Marehemu achaguliwa uongozi wa tawi CCM!

Kama kun mwana-ukoo yeyote yule na huyo marehemu basi akapewe urithi hicho kiti cha CCM maana ni ngekewa kwa ukoo wao kuongoza hata baada ya kwenda ahera.

Kwahiyo akina Rejao, ritz wazeekee huku mtandaoni!?
 
Filipo kama ulichoandika ni kweli basi hii itakuwa kali ya kufungia mwaka lol....ndo kusema wameishiwa au???.... inasikitisha sana!
 
Last edited by a moderator:
Marehemu walipokuwa hai walikuwa wanachama wa CCM. Sasa waliobaki hai hakuna mwanachama na hawaitaki tena CCM. Njia pekee iliyosalia, ni kuwarehemu marehemu...na kuendeleza kazi zao nzuri za kukitumikia CCM. Kwa vile walifariki wakiwa CCM, si vibaya matendo yao yakiendelea kutukuzwa kwa kuendelea kupewa uongozi ndani ya CCM! ndo njia pekee ya kuenzi kazi za marehemu kichama - kiccm!
 
Kha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha hahaaaaa!!

Jamani sisiem kwishiliyaa mbali sasa!
Imebakia kuteuwa marehemu jamani!
Kweli sisiem ni janga kwa Taifa letu la Maziwa na Asali!

Kuzaliwa ni 1977
Kufa zika ni 2015

Itabaki historia ya kwamba tulikuwa na chama kinaitwa chichiem!

Kudadekiiiiiii!
 
Manumbu umenichekesha sana...lol eti kuwarehemu marehemu hahahahahah!!!!!!! .....kuishiwa kubaya jamani daaah... ccm bana wametia fora.
 
Last edited by a moderator:
Filipo kama ulichoandika ni kweli basi hii itakuwa kali ya kufungia mwaka lol....ndo kusema wameishiwa au???.... inasikitisha sana!

kwakweli inaleta mshangao na maswali mengi kuliko majibu!
 
Last edited by a moderator:
Manumbu umenichekesha sana...lol eti kuwarehemu marehemu hahahahahah!!!!!!! .....kuishiwa kubaya jamani daaah... ccm bana wametia fora.

ndicho walichosalia kukifanya kwa kweli. naamini ukiwakuta kwenye vikao vyao vile vya ndani kwa ndani, watakuwa wamenuniana kishenzi. kila mtu kamkasirikia mwenzie, lawama juu ya lawama, laana juu ya laana! wala hawatazamani machoni. na bado. tutasikia wamerushiana makonde kwenye vikao vyao....tuombe uhai tu. tutayaona yote towards kifo cha CCM!!!!!
 

Ni kweli unachosema......kiukweli huko hali zao ni mbaya na ndio mana mpaka wanachanganyikiwa (wanarehemu marehemu lol..... source Manumbu)
 
Last edited by a moderator:

Unajua wakati mwingine wana JF wananishangaza sana,taratibu za uchaguzi siku zote zinajulikana iwe ngazi ya ujumbe wa nyumba kumi mpaka Taifa,sasa huyo Marehemu alijinadi vipi na wakati gani mpaka wapiga kura wakampigia kura?,vitu vingine (hasa visivyowezekana) siyo tunapokea tu na kushadadia tutakuja kushadadia mpaka vyenye madhara
 

Mkuu, hapa tunaleta habari na kuijadili as great thinkers. Nimeweka na source ili kuondoa utata. Sasa kama haikuingii akilini, unatakiwa kuichallenge source! Fungua web ya ipp ulisome hilo gazeti ili upate habari kwa kina! Maneno ya mipasho, sijui kushadadia i'm not used to! Very sorry.
 
Mkuu, mbona hata huko kumejaa akina Nyerere, Sokoine, Kawawa na viongozi wengine wengi tu!

ccm wamebaki wanafanya warm up, kwa kuchagua maiti kuwa kiongozi. Wanajua mwisho wao umefika. Zamani watu walikuwa wanagombania ubalozi wa nyumba 10, lakini leo hawataki hata kwa gharama yoyote. Kuishabikia ccm inatakiwa uwe na akili za maiti.
 

sisi kule kwetu tuliwahi kumchagua diwani aliyefungwa jela miaka 12. Inawezeka mazee usishangae
 

Ila uko used na habari za Wafu kupigiwa kura?
Ukiwa ni sehemu ya Jamii ya Great Thinkers unatakiwa upime na habari yenyewe, je inafanana na uhalisia? siyo ksbb imeandikwa kwenye gazeti na wewe ume'quote source basi ndo tujadili,kuna vitu vya kujadili na vingine siyo vya kujadili,mimi na akili zangu siwezi kujadili "lisilowezekana" kama hilo,jadilini wenyewe...
 

point ni kwamba ccm wamekosa watu wa kuziba pengo. Ndiyo maana wakaamua kulizipa kwa jina la marehemu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…