kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 9,000
- 17,909
Mwanasiasa mwingine akiri: Marekani iliunda kundi la kigaidi la ISIS (Daesh)
Apr 21, 2023 08:22 UTC
[https://media]
Mwanasiasa wa Marekani ambaye ametangaza nia yake ya kugombea katika uchaguzi wa urais mwaka ujao, amekiri kwamba nchi hiyo ndiyo iliyounda kundi la kigaidi la Daesh (ISIS).
Robert F. Kennedy Jr mwenye umri wa miaka 69, mpwa wa rais wa zamani wa Marekani, John F. Kennedy , amesema kwamba: "Polisi wa nchi hii ni wafisadi, tulitengeneza kundi la kigaidi la ISIS na tumetuma wakimbizi milioni 2 Ulaya na kuyumbisha demokrasia barani humo, hali iliyosababisha Brexit na kujiondoa Uingereza katika umoja wa Ulaya."
Mwanasiasa huyo wa chama cha Democratic na mpinzani wa Joe Biden ameongeza kuwa, hii ni sehemu ya gharama za vita vya Iraq vilivyotumia jumla ya dola trilioni 24.
[https://media]Robert F. Kennedy
Kennedy amesisitiza kuwa, gharama hizo hazikuwa na faida yoyote isipokuwa uharibifu kwa tabaka la kati la Marekani na kuna ulazima wa kukomeshwa hali hii.
Mwanasiasa huyo wa Marekani amekosoa sera ya kigeni ya nchi hiyo akakiri kwamba mkakati wa Marekani siku zote umekuwa kutumia silaha za kijeshi kwa ajili ya kutunisha misuli duniani kote.
Zaidi ya miaka ishirini iliyopita, Machi 20, 2003, George W. Bush, rais wa zamani wa Marekani, aliamuru mashambulizi dhidi ya Iraq bila idhini ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na kinyume cha sheria kwa ushirikiano Waziri Mkuu wa Uingereza, Tony Blair.
Mashambulizi na uvamizi wa Marekani na Uingereza dhidi ya Iraq ulipelekea kuuawa malaki ya raia wasio na hatia wa nchi hiyo.
Itakumbukwa kuwa awali aliyekuwa rais wa Marekani, Donald Trump pia alikiri kuwa nchi hiyo ndiyo iliyounda na kuazisha kundi la kigaidi la Daesh lililofanya mauaji ya kutisha na jinai zisizo na mfano katika nchi kama Iraq na Syria.
Apr 21, 2023 08:22 UTC
[https://media]
Mwanasiasa wa Marekani ambaye ametangaza nia yake ya kugombea katika uchaguzi wa urais mwaka ujao, amekiri kwamba nchi hiyo ndiyo iliyounda kundi la kigaidi la Daesh (ISIS).
Robert F. Kennedy Jr mwenye umri wa miaka 69, mpwa wa rais wa zamani wa Marekani, John F. Kennedy , amesema kwamba: "Polisi wa nchi hii ni wafisadi, tulitengeneza kundi la kigaidi la ISIS na tumetuma wakimbizi milioni 2 Ulaya na kuyumbisha demokrasia barani humo, hali iliyosababisha Brexit na kujiondoa Uingereza katika umoja wa Ulaya."
Mwanasiasa huyo wa chama cha Democratic na mpinzani wa Joe Biden ameongeza kuwa, hii ni sehemu ya gharama za vita vya Iraq vilivyotumia jumla ya dola trilioni 24.
[https://media]Robert F. Kennedy
Kennedy amesisitiza kuwa, gharama hizo hazikuwa na faida yoyote isipokuwa uharibifu kwa tabaka la kati la Marekani na kuna ulazima wa kukomeshwa hali hii.
Mwanasiasa huyo wa Marekani amekosoa sera ya kigeni ya nchi hiyo akakiri kwamba mkakati wa Marekani siku zote umekuwa kutumia silaha za kijeshi kwa ajili ya kutunisha misuli duniani kote.
Zaidi ya miaka ishirini iliyopita, Machi 20, 2003, George W. Bush, rais wa zamani wa Marekani, aliamuru mashambulizi dhidi ya Iraq bila idhini ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na kinyume cha sheria kwa ushirikiano Waziri Mkuu wa Uingereza, Tony Blair.
Mashambulizi na uvamizi wa Marekani na Uingereza dhidi ya Iraq ulipelekea kuuawa malaki ya raia wasio na hatia wa nchi hiyo.
Itakumbukwa kuwa awali aliyekuwa rais wa Marekani, Donald Trump pia alikiri kuwa nchi hiyo ndiyo iliyounda na kuazisha kundi la kigaidi la Daesh lililofanya mauaji ya kutisha na jinai zisizo na mfano katika nchi kama Iraq na Syria.