu za 2009. Vifo miongoni mwa watu walioambukizwa VVU pia vinaonyesha kuongezeka,” alibainisha.
Hilo limemfanya ahitimishe hivi: “Dawa za Kimarekani, hata pamoja na ongezeko lililothibitishwa la matumizi nchini Nigeria, hazina faida za kimatibabu zinazoonekana, na raia wa Nigeria wanatumiwa vibaya kama ‘rasilimali ya kliniki bila malipo au Guineapigs."
Kulingana na Urusi, Pentagon inatumia fursa ya afya mbaya ya umma barani Afrika ili kuweza kukusanya takwimu kwa nia ovu na kusafirisha sampuli mbalimbali kwa kutumia mawakala wake ili kuleta maambukizi.
Urusi imesema kuwa baadhi ya miradi imefanywa ili kuepusha tuhuma dhidi ya Pentagon. Kwa mfano wanasema kwamba upo utafiti uliofanywa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Afghanistan kwa niaba ya Marekani wa kuchunguza vimelea hatari kama vya Kimeta na kukusanya sampuli za kibayolojia huko Afghanistan na kuzileta U.S.
America ina historia ovu sana ya kutumia watu wa Kiafrika kwa majaribio ya kimatibabu,kwa hiyo lazima nchi za Afrika,Amerika ya Kusini na Asia ziwe makini sana.
Mamlaka nchini Nigeria na Marekani hata hivyo zimekanusha madai haya na kusisitiza kuwa
wao wanasaidia kuzuia magonjwa na kulinda afya ya umma. Kukanusha huku hata hivyo kulitegemewa.
Ingawa madai haya bado hayajathibitishwa na taasisi zingine huru,hata hivyo zinaweza kuwa na ukweli mkubwa ikizingatiwa kuwa Marekani ina historia ndefu na ya uovu wa kufanya majaribio ya kimatibabu na eugenics kwa Waamerika wenye asili ya Afrika, ambao mara nyingi walitumiwa kama “Guineapigs” na kufanyiwa majaribio mabaya na kuambukizwa magonjwa ili kutafuta matibabu mapya na hata virtual extremination.Kujua kiwango cha uovu wa Marekani mtu anahitaji tu kuona yale yanayo-tokea Ukraine na Gaza sasa.